Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Tuesday 7 May 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 119...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote 
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomna ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe...

Yahweh tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyovimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Yahwe ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona,masikio ya kusikia sauti yako na kuitii..
Baba wa Mbinguni  tunaomba ukatupe neema ya kufuata
njia zako,tukasimamie Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu...
Ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu,ukatufanye chombo chema
ee Mungu wetu nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi....

Tazama watoto wako wenye shida/tabu,wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
kila mmoja na mahitaji yake
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipo kwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele...
Amina...!!


Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,Baba wa Mbinguni aendelee kuwatendea sawasawa na mapenzi yake...
Nawapenda.

1Heri watu wanaoishi bila kosa,
wanaozingatia sheria ya Mwenyezi-Mungu.
2Heri wanaozingatia matakwa yake,
wanaomtafuta kwa moyo wao wote,
3watu wasiotenda uovu kamwe,
bali daima hufuata njia zake.
4Ee Mungu, umetupatia kanuni zako
ili tuzishike kwa uaminifu.
5Laiti mwenendo wangu ungeimarika,
kwa kuyafuata masharti yako!
6Nikizingatia amri zako zote,
hapo kweli sitaaibishwa.
7Nitakusifu kwa moyo mnyofu,
nikijifunza maagizo yako maadilifu.
8Nitayafuata masharti yako;
usiniache hata kidogo.
Kutii sheria ya Mungu
9Kijana atatunzaje maisha yake kuwa safi?
Kwa kuyaongoza kadiri ya neno lako.
10Najitahidi kukutii kwa moyo wote;
usiniache nikiuke amri zako.
11Nimeshika neno lako moyoni mwangu,
nisije nikakukosea.
12Utukuzwe, ee Mwenyezi-Mungu!
Unifundishe masharti yako.
13Nitayarudia kwa sauti
maagizo yako yote uliyotoa.
14Nafurahi kufuata maamuzi yako,
kuliko kuwa na utajiri mwingi.
15Nazitafakari kanuni zako,
na kuzizingatia njia zako.
16Nayafurahia masharti yako;
sitalisahau neno lako.
Kufurahia sheria ya Mungu
17Unitendee mimi mtumishi wako kwa ukarimu,
nipate kuishi na kushika neno lako.
18Uyafumbue macho yangu,
niyaone maajabu ya sheria yako.
19Mimi ni mkimbizi tu hapa duniani;
usinifiche amri zako.
20Roho yangu yaugua kwa hamu kubwa
ya kutaka kujua daima maagizo yako.
21Wewe wawakemea wenye kiburi, walaanifu,
ambao wanakiuka amri zako.
22Uniepushe na matusi na madharau yao,
maana nimeyazingatia maamuzi yako.
23Hata kama wakuu wanakula njama dhidi yangu;
mimi mtumishi wako nitayatafakari maamuzi yako.
24Masharti yako ni furaha yangu;
hayo ni washauri wangu.
Kushika sheria ya Mungu
25Nagaagaa chini mavumbini;
unipe tena uhai kama ulivyoahidi.
26Nimeungama niliyotenda, nawe ukanijibu;
unifundishe masharti yako.
27Unifundishe namna ya kushika kanuni zako,
nami nitayatafakari matendo119:27 matendo yako: Au Mafundisho yako. yako ya ajabu.
28Niko hoi kwa uchungu;
unirudishie nguvu kama ulivyoahidi.
29Uniepushe na njia za upotovu;
unifundishe kwa wema sheria yako.
30Nimechagua njia ya uaminifu;
nimezingatia maagizo yako.
31Nazingatia maamuzi yako, ee Mwenyezi-Mungu;
usikubali niaibishwe!
32Nitafuata maelekezo ya amri zako,
maana unanipa maarifa zaidi.
Kuomba maarifa
33Ee Mwenyezi-Mungu, unifundishe kutii masharti yako;
nami nitayashika mpaka mwisho.
34Unieleweshe nipate kuishika sheria yako,
niifuate kwa moyo wangu wote.
