Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 23 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora4...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Mungu mwenyewe ndiye mwenye kutuimarisha sisi na nyinyi pia katika Kristo, na ndiye anayetuweka wakfu;
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

ndiye aliyetutia mhuri wa kuwa mali yake yeye na kutujalia Roho mioyoni mwetu kama dhamana ya mambo yote ambayo ametuwekea.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Mungu ndiye shahidi wangu; yeye anajua moyo wangu! Mimi sikuja tena Korintho kwa sababu tu ya kuwahurumieni. Hatutaki kutumia mabavu juu ya imani yenu; nyinyi mko imara katika imani yenu. Wajibu wetu ni kufanya kazi pamoja kwa ajili ya furaha yenu.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

Bwana arusi
1Hakika u mzuri ewe mpenzi wangu,
hakika u mzuri!
Macho yako ni kama ya hua
nyuma ya shela lako,
nywele zako ni kama kundi la mbuzi
washukao katika milima ya Gileadi.
2Meno yako ni kama kondoo majike waliokatwa manyoya
wanaoteremka baada ya kuogeshwa.
Kila mmoja amezaa mapacha,
na hakuna yeyote aliyefiwa.
3Midomo yako ni kama utepe mwekundu,
kinywa chako chavutia kweli.
Nyuma ya shela lako,
mashavu yako ni kama nusu mbili za komamanga.
4Shingo yako ni kama mnara wa Daudi,
uliojengwa ili kuhifadhia silaha,4:4 uliojengwa … silaha: Makala katika Kiebrania si dhahiri.
ambako zimetundikwa ngao elfu moja
zote zikiwa za mashujaa.
5Matiti yako ni kama paa mapacha,
ambao huchungwa penye yungiyungi.
6Nitakaa kwenye mlima wa manemane,
na kwenye kilima cha ubani,
hadi hapo kutakapopambazuka,
na giza kutoweka.
7Tazama ulivyo mzuri ee mpenzi wangu,
wewe huna kasoro yoyote.
8Njoo, bibiarusi wangu tuondoke Lebanoni;
na tuiachilie mbali Lebanoni.
Shuka toka kilele cha mlima Amana,
toka kilele cha Seniri na Hermoni,
toka mapango ya simba,
toka milima ya chui.
9Umefurahisha moyo wangu, dada yangu, bi arusi,
umefurahisha moyo wangu,
kwa kunitupia jicho mara moja tu,
na kwa huo mkufu wako shingoni.
10Dada yangu, bi arusi;
pendo lako ni tamu ajabu.
Ni bora kuliko divai,
marashi yako yanukia kuliko viungo vyote.
11Midomo yako yadondosha asali, ee bibiarusi wangu;
ulimi wako una asali na maziwa.
Harufu nzuri ya mavazi yako ni kama ya Lebanoni.
12Dada yangu, naam, bi arusi,
ni bustani iliyofichika,
bustani iliyosetiriwa;
chemchemi iliyotiwa mhuri.
13Machipukizi yako ni bustani ya mikomamanga
pamoja na matunda bora kuliko yote,
hina na nardo.
14Nardo na zafarani, mchai na mdalasini
manemane na udi,
na mimea mingineyo yenye harufu nzuri.
15U chemchemi ya bustani,
kisima cha maji yaliyo hai,
vijito vitiririkavyo kutoka Lebanoni.
Bibi arusi
16Vuma, ewe upepo wa kaskazi,
njoo, ewe upepo wa kusi;
vumeni juu ya bustani yangu,
mlijaze anga kwa manukato yake.
Mpenzi wangu na aje bustanini mwake,
ale matunda yake bora kuliko yote.

Wimbo Ulio Bora4;1-16

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 22 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora3...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Nikiwa na matumaini hayo, nilikusudia kuja kwenu hapo awali ili mpate baraka maradufu. Nilikusudia kupita kwenu nikiwa safarini kwenda Makedonia na wakati wa kurudi pia, ili nipate msaada wenu kwa safari yangu kwenda Yudea.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Je, mnadhani nilipopanga hivyo nimekuwa kama mtu asiye na msimamo? Je, mnadhani kwamba ninafanya uamuzi wangu kwa fikira za kibinadamu na kwamba nasema “Ndiyo” na “Siyo” papo hapo?
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Mungu ni ukweli tupu; basi, kile tulichowaambia nyinyi si jambo la “Ndiyo” na “Siyo”. Maana Kristo Yesu, Mwana wa Mungu, ambaye mimi, Silwano na Timotheo, tulimhubiri kwenu, hakuwa mtu wa “Ndiyo” na “Siyo;” bali yeye daima ni “Ndiyo” ya Mungu. Maana ndani yake ahadi zote za Mungu zimekuwa “Ndiyo”. Kwa sababu hiyo, “Amina” yetu husemwa kwa njia ya Kristo kwa ajili ya kumtukuza Mungu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

