Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 5 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 5....


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Alfajiri na mapema, mfalme Dario aliamka, akaenda kwa haraka kwenye pango la simba. Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni, “Danieli, mtumishi wa Mungu aliye hai! Je, Mungu wako unayemtumikia daima ameweza kukuokoa na simba hawa?”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Danieli akamjibu mfalme, “Uishi, ee mfalme! Mungu wangu alileta malaika wake kuvifumba vinywa vya simba hawa, nao hawakunidhuru. Alifanya hivyo kwa sababu alijua mimi sina lawama yoyote kwake na wala sijafanya lolote baya mbele yako.”
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...


Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Hapo mfalme akafurahi sana; akaamuru Danieli atolewe pangoni. Basi wakamtoa, naye alikuwa hajadhurika hata kidogo, kwa sababu alimtegemea Mungu wake.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.


Wimbo wa shamba la mizabibu
1 5:1-2 Taz Mat 21:33; Marko 12:1; Luka 20:9
 Nitaimba juu ya rafiki yangu,
wimbo wa rafiki yangu na shamba lake la mizabibu:
Rafiki yangu alikuwa na shamba la mizabibu
juu ya kilima chenye rutuba nyingi.
2Alililima vizuri na kuondoa mawe yote,
akaotesha humo mizabibu iliyochaguliwa;
alijenga mnara wa ulinzi katikati yake,
akachimba kisima cha kusindikia divai.
Kisha akangojea lizae zabibu,
lakini likazaa zabibu chungu.
3Kwa hiyo rafiki yangu anasema hivi:
“Enyi wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda,
amueni tafadhali kati yangu na shamba langu.
4Ni kitu gani nilichokosa kulifanyia shamba langu?
Na nilipotazamia lizae zabibu nzuri,
mbona basi, likazaa zabibu chungu?
5“Na sasa nitawaambieni
nitakavyolifanya hilo shamba langu.
Nitauondoa ua wake,
nalo litaharibiwa.
Nitaubomoa ukuta wake,
nalo litakanyagwakanyagwa.
6Nitaliacha liharibiwe kabisa,
mizabibu yake haitapogolewa wala kupaliliwa.
Litaota mbigili na miiba.
Tena nitayaamuru mawingu
yasinyeshe mvua juu yake.”
7Naam! Shamba la mizabibu la Mwenyezi-Mungu wa majeshi
ni jumuiya ya Waisraeli,
na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda.
Yeye alitazamia watende haki,
badala yake wakafanya mauaji;
alitazamia uadilifu,
badala yake wakasababisha kilio!