35Uniongoze katika njia ya amri zako,
maana humo napata furaha yangu.
36Unipe ari ya kuzingatia maamuzi yako,
na si kwa ajili ya kupata faida isiyofaa.
37Uniepushe, nisifuate mambo ya upuuzi;
unioneshe njia yako, unipe uhai.
38Unitimizie mimi mtumishi wako ahadi yako;
ahadi unayowapa wale wanaokuheshimu.
39Uniokoe na lawama ninazoogopa;
maana maagizo yako ni mema.
40Natamani sana kuzitii kanuni zako;
unijalie uhai maana wewe ni mwadilifu.
Kutegemea sheria ya Mungu
41Fadhili zako zinijie, ee Mwenyezi-Mungu;
uniokoe kama ulivyoahidi.
42Hapo nitaweza kuwajibu hao wanaonitukana,
maana mimi nina imani sana na neno lako.
43Unijalie kusema ukweli wako daima,
maana tumaini langu liko katika maagizo yako.
44Nitatii sheria yako daima,
nitaishika milele na milele.
45Nitaishi katika uhuru kamili,
maana nazitilia maanani kanuni zako.
46Nitawatangazia wafalme maamuzi yako,
wala sitaona aibu.
47Furaha yangu ni kuzitii amri zako,
ambazo mimi nazipenda.
48Naziheshimu na kuzipenda amri zako;
nitayatafakari masharti yako.
Kuwa na imani na sheria ya Mungu
49Ukumbuke ahadi yako kwangu mimi mtumishi wako,
ahadi ambayo imenipa matumaini.
50Hata niwapo taabuni napata kitulizo,
maana ahadi yako yanipa uhai.
51Wasiomjali Mungu hunidharau daima,
lakini mimi sikiuki sheria yako.
52Ninapoyakumbuka maagizo yako ya tangu kale,
nafarijika, ee Mwenyezi-Mungu.
53Nashikwa na hasira kali,
nionapo waovu wakivunja sheria yako.
54Masharti yako yamekuwa wimbo wangu,
nikiwa huku ugenini.
55Usiku ninakukumbuka, ee Mwenyezi-Mungu,
na kushika sheria yako.
56Hii ni baraka kubwa kwangu,
kwamba nazishika kanuni zako.
Heshima kwa sheria ya Mungu
57Wewe, ee Mwenyezi-Mungu, ndiwe riziki yangu kuu;
naahidi kushika maneno yako.
58Naomba radhi yako kwa moyo wangu wote;
unionee huruma kama ulivyoahidi!
59Nimeufikiria mwenendo wangu,
na nimerudi nifuate maamuzi yako.
60Bila kukawia nafanya haraka
kuzishika amri zako.
61Waovu wametega mitego waninase,
lakini mimi sisahau sheria yako.
62Usiku wa manane naamka kukusifu,
kwa sababu ya maagizo yako maadilifu.
63Mimi ni rafiki ya wote wakuchao,
rafiki yao wanaozitii kanuni zako.
64Dunia imejaa fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu,
unifundishe masharti yako.
Ukamilifu wa sheria ya Mungu
65Umenitendea vema mimi mtumishi wako,
kama ulivyoahidi, ee Mwenyezi-Mungu.
66Unifundishe akili na maarifa,
maana nina imani sana na amri zako.
67Kabla ya kuniadhibu nilikuwa nikikosea,
lakini sasa nashika neno lako.
68Wewe ni mwema na mfadhili;
unifundishe masharti yako.
69Wenye kiburi wanasema uongo juu yangu,
lakini mimi nashika kanuni zako kwa moyo wote.
70Mioyo yao imejaa upumbavu,
lakini mimi nafurahia sheria yako.
71Nimefaidika kutokana na taabu yangu,
maana imenifanya nijifunze masharti yako.
72Sheria uliyoweka ni bora kwangu,
kuliko mali zote za dunia.
Ukamilifu wa sheria ya Mungu
73Mikono yako iliniumba na kuniunda;
unijalie akili nijifunze amri zako.
74Wakuchao wataniona na kufurahi,
maana tumaini langu liko katika neno lako.
75Najua hukumu zako ni adili, ee Mwenyezi-Mungu,
na kwamba umeniadhibu kwani wewe ni mwaminifu.
76Fadhili zako na zinipe faraja,
kama ulivyoniahidi mimi mtumishi wako.
77Unionee huruma nipate kuishi,
maana sheria yako ni furaha yangu.
78Wenye kiburi waaibike kwa maana wamenifanyia hila,
lakini mimi nitazitafakari kanuni zako.
79Wote wakuchao na waje kwangu,
wapate kuyajua maamuzi yako.
80Moyo wangu na uzingatie masharti yako,
nisije nikaaibishwa.
Sala wakati wa kudhulumiwa
81Niko hoi kwa kukungojea uniokoe;
naweka tumaini langu katika neno lako.
82Macho yangu yanafifia nikingojea ulichoahidi.
