Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Wednesday 5 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 49....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Kisha Mafarisayo na waalimu wa sheria wakafika kutoka Yerusalemu, wakamwendea Yesu, wakamwuliza, “Kwa nini wanafunzi wako hawajali mapokeo tuliyopokea kwa wazee wetu? Hawanawi mikono ipasavyo kabla ya kula!”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako

Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Yesu akawajibu, “Kwa nini nanyi hamjali sheria ya Mungu ila mnapendelea mapokeo yenu wenyewe? Mungu amesema: ‘Waheshimu baba yako na mama yako,’ na ‘Anayemtukana baba yake au mama yake, lazima auawe.’
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Lakini nyinyi mwafundisha ati mtu akiwa na kitu ambacho angeweza kumsaidia nacho baba yake au mama yake, lakini akasema: ‘Kitu hiki nimemtolea Mungu,’ basi, hapaswi tena kumheshimu baba yake! Ndivyo mnavyodharau neno la Mungu kwa kufuata mafundisho yenu wenyewe. Enyi wanafiki! Isaya alitabiri sawa kabisa juu yenu:
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.


Waamoni

1Kuhusu Waamoni.
Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Je, Israeli hana watoto?
Je, hana warithi?
Mbona basi mungu Milkomu amemiliki Gadi
na watu wake kufanya makao yao mijini mwake?
2Basi, wakati unakuja kweli, siku zaja,
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
ambapo nitavumisha sauti ya vita
dhidi ya Raba mji wa Waamoni.
Raba utakuwa rundo la uharibifu,
vijiji vyake vitateketezwa moto;
ndipo Israeli atakapowamiliki wale waliomiliki.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
3“Ombolezeni, enyi watu wa Heshboni,
maana mji wa Ai umeharibiwa!
Lieni enyi binti za Raba!
Jifungeni mavazi ya gunia viunoni
ombolezeni na kukimbia huko na huko uani!
Maana mungu Milkomu atapelekwa uhamishoni,
pamoja na makuhani wake na watumishi wake.
4Mbona mnajivunia mabonde yenu, enyi msioamini,
watu mliotegemea mali zenu, mkisema:
‘Nani atathubutu kupigana nasi?’
5Basi, mimi nitawaleteeni vitisho
kutoka kwa jirani zenu wote,
nanyi mtafukuzwa nje kila mtu kivyake,
bila mtu wa kuwakusanya wakimbizi.
Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.
6Lakini baadaye nitawarudishia Waamoni fanaka yao.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
Edomu
7Kuhusu Edomu.
Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:
“Je, hakuna tena hekima mjini Temani?
Je, wenye busara wao hawana shauri tena?
Hekima imetoweka kabisa?
8Kimbieni enyi wakazi wa Dedani;
geukeni mkaishi mafichoni!
Maana nitawaleteeni maangamizi
enyi wazawa wa Esau;
wakati wa kuwaadhibu umefika.
9Wachuma zabibu watakapokuja kwenu
hawatabakiza hata zabibu moja.
Usiku ule wezi watakapofika,
wataharibu kila kitu mpaka watosheke.
10Lakini nimemnyanganya Esau kila kitu,
naam, nimeyafunua maficho yake,
wala hawezi kujificha tena.
Watoto, ndugu na jirani zake wameangamizwa;
hakuna hata mmoja aliyebaki.
11Niachieni watoto wenu yatima nami nitawatunza;
waacheni wajane wenu wanitegemee.”
12Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Ikiwa wale ambao hawakustahili kunywa kikombe cha adhabu ni lazima wanywe, je, wewe utaachwa bila kuadhibiwa? La! Hutakosa kuadhibiwa; ni lazima unywe hicho kikombe! 13Maana nimeapa kwa nafsi yangu kwamba mji wa Bosra utakuwa kioja na kichekesho, utakuwa uharibifu na laana; vijiji vyote vitakuwa magofu daima. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”
14Nimepata habari kutoka kwa Mwenyezi-Mungu,
mjumbe ametumwa ayatangazie mataifa:
“Jikusanyeni pamoja dhidi ya Edomu;
inukeni mwende kuushambulia!
15Mimi Mwenyezi-Mungu nitakufanya wee Edomu
kuwa mdogo kuliko mataifa yote.
Ulimwengu wote utakudharau.
16Vitisho unavyotoa na kiburi chako vimekudanganya,
ewe ukaaye katika mapango ya miamba,
unayeishi juu ya kilele cha mlima!
Ingawa unaweka makao yako juu kama ya tai,
mimi nitakuporomosha kutoka huko uliko.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