Maovu wanayotenda watu
8Ole wao wanaonunua nyumba baada ya nyumba,
wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao,
mpaka kila sehemu inakuwa mali yao,
na hamna nafasi kwa wengine nchini.
9Nimemsikia Mwenyezi-Mungu wa majeshi akitamka hivi:
“Hakika nyumba nyingi zitabaki tupu,
majumba makubwa mazuri bila wakazi.
10Shamba la mizabibu la eka kumi
litatoa lita5:10 lita: Ni kipimo cha vitu majimaji na sio vitu kama mbegu. nane tu za divai;
anayepanda kilo 100 za mbegu
atavuna kilo 10 tu za nafaka.”
11Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema
wapate kukimbilia kunywa kileo;
wanaokesha hata usiku,
mpaka divai iwaleweshe!
12Katika karamu zao, hapakosekani vinubi,
zeze, matari, filimbi na divai.
Lakini hawajali matendo ya Mwenyezi-Mungu,
wala kuzitambua kazi za mikono yake.
13Kwa hiyo, watu wangu watapelekwa uhamishoni
kwa sababu ya utovu wao wa akili.
Watu wenu mashuhuri watakufa njaa,
watu wengi watakufa kwa kiu.
14Kuzimu inawangoja kwa hamu kubwa,
imepanua kinywa chake mpaka mwisho.
Waheshimiwa pamoja na raia wa Yerusalemu
wanaingia humo makundi kwa makundi,
kadhalika na wote wanaousherehekea.
15Kila mtu atafedheheshwa,
na wenye kiburi wote wataaibishwa.
16Lakini Mwenyezi-Mungu wa majeshi atatukuzwa.
Yeye huonesha ukuu wake
kwa matendo yake ya haki,
kwa kuwahukumu watu wake.
17Wanakondoo, wanambuzi na ndama,
watapata malisho yao kwenye magofu ya miji yao,
kana kwamba hizo ni sehemu za malisho yao.
18Ole wao wanaoburuta uovu kama kwa kamba;
wanaokokota dhambi kama kwa kamba za mkokoteni.
19Wanasema:
“Mwache Mwenyezi-Mungu afanye haraka,
tunataka kuyaona aliyosema atayafanya!
Mtakatifu wa Israeli na atimize kusudi lake.
Hebu na tuone ana mipango gani!”
20Ole wao wanaosema uovu ni wema
na wema ni uovu.
Giza wanasema ni mwanga
na mwanga wanasema ni giza.
Kichungu wanasema ni kitamu
na kitamu wanakiona kuwa kichungu.
21Ole wao wanaojiona kuwa wenye hekima
ambao wanajiona kuwa wenye akili.
22Ole wao mabingwa wa kunywa divai,
hodari sana wa kuchanganya vileo.
23Kwa hongo kidogo wanawaachilia wenye hatia
na kuwanyima wasio na hatia haki yao.
24Kwa hiyo, kama moto uteketezavyo nyasi,
kama majani yateketeavyo katika mwali wa moto
ndivyo na mizizi yao itakavyooza,
na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama vumbi.
Maana wameiacha sheria ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi,
wamedharau neno la yule Mtakatifu wa Israeli.
25Kwa hiyo hasira ya Mwenyezi-Mungu iliwawakia watu wake,
akaunyosha mkono wake dhidi yao, akawachapa,
hata milima ikatetemeka,
maiti zao zikawa kama takataka
katika barabara za mji.
Hata hivyo, hasira yake haikutulia,
mkono wake bado ameunyosha kuwaadhibu.
26Mwenyezi-Mungu analiashiria taifa la mbali;
anawapigia mruzi watu kutoka miisho ya dunia;
nao waja mbio na kuwasili haraka!
27Hawachoki wala hawajikwai;
hawasinzii wala hawalali;
hakuna mshipi wao uliolegea
wala kamba ya kiatu iliyokatika.
28Mishale yao ni mikali sana,
pinde zao zimevutwa tayari.
Kwato za farasi wao ni ngumu kama mawe;
mwendo wa magurudumu ya magari ni kimbunga.
29Askari wao wananguruma kama simba;
wananguruma kama wanasimba
ambao wamekamata mawindo yao
na kuwapeleka mahali mbali
ambapo hakuna awezaye kuwanyanganya.
30Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli
kama mvumo wa bahari iliyochafuka.
Atakayeiangalia nchi kavu
ataona giza tupu na dhiki,
mwanga utafunikwa na mawingu.

Isaya5;1-30

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 4 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 4....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Ndipo mfalme Dario akatoa amri, naye Danieli akaletwa na kutupwa katika pango la simba. Mfalme akamwambia Danieli, “Mungu wako ambaye unamtumikia daima, na akuokoe.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Jiwe likaletwa na kuwekwa mlangoni mwa lile pango. Mfalme akalipiga mhuri wake binafsi na ule wa wakuu wake, ili uamuzi kuhusu Danieli usibatilishwe.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kisha mfalme akarudi katika ikuluni yake ambamo alikesha akifunga; hakufanya tafrija ya aina yoyote, na usingizi ukampaa.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Wakati huo wanawake saba watamvamia mwanamume mmoja na kumwambia, “Chakula na mavazi tutajitafutia wenyewe, lakini wewe utuondolee aibu yetu, uturuhusu tuitwe kwa jina lako.”