1Usiku nikiwa kitandani mwangu,
niliota namtafuta nimpendaye moyoni mwangu;
nilimtafuta, lakini sikumpata.
2Niliamka nikazunguka mjini,
barabarani na hata vichochoroni,
nikimtafuta yule wangu wa moyo.
Nilimtafuta, lakini sikumpata.
3Walinzi wa mji waliniona
walipokuwa wanazunguka mjini.
Basi nikawauliza,
“Je, mmemwona mpenzi wangu wa moyo?”
4Mara tu nilipoachana nao,
nilimwona mpenzi wangu wa moyo;
nikamshika wala sikumwachia aondoke,
hadi nilipompeleka nyumbani kwa mama yangu,
hadi chumbani kwake yule aliyenizaa.
5Nawasihini, enyi wanawake wa Yerusalemu,
kama walivyo paa au swala,
msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,
hadi hapo wakati wake utakapofika.
Shairi la tatu
Bibi arusi
6Ni kitu gani kile kitokacho jangwani
kama mnara wa moshi,
kinukiacho manemane na ubani,
manukato yauzwayo na wafanyabiashara?
7Tazama! Ni machela ya Solomoni;
amebebwa juu ya kiti chake cha enzi;
amezungukwa na walinzi sitini,
mashujaa bora wa Israeli.
8Kila mmoja wao ameshika upanga,
kila mmoja wao ni hodari wa vita.
Kila mmoja ana upanga wake mkononi,
tayari kumkabili adui usiku.
9Mfalme Solomoni alijitengenezea machela,
kwa mbao nzuri kutoka Lebanoni.
10Nguzo zake zilitengenezwa kwa fedha;
mgongo wake kwa dhahabu;
mahali pa kukalia pamefunikwa vitambaa vya zambarau,
walichoshona kwa upendo wanawake wa Yerusalemu,
waliokishonea alama za upendo.
11Njoni basi enyi wanawake wa Siyoni,
mkamwone mfalme Solomoni.
Amevalia taji aliyovikwa na mama yake,
siku alipofanya harusi yake,
naam, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.

Wimbo Ulio Bora3;1-11

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 21 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi; Wimbo Ulio Bora2...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Sisi tunajivunia kitu kimoja: Dhamiri yetu inatuhakikishia kwamba tumeishi ulimwenguni hapa, na hasa kati yenu, kwa unyenyekevu na unyofu tuliojaliwa na Mungu; hatukuongozwa na hekima ya kibinadamu bali na neema ya Mungu.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Tunawaandikia nyinyi mambo mnayoweza kuyasoma na kuyaelewa. Ninatumaini kwamba mtaelewa vizuri kabisa,
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

maana mpaka sasa mmenielewa kiasi fulani tu. Tunajua kwamba katika ile siku ya Bwana Yesu mtaweza kutuonea sisi fahari kama nasi tunavyowaonea nyinyi fahari.
Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Mimi ni ua la Sharoni,
ni yungiyungi ya bondeni.
Bwana arusi
2Kama yungiyungi kati ya michongoma,
ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya wasichana.
Bibi arusi
3Kama mtofaa kati ya miti ya msituni,
ndivyo alivyo mpenzi wangu kati ya wavulana.
Nafurahia kuketi chini ya kivuli chake,
na tunda lake tamu sana kwangu.
4Alinichukua hadi ukumbi wa karamu,
akatweka bendera ya mapenzi juu yangu.
5Nishibishe na zabibu kavu,
niburudishe kwa matofaa,
maana naugua kwa mapenzi!
6Mkono wake wa kushoto chini ya kichwa changu,
mkono wake wa kulia wanikumbatia.
7Nawasihi enyi wanawake wa Yerusalemu,
kama walivyo paa au swala wa porini,
msiyachochee wala kuyaamsha mapenzi,
hadi hapo wakati wake utakapofika.
Shairi la pili
Bibi arusi
8Hiyo ni sauti ya mpenzi wangu,
yuaja mbio,
anaruka milima,
vilima anavipita kasi!
9Mpenzi wangu ni kama paa,
ni kama swala mchanga.
Amesimama karibu na ukuta wetu,
achungulia dirishani,
atazama kimiani.
10Mpenzi wangu aniambia:
Bwana arusi
“Inuka basi, ewe mpenzi wangu, unipendezaye,
njoo twende zetu.
11Tazama, majira ya baridi yamepita,
nazo mvua zimekwisha koma;
12maua yamechanua kila mahali.
Wakati wa kuimba umefika;
sauti ya hua yasikika mashambani mwetu.
13Mitini imeanza kuzaa;
na mizabibu imechanua;
inatoa harufu nzuri.
Njoo, basi, ewe mpenzi wangu unipendezaye,
njoo twende.
14Ee hua wangu, uliyejificha miambani.
Hebu niuone uso wako,
hebu niisikie sauti yako,
maana sauti yako yapendeza na uso wako wavutia.
15“Tukamatieni mbweha,
wale mbweha wadogowadogo,
wanaoiharibu mizabibu yetu inayochanua.”
Bibi arusi
16Mpenzi wangu ni wangu, nami ni wake.
Yeye hulisha kondoo wake penye yungiyungi,
17hadi hapo jua linapochomoza
na vivuli kutoweka.
Rudi kama paa mpenzi wangu,
kama swala mdogo juu ya milima ya Betheri.