17“Edomu itakuwa kitisho na kila mtu atakayepita karibu yake atashangaa, na kuizomea kwa sababu ya maafa yatakayoipata. 18Kama vile Sodoma na Gomora na miji jirani yake ilivyoangamizwa, mimi Mwenyezi-Mungu nasema, hakutakuwa na mtu yeyote atakayeishi Edomu wala kufanya mashauri humo. 19Kama vile simba anavyochomoza kutoka msitu wa mto Yordani na kuingia kwenye malisho mazuri, ndivyo nitakavyowafukuza ghafla Waedomu kutoka nchi yao. Nami nitamweka huko kiongozi yeyote nitakayemchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani awezaye kunishtaki? Ni mchungaji gani awezaye kunipinga? 20Kwa hiyo, sikilizeni mpango ambao mimi Mwenyezi-Mungu nimepanga dhidi ya Edomu pamoja na mambo niliyokusudia kuwafanyia wakazi wa Temani: Hakika, watoto wao wadogo wataburutwa na kuchukuliwa; kweli kutakuwa na mshangao mkubwa katika makao yao! 21Kwa kishindo cha kuanguka kwao, dunia itatetemeka; sauti ya kilio chao itasikika mpaka bahari ya Shamu. 22Tazama, adui atapanda juu na kuruka kama tai na kutandaza mabawa yake juu ya Bosra. Siku hiyo moyo wa mashujaa wa Edomu utakumbwa na hofu kama ya mwanamke anayejifungua.”
Damasko
23Kuhusu Damasko:
“Miji ya Hamathi na Arpadi, imejaa wasiwasi
kwa kufikiwa na habari mbaya;
mioyo ya watu wake inayeyuka kwa hofu,
imefadhaika kama bahari isiyoweza kutulia.
24Watu wa Damasko wamekufa moyo;
wamegeuka wapate kukimbia;
hofu kubwa imewakumba,
uchungu na huzuni vimewapata,
kama mwanamke anayejifungua
25Ajabu kuachwa kwa mji maarufu,
mji uliokuwa umejaa furaha!49:25 Baadhi ya tafsiri za zamani: Umejaa furaha: Kiebrania furaha yangu.
26Basi vijana wake wataanguka viwanjani mwake,
askari wake wote wataangamizwa siku hiyo.
Mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nimesema.
27Nitawasha moto katika kuta za Damasko,
nao utateketeza ngome za mfalme Ben-hadadi.”
Makabila ya Kedari na Hazori
28Kuhusu Kedari na falme za Hazori ambazo Nebukadneza mfalme wa Babuloni, alizishambulia na kuzishinda, Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Inuka uende kulishambulia kabila la Kedari!
Waangamize watu wa mashariki!
29Hema zao na kondoo wao vitachukuliwa,
kadhalika mapazia yao na mali yao yote;
watanyanganywa ngamia wao,
na kilio kitasikika: ‘Kitisho kila upande!’
30Kimbieni, nendeni mbali, kaeni mashimoni.
Enyi wakazi wa Haziri,
kimbieni mtangetange na kukaa mafichoni!
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Maana Nebukadneza mfalme wa Babuloni,
amefanya mpango dhidi yenu,
amepania kuja kuwashambulia.
31Inuka uende kulishambulia taifa linalostarehe,
taifa linaloishi kwa usalama.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Taifa hilo halina malango wala pao za chuma;
ni taifa ambalo liko peke yake.
32“Ngamia wao watatekwa
mifugo yao itachukuliwa mateka.
Nitawatawanya kila upande,
watu wale wanaonyoa denge.
Nitawaletea maafa kutoka kila upande.
Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
33Mji wa Hazori utakuwa makao ya mbweha,
utakuwa jangwa daima;
hakuna mtu atakayekaa humo,
wala atakayeishi humo.”
Elamu
34Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia nabii Yeremia kuhusu Elamu, mwanzoni mwa utawala wa Sedekia, mfalme wa Yuda. 35Mwenyezi-Mungu wa majeshi, asema hivi: “Nitavunja upinde wa watu wa Elamu ulio msingi wa nguvu zao. 36Nitaleta upepo kutoka pande zote za mbingu; nitawatawanya kila mahali, wala hapatakuwa na taifa lolote ambalo halitakuwa na wakimbizi wa Elamu. 37Nitawafadhaisha watu wa Elamu mbele ya maadui zao na mbele ya wale wanaotaka kuyaangamiza maisha yao. Nitawaletea maafa na hasira yangu kali. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema. Nitawaletea upanga kuwafuata mpaka niwaangamize kabisa. 38Nitaweka kiti changu cha enzi huko Elamu na kumwangamiza mfalme wao pamoja na wakuu wao. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema. 39Lakini katika siku za mwisho, nitaurudishia mji wa Elamu fanaka yake. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”