Nauliza: “Utakuja lini kunifariji?”
83Nimekunjamana kama kiriba katika moshi,
hata hivyo sijasahau masharti yako.
84Mimi mtumishi wako nitasubiri mpaka lini?
Utawaadhibu lini wale wanaonidhulumu?
85Wenye kiburi wamenichimbia mashimo,
watu ambao hawafuati sheria yako.
86Amri zako zote ni za kuaminika;
watu wananitesa bila haki; unisaidie!
87Karibu wangefaulu kuniangamiza,
lakini mimi sijavunja kanuni zako.
88Unisalimishe kadiri ya fadhili zako,
nipate kuzingatia maamuzi uliyotamka.
Sheria ya Mungu ni ya kutegemewa
89Neno lako, ee Mwenyezi-Mungu, ladumu milele;
limethibitika juu mbinguni.
90Uaminifu wako wadumu vizazi vyote,
umeiweka dunia mahali pake nayo yadumu.
91Kwa amri yako viumbe vyote vipo leo,
maana vitu vyote ni watumishi wako.
92Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu,
ningalikwisha angamia kwa taabu zangu.
93Sitasahau kamwe kanuni zako,
maana kwa hizo umenipa uhai.
94Mimi ni wako, uniokoe,
maana nimejitahidi kuzishika kanuni zako.
95Waovu wanivizia wapate kuniua;
lakini mimi natafakari masharti yako.
96Nimetambua kila kitu hufikia kikomo,
lakini amri yako ni kamilifu.
Kuipenda sheria ya Mungu
97Naipenda sana sheria yako!
Naitafakari mchana kutwa!
98Amri yako iko nami daima,
yanipa hekima kuliko maadui zangu.
99Ninaelewa kuliko waalimu wangu wote,
kwa kuwa nayatafakari maamuzi yako.
100Nawapita wazee kwa busara yangu,
kwa sababu nazishika kanuni zako.
101Najizuia nisifuate njia mbaya,
nipate kulizingatia neno lako.
102Sikukiuka maagizo yako,
maana wewe mwenyewe ulinifundisha.
103Maneno yako ni matamu sana kwangu;
naam, ni matamu kuliko asali!
104Kwa kanuni zako napata hekima,
kwa hiyo nachukia kila mwenendo mbaya.
Sheria ya Mungu ni mwanga
105Neno lako ni taa ya kuniongoza,
na mwanga katika njia yangu.
106Nimeapa na kuthibitisha kiapo changu,
kwamba nitashika maagizo yako adili.
107Ee Mwenyezi-Mungu, ninateseka mno;
unijalie uhai kama ulivyoahidi.
108Ee Mwenyezi-Mungu, upokee sala yangu ya shukrani;
na kunifundisha maagizo yako.
109Maisha yangu yamo hatarini daima,
lakini siisahau sheria yako.
110Waovu wamenitegea mitego,
lakini sikiuki kanuni zako.
111Maamuzi yako ni riziki kubwa kwangu milele;
hayo ni furaha ya moyo wangu.
112Nimekusudia kwa moyo wote
kufuata masharti yako milele.
Usalama katika sheria ya Mungu
113Nawachukia watu wanafiki,
lakini naipenda sheria yako.
114Wewe ni ngao yangu, kwako napata usalama;
naweka tumaini langu katika neno lako.
115Ondokeni kwangu, enyi waovu,
ili nipate kushika amri za Mungu wangu.
116Uniimarishe ulivyoahidi, nami nitaishi;
usikubali niaibike katika tumaini langu.
117Unitegemeze, niwe salama;
niwe daima msikivu kwa masharti yako.
118Unawakataa wote wanaokiuka masharti yako;
mawazo yao maovu ni ya bure.
119Waovu wote wawaona kuwa takataka,
kwa hiyo mimi napenda maamuzi yako.
120Natetemeka kwa kukuogopa wewe;
nimejaa hofu kwa sababu ya hukumu zako.
Utii wa sheria ya Mungu
121Nimefanya mambo mema na adili;
usiniache makuchani mwa maadui zangu.
122Uahidi kunisaidia mimi mtumishi wako;
usikubali wenye kiburi wanidhulumu.
123Macho yangu yanafifia nikingojea uniokoe,
nikingojea utimize uliyoahidi.
124Unitendee mimi mtumishi wako kadiri ya wema wako,
unifundishe masharti yako.
125Mimi ni mtumishi wako, unipe maarifa,
nipate kujua maamuzi yako.
126Ee Mwenyezi-Mungu, sasa ni wakati wa kufanya kitu,
kwa maana watu wanavunja sheria yako.
127Mimi, nazipenda amri zako,
kuliko hata dhahabu safi kabisa.
128Kwa hiyo, nafuata kanuni zako zote;119:128 nafuata kanuni zako zote: Maana katika Kiebrania si dhahiri.
kila njia potovu naichukia.