Wimbo Ulio Bora2;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 20 August 2019

Kikombe Cha Asubuhi;Tunamshukuru Mungu tumemaliza Kitabu cha Mhubiri,Leo tunaanza Kitabu Cha Wimbo Ulio Bora1...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana..
Tunamshukuru Mungu kwa kutupa kibali cha

 kupitia kitabu cha "MUHUBIRI
"
Ni matumaini yangu kuna mengi tumejifunza/kufaidika
na kutupa mwanga/kuelewa kwenye kitabu hiki...


Leo tunapokwenda anza kupitia Kitabu cha"Wimbo Ulio Bora"
tunamuomba Mungu wetu akatupe kibali,macho ya rohoni
 na akili ya kuelewa katika kujifunza NENO lake...
Ee Mungu  tunaomba ukatuongoze...!!

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni
Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!


Ndugu, tunataka kuwajulisheni taabu zilizotupata kule Asia; taabu hizo zilitulemea kupita kiasi, hata tukakata matumaini yote ya kuendelea kuishi.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....


Naam, tulikuwa kama watu waliohukumiwa kuuawa, ili tufundishwe kumtegemea Mungu mwenye kuwafufua wafu, badala ya kutegemea nguvu zetu sisi wenyewe. Yeye alituokoa katika hatari kubwa ya kifo, na anaendelea kutuokoa; sisi tumemwekea tumaini letu kwamba atatuokoa tena,
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...


nyinyi mkiwa mnatuunga mkono kwa kutuombea. Hivyo neema tutakazokuwa tumepata kutokana na maombi ya watu wengi hivyo, ziwe sababu ya watu wengi zaidi kumshukuru Mungu kwa ajili yetu.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

1 Taz 1Fal 4:32 Wimbo wa Solomoni1:1 wa Solomoni: Au Kwa heshima ya Solomoni, au juu ya Solomoni. ulio bora kuliko nyimbo zote.
Shairi la kwanza
Bibi arusi
2Heri midomo yako inibusu,
maana pendo lako ni bora kuliko divai.
3Manukato yako yanukia vizuri,
na jina lako ni kama marashi yaliyomiminwa.
Kwa hiyo wanawake hukupenda!
4Nichukue, twende zetu haraka,
mfalme amenileta katika chumba chake.
Tutafurahi na kushangilia kwa sababu yako,
tutasifu mapenzi yako kuliko divai.
Wanawake wana haki kukupenda!
5Enyi wanawake wa Yerusalemu,
mimi ni mweusi na ninapendeza,
kama mahema ya Kedari,
kama mapazia ya Solomoni.
6Msinishangae kwa sababu ni mweusi,
maana jua limenichoma.
Ndugu zangu walinikasirikia,
wakanifanya mlinzi wa mashamba ya mizabibu.
Lakini sikutunza shamba langu la mizabibu.
7Hebu niambie ee wangu wa moyo,
utawalisha wapi kondoo wako?
Ni wapi watakapopumzikia adhuhuri?
Kwa nini mimi nikutafute
kati ya makundi ya wenzako?1:7 Kwa nini … wenzako: Kiebrania si dhahiri.
Bwana arusi
8Ewe upendezaye kuliko wanawake wote;
kama hujui, fanya hivi:
Zifuate nyayo za kondoo;
basi, walishe mbuzi wako karibu na hema za wachungaji.
9Wewe ee mpenzi wangu,
nakulinganisha na farasi dume wa magari ya Farao.
10Mashavu yako yavutia kwa vipuli,
na shingo yako kwa mikufu ya johari.
11Lakini tutakufanyizia mikufu ya dhahabu,
iliyopambwa barabara kwa fedha.
Bibi arusi
12Mfalme alipokuwa kwenye kochi lake,
marashi yangu ya nardo yalisambaa kila mahali.
13Mpenzi wangu ni kama mfuko wa manemane kwangu,
kati ya matiti yangu.
14Mpenzi wangu ni kama maua ya hina yachanuayo,
kwenye mashamba ya mizabibu huko Engedi.
Bwana arusi
15Hakika u mzuri, ee mpenzi wangu,
hakika u mzuri!
Macho yako ni kama ya hua!
Bibi arusi
16Hakika u mzuri ewe nikupendaye,
u mzuri kweli!
Majani mabichi yatakuwa kitanda chetu;
17mierezi itakuwa nguzo za nyumba yetu,
na miberoshi itakuwa dari yake.


Wimbo Ulio Bora1;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.