Yeremia49;1-39

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 48....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Kisha Yesu akasema kwa sauti kubwa, “Mtu anayeniamini, haniamini mimi tu, ila anamwamini pia yule aliyenituma. Anayeniona mimi anamwona pia yule aliyenituma.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Mimi ni mwanga, nami nimekuja ulimwenguni ili wote wanaoniamini wasibaki gizani. Anayeyasikia maneno yangu lakini hayashiki, mimi sitamhukumu; maana sikuja kuuhukumu ulimwengu bali kuuokoa. Asiyeyashika maneno yangu anaye wa kumhukumu: Neno lile nililosema ni hakimu wake siku ya mwisho.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....


Mimi sikunena kwa mamlaka yangu mwenyewe, ila Baba aliyenituma ndiye aliyeniamuru niseme nini na niongee nini. Nami najua kuwa amri yake huleta uhai wa milele. Basi, mimi nasema tu yale Baba aliyoniagiza niyaseme.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Moabu
1Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, asema hivi:
“Ole watu wa Nebo, maana mji wake umeharibiwa!
Kiriathaimu umeaibishwa, umetekwa,
ngome yake imebomolewa mbali;
2fahari ya Moabu imetoweka.
Mpango ulifanywa huko Heshboni dhidi yake:
‘Haya! Tuwaangamize wasiwe tena taifa!’
Nawe Madmeni utanyamazishwa,
upanga utakufuatia.
3Sikiliza! Kilio kutoka Horonaimu:
‘Maangamizi na uharibifu mkubwa!’
4Moabu tayari imeangamizwa
kilio chake chasikika mpaka Soari.
5Walionusurika wanapanda kwenda Luhithi
huku wanalia kwa sauti.
Wanapoteremka kwenda Horonaimu,
wanasikia kilio cha uharibifu.
6Kimbieni! Jiokoeni wenyewe!
Kimbieni kama pundamwitu jangwani!
7“Moabu, ulitumainia ngome na hazina zako,
lakini sasa wewe pia utatekwa;
mungu wako Kemoshi atapelekwa uhamishoni
pamoja na makuhani na watumishi wake.
8Mwangamizi atapita katika kila mji,
hakuna mji utakaomwepa;
kila kitu mabondeni kitaangamia
nyanda za juu zitaharibiwa,
kama alivyosema Mwenyezi-Mungu.
9Mchimbieni Moabu kaburi,
maana kuangamia kwake ni hakika;
miji yake itakuwa tupu,
bila mkazi hata mmoja.
10Na alaaniwe mtu afanyaye kazi ya Mwenyezi-Mungu kwa ulegevu; alaaniwe anayezuia upanga wake usimwage damu!
11Moabu amestarehe tangu ujana wake,
ametulia kama divai katika gudulia.
Hajamiminiwa toka chombo hata chombo,
hajapata kuchukuliwa uhamishoni.
Kwa hiyo yungali na ladha yake,
harufu yake nzuri haijabadilika kamwe.
12“Kwa hiyo, wakati waja, nasema mimi Mwenyezi-Mungu ambapo nitampelekea wamiminaji ambao wataimimina divai yake. Wataimwaga yote kutoka vyombo vyake na kuvivunja vipandevipande. 13Hapo Wamoabu watamwonea aibu mungu wao Kemoshi, kama vile watu wa Israeli walivyomwonea aibu Betheli, mungu waliyemtegemea.
14Mwawezaje kusema: ‘Sisi ni mashujaa,
na watu wenye nguvu nyingi za vita?’
15Mwangamizi wa Moabu na miji yake amewasili
vijana wake wazuri wamechinjwa.
Nimesema mimi mfalme
niitwaye Mwenyezi-Mungu wa Majeshi.
16Janga la Moabu limekaribia,
maangamizi yake yanawasili haraka.
17Mwomboleezeni Moabu, enyi jirani zake wote,
na nyote mnaomjua vizuri
semeni: ‘Jinsi gani fimbo ya nguvu ilivyovunjwa,
naam fimbo ile ya fahari!’
18Enyi wenyeji wa Diboni:
Shukeni kutoka mahali penu pa fahari,
mkaketi katika ardhi isiyo na maji.
Maana mwangamizi wa Moabu,
amefika kuwashambulia;
amekwisha haribu ngome zenu.
19Enyi wakazi wa Aroeri,
simameni kando ya njia mtazame!
Mwulizeni anayekimbia na anayetoroka:
‘Kumetokea nini?’
20Moabu imeaibishwa maana imevunjwa;
ombolezeni na kulia.
Tangazeni kando ya mto Arnoni,
kwamba Moabu imeharibiwa kabisa.