Hamu ya kutii sheria za Mungu
129Maamuzi yako ni ya ajabu;
kwa hiyo nayashika kwa moyo wote.
130Maelezo ya mafundisho yako huleta mwanga;
huwapa akili watu wasiojua kitu.
131Nafungua kinywa kwa hamu kubwa,
maana ninatamani sana amri zako.
132Unigeukie na kunionea huruma,
kama uwatendeavyo wanaokupenda.
133Uniimarishie hatua zangu kama ulivyoahidi;
usikubali mimi nitawaliwe na uovu.
134Unikomboe kutoka udhalimu wa binadamu,
ili nipate kuzishika kanuni zako.
135Uniangazie uso wako kwa wema,
unifundishe masharti yako.
136Macho yangu yabubujika machozi kama mto,
kwa sababu watu hawaishiki sheria yako.
Ukamilifu wa sheria ya Mungu
137Ee Mwenyezi-Mungu, wewe ni mwadilifu;
na hukumu zako ni za haki.
138Umetoa maamuzi yako,
kwa haki na uthabiti.
139Upendo wangu kwako wanifanya niwake hasira,
maana maadui zangu hawajali maneno yako.
140Ahadi yako ni hakika kabisa,
nami mtumishi wako naipenda.
141Mimi ni mdogo na ninadharauliwa;
hata hivyo sisahau kanuni zako.
142Uadilifu wako ni wa haki milele;
sheria yako ni ya kweli.
143Taabu na huzuni vimenipata,
lakini amri zako ndizo furaha yangu.
144Maamuzi yako ni ya haki daima;
unijalie maarifa nipate kuishi.
Kuomba usalama
145Nakulilia kwa moyo wangu wote;
unijibu, ee Mwenyezi-Mungu, nifuate kanuni zako.
146Nakulilia, unisalimishe;
nipate kuyazingatia maamuzi yako.
147Naamka kabla ya pambazuko na kukuomba msaada;
naweka tumaini langu katika maneno yako.
148Nakaa macho usiku kucha,
ili nitafakari juu ya maagizo yako.
149Kwa fadhili zako, ee Mwenyezi-Mungu, unisikie;
unisalimishe kwa uadilifu wako.
150Wale wanaonidhulumu vibaya wanakaribia,
hao wako mbali kabisa na sheria yako.
151Lakini wewe u karibu nami, ee Mwenyezi-Mungu,
na amri zako zote ni za kuaminika.
152Tangu zamani, nimejifunza maamuzi yako;
ambayo umeyaweka hata yadumu milele.
Kuomba msaada
153Uangalie mateso yangu, uniokoe,
kwa maana sikuisahau sheria yako.
154Unitetee na kunikomboa;
unijalie uhai kama ulivyoahidi.
155Waovu hawataokolewa kamwe,
maana hawajali juu ya masharti yako.
156Huruma yako ni kubwa, ee Mwenyezi-Mungu,
unijalie uhai kama ulivyoahidi.
157Maadui na wadhalimu wangu ni wengi,
lakini mimi sikiuki maamuzi yako.
158Niwaonapo wahaini hao nachukizwa mno,
kwa sababu hawazishiki amri zako.
159Tazama, ee Mungu, ninavyozipenda kanuni zako!
Unijalie uhai kadiri ya fadhili zako.
160Kitovu cha neno lako ni ukweli,
maagizo yako yote adili, yadumu milele.
Kuzingatia sheria ya Mungu
161Wakuu wanidhulumu bila kisa,
lakini mimi naheshimu maneno yako kwa moyo wote.
162Nafurahi kwa sababu ya neno lako,
kama mtu aliyekuta kitu cha thamani kuu.
163Nachukia kabisa uongo,
lakini naipenda sheria yako.
164Nakusifu mara saba kila siku,
kwa sababu ya maagizo yako adili.
165Wapendao sheria yako wana amani kuu;
hakuna kinachoweza kuwaangusha.
166Ee Mwenyezi-Mungu, nakungojea uniokoe;
mimi natimiza amri zako.
167Nazingatia maamuzi yako;
nayapenda kwa moyo wote.
168Nazingatia kanuni na maamuzi yako;
wewe wauona mwenendo wangu wote.
Kuomba msaada
169Kilio changu kikufikie, ee Mwenyezi-Mungu!
Unijalie akili kama ulivyoahidi.
170Ombi langu likufikie;
uniokoe kama ulivyoahidi.
171Nitasema sifa zako mfululizo,
maana wanifundisha masharti yako.
172Nitaimba juu ya neno lako,
maana amri zako zote ni za haki.
173Uwe daima tayari kunisaidia,
maana nimeamua kufuata kanuni zako.
174Natazamia sana uniokoe, ee Mwenyezi-Mungu;
sheria yako ndiyo furaha yangu.
175Unijalie kuishi nipate kukusifu;
na maagizo yako yanisaidie.
176Natangatanga kama kondoo aliyepotea;
uje kunitafuta mimi mtumishi wako,
maana sikusahau amri zako.