Mji wa Yerusalemu utarekebishwa
2Siku ile, tawi atakalochipusha Mwenyezi-Mungu litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya nchi yatakuwa ya fahari na utukufu kwa wale Waisraeli watakaosalia. Waisraeli watakaobaki watayaonea fahari na kujivunia mazao ya nchi yao. 3Wale watakaosalia hai mjini Yerusalemu, naam, wale watakaobaki huko Siyoni, wataitwa “Wateule wa Mungu;” hao ndio wale wote watakaokuwa wameandikwa kitabuni mwake waishi huko Yerusalemu. 4Kwa roho yake, Bwana atawaweka sawa na kuwatakasa. Na atakapokwisha kuwatakasa wanawake wa Siyoni uchafu wao na kufuta madoa ya damu yaliyomo humo Yerusalemu, 54:5 Taz Kut 13:21; 24:16 hapo atafanya kila mahali juu ya mlima Siyoni na juu ya mikutano ya watu kuwe na wingu wakati wa mchana, na moshi na moto uwakao vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda mji wote. 6Utukufu wake utakuwa kwao kivuli kuwakinga na joto la mchana; na kimbilio na kinga yao wakati wa dhoruba na mvua.

Isaya4;1-6

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 3 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 3....

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Basi, walikwenda kwa mfalme na kumshtaki Danieli kwa kutumia ile sheria, wakisema, “Mfalme Dario, je, hukutia sahihi hati ya sheria kuwa kwa muda wa siku thelathini hakuna mtu yeyote atakayeruhusiwa kuomba kitu chochote, kwa mungu yeyote, au kwa mtu yeyote isipokuwa kutoka kwako wewe, ee mfalme, na kwamba yeyote atakayevunja sheria hii atatumbukizwa katika pango la simba?” Mfalme akaitikia, “Hivyo ndivyo ilivyo, kulingana na sheria ya Wamedi na Wapersi ambayo haiwezi kubatilishwa.”
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Wakamwambia mfalme, “Yule Danieli aliye mmoja wa mateka kutoka nchi ya Yuda hakuheshimu wewe mfalme wala haitii amri uliyotia sahihi. Yeye anasali mara tatu kila siku.” Mfalme aliposikia maneno hayo, alisikitika sana. Akajitahidi sana kupata njia ya kumwokoa Danieli. Aliendelea kujaribu mpaka jua likatua.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Wale watu wakamwendea mfalme Dario kwa pamoja na kumwambia, “Ee mfalme, ujue kuwa hakuna sheria wala amri yoyote ya Wamedi na Wapersi inayoweza kubatilishwa baada ya kuwekwa na mfalme.”
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Msukosuko Yerusalemu
1Sasa, Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi
ataondoa kutoka Yerusalemu na Yuda kila tegemeo:
Tegemeo lote la chakula,
na tegemeo lote la kinywaji.
2Ataondoa mashujaa na askari,
waamuzi na manabii,
waaguzi na wazee,
3majemadari wa vikosi vya watu hamsini,
na watu wenye vyeo,
washauri, wachawi stadi na walozi hodari.
4Mungu ataweka watoto wawatawale;
naam, watoto wachanga watawatawala.
5Watu watadhulumiana,
kila mtu na jirani yake;
vijana watawadharau wazee wao,
na watu duni watapuuza wakuu wao.
6Wakati huo ndugu atamwambia ndugu yake
wakiwa bado nyumbani kwa baba yao:
“Wewe unalo koti;
utakuwa kiongozi wetu.
Chukua hatamu juu ya uharibifu huu!”
7Lakini siku hiyo atasema,
“Mimi siwezi kuwa mwuguzi,
nyumbani mwangu hamna chakula wala mavazi.
Msinifanye mimi kuwa kiongozi wenu.”
8Watu wa Yerusalemu wamejikwaa,
watu wa Yuda wameanguka,
kwa kuwa wanampinga Mwenyezi-Mungu
kwa maneno na matendo,
wakipuuza utukufu wake miongoni mwao.
9Ubaguzi wao unashuhudia dhidi yao;
wanatangaza dhambi yao kama ya Sodoma,
wala hawaifichi.
Ole wao watu hao,
kwani wamejiletea maangamizi wenyewe.
10Waambieni waadilifu jinsi walivyo na bahati:
Kwani watakula matunda ya matendo yao.
11Lakini ole wao watu waovu!
Mambo yatawaendea vibaya,
kwani waliyotenda yatawapata wao wenyewe.
12Watu wangu watadhulumiwa na watoto;
wanawake ndio watakaowatawala.
Enyi watu wangu, viongozi wenu wanawapotosha,
wanavuruga njia mnayopaswa kufuata.