21“Hukumu imeifikia miji iliyo nyanda za juu: Holoni, Yasa, Mefaathi, 22Diboni, Nebo, Beth-diblathaimu, 23Kiriathaimu, Beth-gamuli, Beth-meoni, 24Keriothi na Bosra. Naam, hukumu imeifikia miji yote ya Moabu mbali na karibu. 25Nguvu za Moabu zimevunjiliwa mbali na uwezo wake umevunjwa. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
26“Mlewesheni Moabu kwa sababu alijikuza dhidi yangu mimi Mwenyezi-Mungu. Moabu atagaagaa katika matapishi yake na watu watamcheka. 27Kumbuka Moabu ulivyomcheka Israeli. Je, alikamatwa pamoja na wezi, hata ukawa unatikisa kichwa chako kila ulipoongea juu yake?
28“Enyi wenyeji wa Moabu,
tokeni mijini, mkakae mapangoni!
Mwigeni njiwa ajengaye kiota penye genge.
29Tumesikia juu ya kiburi cha Moabu;
Moabu ana majivuno sana.
Tumesikia juu ya kujiona, kiburi na majivuno yake;
tumesikia jinsi anavyojigamba moyoni.
30“Nami Mwenyezi-Mungu nasema:
Najua ufidhuli wake;
Majivuno yake ni ya bure,
na matendo yake si kitu.
31Kwa hiyo ninaomboleza juu ya Moabu,
ninalia kwa ajili ya Wamoabu wote,
naomboleza juu ya watu wa Kir-heresi.
32Nakulilia wewe bustani ya Sibma
kuliko hata watu wa Yazeri.
Matawi yako yametanda
mpaka ngambo ya bahari ya Chumvi
yakafika hata mpaka Yazeri.
Lakini mwangamizi ameyakumba
matunda yako ya kiangazi na zabibu zako.
33Furaha na shangwe zimeondolewa
kutoka nchi ya Moabu yenye rutuba.
Nimeikomesha divai kutoka mashinikizo
hakuna mtu anayekamua zabibu kwa shangwe;
kelele zinazosikika si za shangwe.
34“Kilio cha watu wa Heshboni chasikika huko Eleale mpaka Yahazi; kinaenea kutoka Soari mpaka Horonaimu na hata Eglath-shelishiya. Hata maji ya kijito Nimrimu yamekauka. 35Nami nitamfutilia mbali kila mtu katika Moabu ambaye anatambikia vilimani na kumfukizia ubani mungu wake.
36“Kwa hiyo, moyo wangu unaomboleza juu ya watu wa Moabu na watu wa Kir-heresi, kama mpiga zumari mazishini; maana hata mali yote waliyojipatia imeangamia. 37Kila mtu amenyoa upara na ndevu zake. Wote wamejikatakata mikononi na viunoni wamevaa mavazi ya gunia. 38Juu ya nyumba za Moabu na katika viwanja vyao hakuna kinachosikika ila tu maombolezo. Mimi nimemvunja Moabu kama chombo kisichotakiwa na mtu. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema. 39Tazama alivyovunjika! Tazama wanavyoomboleza! Ajabu jinsi Moabu alivyorudi nyuma kwa aibu! Moabu amekuwa kichekesho na kioja kwa jirani zake wote.”
40Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Tazama, taifa litaruka kasi kuivamia Moabu,
kama tai aliyekunjua mabawa yake.
41Miji yake itatekwa,
ngome zitachukuliwa.
Siku hiyo mioyo ya wanajeshi wa Moabu,
itaogopa kama mwanamke anayejifungua.
42Wamoabu wataangamizwa, wasiwe tena taifa,
kwa sababu walijikweza dhidi ya Mwenyezi-Mungu.
43Kitisho, mashimo na mtego,
vinawasubiri enyi watu wa Moabu.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
44Atakayetoroka kitisho
atatumbukia shimoni;
atakayetoka shimoni
atanaswa mtegoni.
Kwa maana nitaleta mambo hayo juu ya Moabu,
katika mwaka wao wa adhabu.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
45Wakimbizi wachovu wanatua Heshboni kutaka usalama,
maana moto umezuka huko mjini;
mwali wa moto toka ikulu ya mfalme Sihoni;
umeteketeza mipaka48:45 mipaka: Kiebrania: Uso. ya Moabu,
umeunguza milima48:45 milima: Kiebrania: Utosi. yao hao watukutu.
46Ole wenu watu wa Moabu!
Watu wa Kemoshi sasa mmeangamizwa,
wana wenu wamechukuliwa mateka,
binti zenu wamepelekwa uhamishoni.
47Lakini siku zijazo
nitamstawisha tena Moabu.
Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.
Hii ndiyo hukumu juu ya Moabu.”