Zaburi119;1-176

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 6 May 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 118...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Haleluyah ni siku/wiki/mwezi   mwingine tena Mungu wetu ametuchagua

na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Si kwamba sisi tumetenda mema sana wala si kwa nguvu zetu
si kwa utashi wetu wala si kwa akili zetu si kwamba sisi
ni wazuri mno si kwa uwezo wetu sisi kuwa hivi tulivyo leo hii
Ni kwa rehema/neema zake ni kwa mapenzi yake Mungu wetu....

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari kwa majukumu yetu
Sifa na Utukufu tunakurudshia Mungu wetu....!!

Yeye huwaporomosha wakuu wenye nguvu, watawala wa dunia huwafanya kuwa si kitu. Mara tu wanaposimikwa na kuanza kuota, hata kabla hawajatoa mizizi kama miti udongoni, Mwenyezi-Mungu akiwapulizia hunyauka, kimbunga huwapeperusha kama makapi!
Tazama jana imepita ee Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni siku nyingine Jehovah tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
 Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Jehovah usitutie majaribu Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni utufunike kwa Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona
Kwakupigwa kwake sisi tumepata kupona...

Mungu Mtakatifu auliza hivi: “Nani basi, mtakayemlinganisha nami? Je, kuna mtu aliye kama mimi?” Inueni macho yenu juu mbinguni! Je, ni nani aliyeziumba nyota hizo? Ni yule aziongozaye kama jeshi lake, anayeijua idadi yake yote, aziitaye kila moja kwa jina lake. Kwa sababu yeye ni mwenye nguvu nyingi, hakuna hata moja inayokosekana.
Yahweh tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Baba wa Mbinguni tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Enyi watu wa Israeli wazawa wa Yakobo, kwa nini mnalalamika na kusema: “Mwenyezi-Mungu hatujali sisi! Mungu wetu hajali haki yetu!” Je, nyinyi bado hamjui? Je, hamjapata kusikia? Mwenyezi-Mungu ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu duniani. Yeye hafifii kamwe wala kuishiwa nguvu. Maarifa yake hayachunguziki. Yeye huwapa uwezo walio hafifu, wanyonge huwapa nguvu. Hata vijana watafifia na kulegea; naam, wataanguka kwa uchovu. Lakini wote wanaomtumainia Mwenyezi-Mungu, watapata nguvu mpya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai; watakimbia bila kuchoka; watatembea bila kulegea.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,wote wanaopotia magumu/majaribu mbalimbali
Mungu wetu tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
 kila mmoja na mahitaji yake 
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Baba wa Mbinguni ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako
wakasimaie Neno lako nalo likaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kuomba kwetu
Mungu wetu ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina...!!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami
Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea 
kama inavyompendeza yeye....
Nawapenda.

Sala ya shukrani
1 Taz Zab 100:5; 106:1; 136:1 Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, kwa kuwa ni mwema,
kwa maana fadhili zake zadumu milele.
2Watu wa Israeli na waseme:
“Fadhili zake zadumu milele.”
3Wazawa wa Aroni na waseme:
“Fadhili zake zadumu milele.”
4Wote wamchao Mwenyezi-Mungu na waseme:
“Fadhili zake zadumu milele.”
5Katika taabu yangu nilimwomba Mwenyezi-Mungu,
naye akanisikia na kuniweka huru.
6 Taz Ebr 13:6 Mwenyezi-Mungu yuko nami, siogopi kitu;
binadamu ataweza kunifanya nini?
7Mwenyezi-Mungu yuko nami, kunisaidia;
nami nitawaona maadui zangu wameshindwa.
8Afadhali kukimbilia usalama kwa Mwenyezi-Mungu,
kuliko kumtumainia mwanadamu.
9Afadhali kukimbilia usalama kwa Mwenyezi-Mungu,
kuliko kuwatumainia viongozi wa dunia.
10Mataifa yote yalinizingira,
lakini kwa jina la Mwenyezi-Mungu nikayaangamiza!
11Yalinizunguka kila upande,
lakini kwa jina la Mwenyezi-Mungu, nikayaangamiza!
12Yalinizunguka, mengi kama nyuki,
lakini yakateketea kama kichaka motoni;
kwa jina la Mwenyezi-Mungu niliyaangamiza!
13Nilishambuliwa mno karibu nishindwe,
lakini Mwenyezi-Mungu alinisaidia.
14Mwenyezi-Mungu ni nguvu yangu kuu;
yeye mwenyewe ndiye wokovu wangu.
15Sauti za furaha ya ushindi zasikika hemani mwao waadilifu:
“Mkono wa Mwenyezi-Mungu umetenda mambo makuu!
16Mkono wa nguvu wa Mwenyezi-Mungu umeleta ushindi!
Mkono wa Mwenyezi-Mungu umetenda mambo makuu!”
17Sitakufa, bali nitaishi,
na kusimulia matendo ya Mwenyezi-Mungu.
18Mwenyezi-Mungu ameniadhibu sana,
lakini hakuniacha nife.
19Nifungulie milango ya watu waadilifu,
niingie na kumshukuru Mwenyezi-Mungu!
20Huu ndio mlango wa Mwenyezi-Mungu,
watu waadilifu watapitia humo.
21Nakushukuru, ee Mungu kwa kunijibu;
kwa sababu wewe ni wokovu wangu.
22 Taz Luka 20:17; Mate 4:11; 1Pet 2:7 Jiwe walilokataa waashi,
limekuwa jiwe kuu la msingi. Taz Mat 21:42; Marko 12:10-11
23Hiyo ni kazi yake Mwenyezi-Mungu
nayo ni ya ajabu sana kwetu.
24Hii ndiyo siku aliyoifanya Mwenyezi-Mungu;
tushangilie na kufurahi.
25 Taz Mat 21:9; Marko 11:9; Yoh 12:13 Tafadhali utuokoe, ee Mwenyezi-Mungu!
Tafadhali utufanikishe, ee Mwenyezi-Mungu!
26 Taz Mat 21:9; 23:39; Marko 11:9; Luka 13:35; 19:38; Yoh 12:13 Abarikiwe huyo ajaye kwa jina la Mwenyezi-Mungu!
Twawabariki kutoka nyumbani mwa Mwenyezi-Mungu
27Mwenyezi-Mungu ni Mungu;
yeye ametujalia mwanga wake
Shikeni matawi ya sherehe,
mkiandamana mpaka madhabahuni.
28Wewe ni Mungu wangu, nami ninakushukuru;
ninakutukuza, ee Mungu wangu.
29Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema,
kwa maana fadhili zake zadumu milele.