Mwenyezi-Mungu awahukumu watu wake
13Mwenyezi-Mungu yu tayari kuanza mashtaka,
anasimama kuwahukumu watu wake.
14Mwenyezi-Mungu anawashtaki
wazee na wakuu wa watu wake:
“Nyinyi ndio mlioliharibu shamba la mizabibu;
mali walizowanyanganywa maskini zimo nyumbani kwenu.
15Mnamaanisha nini kuwakandamiza watu wangu,
kuwatendea ukatili watu maskini?
Nauliza mimi Bwana, Mwenyezi-Mungu wa majeshi.”

Onyo kwa wanawake wa Yerusalemu
16Mwenyezi-Mungu asema:
“Wanawake wa Siyoni wana kiburi;
wanatembea wameinua shingo juu,
wakipepesa macho yao kwa tamaa.
Hatua zao ni za maringo,
na miguuni njuga zinalia.
17Basi, mimi Mwenyezi-Mungu nitawaadhibu;
nitawanyoa nywele hao wanawake wa Siyoni,
na kuwavua nguo za kufunika uchi wao.”
18Siku yaja ambapo Mwenyezi-Mungu atawanyanganya wanawake wa Yerusalemu vitu vyote wanavyoringia: Njuga, kaya, mikufu, 19vipuli, vikuku, shungi, 20vitambaa vya kichwani, bangili, vibwebwe, vibweta vya marashi, hirizi, 21pete, hazama, 22mavazi ya sikukuu, mitandio, majoho, mikoba, 23mavazi yaoneshayo, mavazi ya kitani, vilemba na shela.
24Badala ya kunukia marashi watatoa uvundo;
badala ya mishipi mizuri watatumia kamba;
badala ya nywele nzuri watakuwa na upara;
badala ya mavazi mazuri watavaa matambara;
uzuri wao wote utageuka kuwa aibu.
25Wanaume wenu wataangamia kwa upanga,
watu wenu wenye nguvu watakufa vitani.
26Malango ya mji yatalia na kuomboleza;
nao mji utakuwa kama mwanamke aliyepokonywa kila kitu, ameketi mavumbini.

Isaya3;1-26

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 2 September 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Isaya 2....



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah ni siku/wiki/mwezi mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Hivyo, ee mfalme Dario, utoe amri hiyo na kuitia hati sahihi yako ili isibadilishwe. Nayo itakuwa sheria ya Wamedi na Wapersi, sheria ambayo haibatilishwi.” Hivyo, mfalme Dario akaitia sahihi hati ya sheria hiyo.
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona....

Danieli alipojua kuwa ile hati imetiwa sahihi, alirudi nyumbani kwake ghorofani katika chumba chake kilichokuwa na madirisha yaliyofunguka kuelekea Yerusalemu. Humo, Danieli, kama ilivyokuwa kawaida yake, alipiga magoti mara tatu kila siku akamwomba na kumshukuru Mungu wake.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Watu wale waliofanya mpango dhidi ya Danieli waliingia ndani, wakamkuta Danieli akiomba dua na kumsihi Mungu wake.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimamie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.