Yeremia48;1-47

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 4 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 47....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu



Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!


Ingawa Yesu alifanya miujiza hii yote mbele yao, wao hawakumwamini. Hivyo maneno aliyosema nabii Isaya yakatimia: “Bwana, nani aliyeuamini ujumbe wetu? Na uwezo wa Bwana umedhihirishwa kwa nani?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Hivyo hawakuweza kuamini, kwani Isaya alisema tena: “Mungu ameyapofusha macho yao, amezipumbaza akili zao; wasione kwa macho yao, wasielewe kwa akili zao; wala wasinigeukie, asema Bwana, ili nipate kuwaponya.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliuona utukufu wa Yesu, akasema habari zake. Hata hivyo, wengi wa viongozi wa Wayahudi walimwamini Yesu. Lakini kwa sababu ya Mafarisayo, hawakumkiri hadharani kwa kuogopa kwamba watatengwa na sunagogi. Walipendelea kusifiwa na watu kuliko kusifiwa na Mungu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Tamko la Mwenyezi-Mungu juu ya Filistia
1Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia nabii Yeremia kuhusu Wafilisti, kabla Farao hajaushambulia mji wa Gaza:
2Mwenyezi-Mungu asema hivi:
“Tazama! Maji yanapanda kutoka kaskazini,
nayo yatakuwa mto uliofurika;
yataifunika nchi nzima na vyote vilivyomo,
mji na wakazi na wanaoishi humo.
Watu watalia,
wakazi wote wa nchi wataomboleza.
3Watasikia mshindo wa kwato za farasi,
kelele za magari ya vita,
na vishindo vya magurudumu yao.
Kina baba watawasahau watoto wao,
mikono yao itakuwa imelegea mno.
4Hiyo ni siku ya kuwaangamiza Wafilisti wote,
kukomesha msaada uliobakia kutoka Tiro na Sidoni.
Maana Mwenyezi-Mungu anawaangamiza Wafilisti,
watu waliosalia wa kisiwa cha Kaftori.
5Watu wa Gaza wamenyoa upara kuomboleza;
mji wa Ashkeloni umeangamia.
Enyi watu wa Anakimu mliobaki
mpaka lini mtajikatakata kwa huzuni?
6Ee upanga wa Mwenyezi-Mungu!
Utachukua muda gani ndipo utulie?
Ingia katika ala yako,
ukatulie na kunyamaa!
7Lakini utawezaje kutulia,
hali Mwenyezi-Mungu ameupa kazi?
Ameuamuru ushambulie mji wa Ashkeloni
na watu wanaoishi pwani.”