Zaburi118;1-29

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 3 May 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 117...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Mataifa yote si kitu mbele yake; kwake ni vitu duni kabisa na batili. Mtamlinganisha Mungu na nini basi, au ni kitu gani cha kumfananisha naye?
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Je, anafanana na kinyago? Hicho, fundi hukichonga, mfua dhahabu akakipaka dhahabu, na kukitengenezea minyororo ya fedha! Au ni sanamu ya mti mgumu? Hiyo ni ukuni mtu anaochagua, akamtafuta fundi stadi, naye akamchongea sanamu imara!
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe



Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Je, nyinyi bado hamjui? Je, hamjapata kusikia? Je, hamkuambiwa tangu mwanzo? Je, hamjafahamu mwanzo wa dunia? Dunia iliumbwa na huyo aketiye juu ya mbingu; kutoka huko wakazi wa dunia ni kama panzi! Yeye amezitandaza mbingu kama pazia, na kuzikunjua kama hema la kuishi.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....
Nawapenda.

Kumsifu Mungu
1 Taz Rom 15:11 Enyi mataifa yote, msifuni Mwenyezi-Mungu!
Enyi watu wote mhimidini!
2Maana fadhili zake kwetu sisi ni kuu;
uaminifu wake Mwenyezi-Mungu wadumu milele!
Msifuni Mwenyezi-Mungu!



Zaburi117;1-2

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 2 May 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 116...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu katika yote....

Mungu wetu Baba yetu,Muumba wetu Muumba wa Mbingu na Nchi
Muumba wa vyote vilivyomo vinavyoonekana na visivyoonekana
Mungu wa walio hai,Mungu  mwenye huruma,Mungu wa upendo
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Asante kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu

Neema yako yatutosha ee Mungu wetu....!!

Nani awezaye kupima maji ya bahari kwa konzi yake, kuzipima mbingu kwa mikono yake? Nani awezaye kuutia udongo wa dunia kikombeni; kuipima milima kwa mizani au vilima kwa kipimo cha uzani?
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya
Kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba ukatupe neema
ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea
Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe
na yule mwovu na kazi zake zote
Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu
Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa Damu
ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Nani awezaye kuiongoza akili ya Mwenyezi-Mungu, au kuwa mshauri wake na kumfunza? Mwenyezi-Mungu alimtaka nani shauri, ndipo akapata kuwa mwenye ujuzi? Nani aliyemfunza njia za haki? Nani aliyemfundisha maarifa, na kumwonesha namna ya kuwa na akili?
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi ukatupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji
Tusipungukiwe katika mahitaji yetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe kama inavyokupendeza wewe....
Yahweh  tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni

Yahweh ukatupe akili ya kutambua mema na mabaya
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu
Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
ukatuguse kwa mkono wako wenye nguvu
Ukatufanye chombo chema ee Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Kwake mataifa ni kama tone la maji katika ndoo, ni kama vumbi juu ya mizani. Kwake visiwa ni vyepesi kama vumbi laini. Kuni zote za Lebanoni na wanyama wake wote havitoshi kwa sadaka ya kuteketezwa mbele yake.
Mungu wetu tunawaweka mikononi mwako wenye shida/tabu,
wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali
Jehovah ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu kila mmoja na mahitaji yake...
Mungu wetu tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda kinyume nawe
Yahweh tunaomba ukawape neema ya kujiombea,kufuata njia zako nazo zikawaweke huru...
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao....
Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako,
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele....
Amina..!