Amani ya kudumu
(Mika 4:1-3)
1Neno alilopewa Isaya, mwana wa Amozi, kuhusu Yuda na Yerusalemu.
2Siku zijazo mlima wa nyumba ya Mwenyezi-Mungu
utaimarishwa kupita milima yote,
utainuliwa juu ya vilima vyote.
Mataifa yote yatamiminika huko,
3watu wengi wataujia na kusema,
“Njoni tupande mlima wa Mwenyezi-Mungu,
twende nyumbani kwa Mungu wa Yakobo,
apate kutufundisha njia zake,
nasi tuishi kadiri ya mwongozo wake.
Maana sheria itakuja kutoka Siyoni;
neno la Mwenyezi-Mungu kutoka Yerusalemu.”
4 2:4 Taz Yoe 3:10 Mungu atasuluhisha mizozo ya mataifa
atakata mashauri ya watu wengi.
Watu watafua panga za vita kuwa majembe
na mikuki yao kuwa miundu ya kupogolea.
Taifa halitapigana na taifa lingine
wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.
5Sasa, enyi wazawa wa Yakobo, njoni,
tutembee katika mwanga wa Mwenyezi-Mungu.

Kiburi kitaondolewa
6Sasa, ee Mungu, umewatupa watu wako, wazawa wa Yakobo.
Maana kweli wachawi wa mashariki wamejaa kati yao,
wapo na wapiga ramli kama kwa Wafilisti.
Wanashirikiana na watu wageni.
7Nchi yao imejaa fedha na dhahabu,
hazina yao ni kubwa kupindukia.
Nchi yao imejaa farasi,
magari yao ya kukokotwa hayana idadi.
8Nchi yao imejaa vinyago vya miungu,
huabudu kazi ya mikono yao,
vitu walivyotengeneza wao wenyewe.
9Kwa hiyo, kila mtu ataaibishwa na kufedheheshwa.
Usiwasamehe hata kidogo, ee Mungu!
10 2:10 Taz Ufu 6:15; 2Thes 1:9 Ingieni katika mwamba,
mkajifiche mavumbini,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake.
11Siku yaja ambapo kiburi cha watu kitashushwa,
majivuno ya kila mtu yatavunjwa;
na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
12Naam, yaja siku ya Mwenyezi-Mungu wa majeshi
dhidi ya wenye kiburi na majivuno,
dhidi ya wote wanaojikweza;
13dhidi ya mierezi yote ya Lebanoni,
ambayo ni mirefu na mizuri,
dhidi ya mialoni yote nchini Bashani;
14dhidi ya milima yote mirefu,
dhidi ya vilima vyote vya juu;
15dhidi ya minara yote mirefu,
dhidi ya kuta zote za ngome;
16dhidi ya meli zote za Tarshishi,
na dhidi ya meli zote nzuri.
17Kiburi chote cha watu kitakomeshwa,
majivuno ya kila mtu yatavunjwa.
Na Mwenyezi-Mungu peke yake atatukuzwa siku hiyo.
18Vinyago vyote vya miungu vitatoweka kabisa.
19Ingieni katika mapango miambani,
katika mashimo ardhini,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake,
atakapokuja kuitia hofu dunia.
20Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo
vinyago vyao vya fedha na dhahabu
walivyojitengenezea ili kuviabudu.
21Nao wataingia katika mapango miambani
na kwenye nyufa za miamba,
kuiepa hasira ya Mwenyezi-Mungu,
mbali na utukufu wa enzi yake,
atakapokuja kuitia hofu dunia.
22Usimwamini binadamu,
uhai wake haudumu kama pumzi.
Yeye anafaa kitu gani?

Isaya2;1-22

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.