Yeremia47;1-7

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 3 February 2020

Kikombe Cha Asubuhi; Yeremia 46....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu

Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!


“Sasa roho yangu imefadhaika, na niseme nini? Je, niseme: ‘Baba, usiruhusu saa hii inifikie?’ Lakini ndiyo maana nimekuja – ili nipite katika saa hii. Baba, ulitukuze jina lako.” Hapo sauti ikasema kutoka mbinguni, “Nimelitukuza, na nitalitukuza tena.”
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Umati wa watu waliokuwa wamesimama hapo walisikia sauti hiyo, na baadhi yao walisema, “Ni ngurumo.” Lakini wengine wakasema, “Malaika ameongea naye!” Lakini Yesu akawaambia, “Sauti hiyo haikutokea kwa ajili yangu mimi, ila kwa ajili yenu. Sasa ndio wakati wa ulimwengu huu kuhukumiwa; sasa mtawala wa ulimwengu huu atapinduliwa. Nami nitakapoinuliwa juu ya nchi nitamvuta kila mmoja kwangu.” (Kwa kusema hivyo alionesha atakufa kifo gani).
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


Basi, umati huo ukamjibu, “Sisi tunaambiwa na sheria yetu kwamba Kristo atadumu milele. Wawezaje basi, kusema ati Mwana wa Mtu anapaswa kuinuliwa? Huyo Mwana wa Mtu ni nani?” Yesu akawaambia, “Mwanga bado uko nanyi kwa muda mfupi. Tembeeni mngali mnao huo mwanga ili giza lisiwapate; maana atembeaye gizani hajui aendako. Basi, wakati mnao huo mwanga uaminini ili mpate kuwa watu wa mwanga.” Baada ya kusema maneno hayo, Yesu alikwenda zake na kujificha mbali nao.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