Asanteni sana wapendwa katika Kristo Yesu kwakuwa nami,
Mungu Baba aendelee kuwatendea sawasawa na mapezni yake...

Nawapenda.

Shukrani kwa kuokolewa kifoni
1Nampenda Mwenyezi-Mungu,
kwa maana anisikia,
maana amesikia kilio cha ombi langu.
2Yeye amenitegea sikio,
hivyo nitamwomba muda wote niishio.
3Hatari ya kifo ilinizunguka,
vitisho vya kaburi vilinivamia;
nilijawa na mahangaiko na majonzi.
4Kisha nikamlilia Mwenyezi-Mungu:
“Ee Mwenyezi-Mungu, tafadhali unisalimishe!”
5Mwenyezi-Mungu amejaa wema na uaminifu;
Mungu wetu ni mwenye huruma.
6Mwenyezi-Mungu huwalinda wanyofu;
nilipokuwa nimekandamizwa aliniokoa.
7Uwe na utulivu mkuu, ee nafsi yangu,
maana Mwenyezi-Mungu amenitendea mema.
8Ameniokoa kifoni na kufuta machozi yangu;
akanilinda nisije nikaanguka.
9Nitatembea mbele yake Mwenyezi-Mungu,
katika nchi ya watu walio hai.
10 Taz 2Kor 4:13 Nilikuwa na imani hata niliposema:
“Mimi nimetaabika mno.”
11Hata nilisema kwa hofu yangu:
“Binadamu wote hawaaminiki!”
12Nimrudishie nini Mwenyezi-Mungu,
kwa ukarimu wote alionitendea?
13Nitamtolea tambiko ya divai kwa kunikomboa,
nitaomba kwa jina lake Mwenyezi-Mungu.
14Nitamtimizia Mwenyezi-Mungu nadhiri zangu,
mbele ya watu wake wote.
15Kifo cha waaminifu wake Mwenyezi-Mungu
si jambo dogo mbele yake.
16Ee Mwenyezi-Mungu, mimi ni mtumishi wako;
ni mtumishi wako, mtoto wa mjakazi wako;
umenifungulia vifungo vyangu.
17Nitakutolea tambiko za shukrani,
na kukupa heshima zangu.
18Nitakutimizia ahadi zangu, ee Mwenyezi-Mungu
mbele ya watu wako wote,
19waliokusanyika hekaluni mwako,
katikati ya Yerusalemu.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!


Zaburi116;1-19

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 1 May 2019

Kikombe Cha Asubuhi ;Zaburi 115...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote...

Asante  Mungu wetu kwa wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwatayari kwa majukumu yetu


Utukuzwe ee Mungu wetu,usifiwe Baba wa Mbinguni

Neema yako yatutosha  Mungu wetu..!

Sauti ya mtu anaita jangwani: “Mtayarishieni Mwenyezi-Mungu njia, nyosheni barabara kuu kwa ajili ya Mungu wetu. Kila bonde litasawazishwa, kila mlima na kilima vitashushwa; ardhi isiyo sawa itafanywa sawa, mahali pa kuparuza patalainishwa.
Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,tukijishusha na kujiachilia mikononi mwako
Mungu wetu tunaomba utusamehe dhambi zetu zote
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wale wote waliotukosea,Usitutie majaribuni Mungu wetu tunaomba utuepushe na yule mwovu na kazi zake zote,Jehovah ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni tunaomba utufunike kwa  Damu ya Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti,
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona....

Kisha utukufu wa Mwenyezi-Mungu utafunuliwa, na watu wote pamoja watauona. Mwenyezi-Mungu mwenyewe ametamka hayo.” Sikiliza! Kuna sauti inasema, “Tangaza!” Nami nikauliza, “Nitangaze nini?” Naye: “Tangaza: Binadamu wote ni kama majani; uthabiti wao ni kama ua la shambani. Majani hunyauka na ua hufifia, Mwenyezi-Mungu avumishapo upepo juu yake. Hakika binadamu ni kama majani.
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe ubunifu na maarifa 
katika utendaji
Jehovah nasi tukatende sawasawa na mapenzi yako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki ridhiki zetu
ziingiazo/zitokazo
Mungu wetu nasi tunaomba ukatupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Mungu wetu ukatupe kama inavyokupendeza wewe

Jehovah tunayaweka maisha yetu mikononi mwako
Baba wa Mbinguni tunaomba ukabariki nyumba/ndoa zetu,
watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote wanaotuzunguka
Jehovah tunaomba ulinzi wako kwetu na kwa vyote tunavyo vimiliki
Yahweh tunaomba ukatubariki tuingiapo/tutokapo
Mungu wetu tunaomba ukavibariki vyote tunavyoenda kugusa/kutumia
Baba wa Mbinguni ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia
Baba wa Mbinguni tukawe salama rohoni
Mfalme wa amani amani yako ikatawale katika maisha yetu
Mungu wetu ukatupe macho ya kuona na masikio ya kusikia 
sauti yako na kuitii
Baba wa Mbinguni tunaomba ukatupe neema ya kufuata njia zako
Yahweh tukasimamie Neno lako amri na sheria zako siku zote 
za maisha yetu

Mungu  wetu ukaonekane katika maisha yetu popote tupitapo na ikajulikane kwamba upo 

Neema zako zikawe nasi Nuru yako ikaangaze katika maisha yetu
Ukatufanye barua njema ee Mungu wetu nasi tukasomeke kama
inavyokupendeza wewe
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi...

Majani hunyauka na ua hufifia, lakini neno la Mungu wetu ladumu milele.” Nenda juu ya mlima mrefu, ewe Siyoni, ukatangaze habari njema. Paza sauti yako kwa nguvu, ewe Yerusalemu, ukatangaze habari njema. paza sauti yako bila kuogopa. Iambie miji ya Yuda: “Mungu wenu anakuja.” Bwana Mungu anakuja na nguvu, kwa mkono wake anatawala. Zawadi yake iko pamoja naye, na tuzo lake analo. Atalilisha kundi lake kama mchungaji, atawakusanya wanakondoo mikononi mwake, atawabeba kifuani pake, na kondoo wanyonyeshao atawaongoza polepole.
Tazama wenye shida/tabu,Mungu wetu tunaomba
 ukawaguse kila mmoja na mahitaji yake
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawasamehe pale walipokwenda
kinyume nawe
Mungu wetu ukawape neema ya kujiombea,macho ya rohoni,masikio yakusikia sauti yako,wakafuate njia zako nazo zikawaweke huru
Mungu wetu tunaomba ukasikie kulia kwao
Baba wa Mbinguni tunomba ukawafute machozi yao
Nuru yako ikaangaze katika maisha yao
Mungu wetu tunaomba ukawatendee sawasawa na mapenzi yako
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele
Amina....!!!


Wapendwa katika Kristo Yesu asanteni sana
kwakuwanami/kunisoma

Mungu Baba aendelee kuwabariki na kuwatendea
kama inavyompendeza yeye
Amani ya Bwana wetu Yesu Kristo na upendo wa Mungu Baba
ukae nanyi daima....

Nawapenda.

Mungu mmoja wa kweli
1Sio sisi, ee Mwenyezi-Mungu, sio sisi;
bali wewe peke yako utukuzwe,
kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako.
2Kwa nini mataifa yaseme:
“Mungu wenu yuko wapi?”
3Mungu wetu yuko mbinguni;
yeye hufanya yote anayotaka.
4 Taz Zab 135:15-18; Ufu 9:20 Miungu yao ni ya fedha na dhahabu;
imetengenezwa kwa mikono ya wanadamu.
5Ina vinywa, lakini haisemi.
Ina macho, lakini haioni.
6Ina masikio, lakini haisikii.
Ina pua, lakini hainusi.
7Ina mikono, lakini haipapasi.
Ina miguu, lakini haitembei.
Haiwezi kamwe kutoa sauti.
8Wote wanaoitengeneza wanafanana nayo,
kadhalika na wote wanaoitumainia.
9Enyi Waisraeli, mtumainieni Mwenyezi-Mungu;
yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.
10Enyi wazawa wa Aroni, mtumainieni Mwenyezi-Mungu;
yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.
11Enyi mnaomcha Mwenyezi-Mungu, mtumainini,
yeye ndiye msaada wenu na ngao yenu.
12Mwenyezi-Mungu atukumbuka na atatubariki;
atawabariki watu wa Israeli,
atawabariki wazawa wa Aroni.
13 Taz Ufu 11:18; 19:5 Atawabariki wote wamchao,
atawabariki wakubwa na wadogo.
14Mwenyezi-Mungu awajalieni muongezeke;
awajalieni muongezeke nyinyi na wazawa wenu!
15Mbarikiwe na Mwenyezi-Mungu,
aliyeziumba mbingu na dunia.
16Mbingu ni mali yake Mwenyezi-Mungu,
bali dunia amewapa binadamu.
17Wafu hawamsifu Mwenyezi-Mungu,
wala wale wanaoshuka katika nchi ya kimya.
18Lakini sisi tulio hai twamsifu Mwenyezi-Mungu;
tutamsifu sasa na hata milele.
Msifuni Mwenyezi-Mungu!

Zaburi115;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.