1Neno la Mwenyezi-Mungu lililomjia Yeremia kuhusu watu wa mataifa.
Tamko la Mwenyezi-Mungu juu ya Misri
2Kuhusu Misri na jeshi la Farao Neko mfalme wa Misri, lililokuwa huko Karkemishi karibu na mto Eufrate ambalo Nebukadneza mfalme wa Babuloni alilishambulia mnamo mwaka wa nne wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia, mfalme wa Yuda:
3Tayarisheni ngao ndogo na kubwa
msonge mbele kupigana vita.
4Tandikeni farasi na kuwapanda,
Shikeni nafasi zenu na kofia za chuma mvae.
Noeni mikuki yenu,
vaeni mavazi yenu ya chuma!
5Lakini mbona nawaona wametishwa?
Wamerudi nyuma.
Mashujaa wao wamepigwa,
wamekimbia mbio,
bila hata kugeuka nyuma.
Kitisho kila upande.
Mwenyezi-Mungu amesema.
6Walio wepesi kutoroka hawawezi,
mashujaa hawawezi kukwepa;
huko kaskazini kwenye mto Eufrate
wamejikwaa na kuanguka.
7Nani huyo aliye kama mto Nili uliofurika
kama mito inayoumuka mawimbi?
8Misri ni kama mto Nili uliofurika
kama mito inayoumuka mawimbi
Ilisema: “Nitajaa, nitaifunika nchi,
nitaiharibu miji na wakazi wake.
9Songeni mbele, enyi farasi,
shambulieni enyi magari ya farasi.
Mashujaa wasonge mbele:
Watu wa Kushi na Puti washikao ngao,
watu wa Ludi, stadi wa kutumia pinde.”
10Siku hiyo ni siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
ni siku ya kulipiza kisasi;
naam, siku ya kuwaadhibu maadui zake.
Upanga utawamaliza hao na kutosheka,
utainywa damu yao na kushiba.
Maana Mwenyezi-Mungu wa majeshi anayo kafara
huko kaskazini karibu na mto Eufrate.
11Pandeni Gileadi, enyi watu wa Misri,
mkachukue dawa ya marhamu.
Mmetumia dawa nyingi bure;
hakuna kitakachowaponya nyinyi.
12Mataifa yamesikia aibu yenu,
kilio chenu kimeenea duniani kote;
mashujaa wamegongana wenyewe kwa wenyewe,
wote pamoja wameanguka.
Misri inavamiwa
13Neno ambalo Mwenyezi-Mungu alimwambia Yeremia wakati alipofika Nebukadneza mfalme wa Babuloni kuishambulia nchi ya Misri:
14“Tangaza nchini Misri,
piga mbiu huko Migdoli,
tangaza huko Memfisi na Tahpanesi.
Waambie: ‘Kaeni tayari kabisa
maana upanga utawaangamiza kila mahali.’
15Kwa nini shujaa wako amekimbia?
Mbona fahali wako hakuweza kustahimili?
Kwa sababu mimi Mwenyezi-Mungu nilimwangusha chini!
16Wengi walijikwaa, wakaanguka,
kisha wakaambiana wao kwa wao:
‘Simameni, tuwaendee watu wetu,
turudi katika nchi yetu,
tuukimbie upanga wa adui.’
17“Naye Farao, mfalme wa Misri, mpangeni jina hili:
‘Kishindo kitupu!’
18Mimi naapa kwa uhai wangu
nasema mimi mfalme niitwaye Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
kweli adui anakuja kuwashambulieni:
Ni hakika kama Tabori ulivyo mlima
kama mlima Karmeli uonekanavyo kutoka baharini.
19Enyi wakazi wa Misri
jitayarisheni na mizigo kwenda uhamishoni!
Maana mji wa Memfisi utaharibiwa kabisa,
utakuwa magofu yasiyokaliwa na watu.
20Misri ni kama mtamba mzuri wa ng'ombe,
lakini kipanga kutoka kaskazini amemvamia.
21Hata askari wake wa kukodiwa ni kama ndama wanono;
nao pia wamegeuka, wakakimbia pamoja,
wala hawakuweza kustahimili,
kwa maana siku yao ya kuangamizwa imefika,
wakati wao wa kuadhibiwa umewadia.
22Misri anatoa sauti kama nyoka anayekimbia;
maana maadui zake wanamjia kwa nguvu,
wanamjia kwa mashoka kama wakata-miti.
23Wataukata kabisa msitu wake, ingawa haupenyeki,
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
maana wao ni wengi kuliko nzige wasiohesabika.
24Watu wa Misri wataaibishwa,
watatiwa mikononi mwa watu kutoka kaskazini.”
25Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, alisema: “Tazama, mimi nitamwadhibu Amoni mungu wa Thebesi, nitaiadhibu Misri na miungu yake na wafalme wake, nitamwadhibu Farao na wote wanaomtegemea. 26Nitawatia mikononi mwa wale wanaotaka kuyaangamiza maisha yao, yaani Nebukadneza mfalme wa Babuloni na maofisa wake. Baadaye, nchi ya Misri itakaliwa na watu kama ilivyokuwa hapo zamani. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.
Mwenyezi-Mungu atawaokoa watu wake
27“Lakini wewe usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,
usifadhaike, ee Israeli;
maana, kutoka mbali nitakuokoa,
nitakuja kuwaokoa wazawa wako
kutoka nchi walimohamishwa.
Yakobo utarudi na kutulia na kustarehe,
wala hakuna yeyote atakayekutia hofu.
28Usiogope, ee Yakobo mtumishi wangu,
kwa maana mimi niko pamoja nawe.
Nitayaangamiza kabisa mataifa yote
ambayo nimekutawanya kati yao,
lakini wewe sitakuangamiza.
Nitakuchapa kadiri unavyostahili,
sitakuacha bila kukuadhibu.”

Yeremia46;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.