Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 3 November 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 19...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tumshukuru Mungu wetu katika yote..

Mtakatifu..!Mtakatifu.!Mtakatifu..!Baba wa Mbinguni..
Mungu wetu,Baba yetu,Muumba wetu,Mungu wa wote walio hai..
Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo...
Muweza wa yote,kimbilio letu,Mungu mwenye huruma,Mponyaji wetu
Baba wa upendo,Baba wa yatima,Baba wa baraka na amani..
Jehovah Jireh..!Jehovah Rapha..!Jehovah Nissi..!Jehovah Raah..!
Jehovah Shammah,Jehovah Shalom..!Emanueli-Mungu pamoja nasi..!!

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa kutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea
kuiona leo hii..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kuwa tayari katika majukumu yetu..

Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachilia mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Tunaomba utusamehe makosa yetu yote tuliyoyafanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua Jehovah..
Yahweh nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea..
Mungu wetu tunaomba utuepushe katika majaribu Yahweh utuokoe
na yule mwovu na kazi zake zote..
Baba wa Mbinguni tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Mungu wetu utufunike kwa damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Hatimaye, ndugu, tuombeeni ili ujumbe wa Bwana uzidi kuenea upesi na kupokelewa kwa heshima kama vile ulivyo kati yenu. Ombeni pia ili Mungu atuokoe na watu wapotovu na waovu, maana si wote wanauamini ujumbe huu. Lakini Bwana ni mwaminifu. Yeye atawaimarisheni na kuwalinda salama na yule Mwovu. Naye Bwana anatupatia tumaini kubwa juu yenu, na hatuna shaka kwamba mnafanya na mtaendelea kufanya yale tuliyowaambieni. Bwana aiongoze mioyo yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.

Jehovah tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu Yahweh
ukatupe ubunifu,maarifa katika yote tunayoenda kufanya
Baba wa Mbinguni tukafanye/kutenda sawasawa na mapenzi yako..
Mungu wetu ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo...
 Yahweh nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Jehovah tunaomba tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Yahweh ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Ndugu, tunawaamuru kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo, mjiepushe na ndugu wote walio wavivu na ambao hawafuati maagizo tuliyowapa. Nyinyi wenyewe mnajua kwamba mnapaswa kufuata mfano wetu. Sisi tulipokuwa nanyi hatukuwa wavivu; hatukula chakula kwa mtu yeyote bila ya kumlipa. Tulifanya kazi kwa bidii na taabu mchana na usiku ili tusiwe mzigo kwa mtu yeyote kati yenu. Tulifanya hivyo si kwa kuwa hatuna haki ya kutaka msaada wenu, ila kwa sababu tunataka kuwapeni mfano. Tulipokuwa pamoja nanyi tulikuwa tukiwaambieni, “Mtu yeyote asiyependa kufanya kazi, asile chakula.” Tunasema mambo hayo kwa sababu tumesikia kwamba wako baadhi yenu ambao ni wavivu na ambao hawafanyi chochote, isipokuwa tu kujiingiza katika mambo ya watu wengine. Kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo tunawaamuru na kuwaonya watu hao wawe na nidhamu na kufanya kazi ili wajipatie maslahi yao wenyewe. Lakini nyinyi ndugu, msichoke kutenda mema. Huenda kwamba huko kuna mtu ambaye hatautii huu ujumbe tunaowapelekeeni katika barua hii. Ikiwa hivyo, basi, mfichueni mtu huyo na msiwe na uhusiano wowote naye, kusudi aone aibu. Lakini msimtendee mtu huyo kama adui, bali mwonyeni kama ndugu.

Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote
wanaotuzunguka,Mungu wetu tunaomba ulinzi wako kwetu
na kwa vyote tunavyo vimiliki..Baba wa Mbinguni ukatamalaki na
kutuatamia,Ukatubariki na kututendea kama inavyokupendeza wewe
Yahweh ukatupe neema ya kusimamia Neno lako amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu,Ukatuokoe na majivuno,ubinafsi,fitina,
kiburi,unafiki,usengenyaji,uchoyo,makwazo na ukatupe neema
ya kuombeana/kujiombea,kufuata njia zako na kuelimishana/kuonyana
kwa upole na amani,Upendo kati yetu na ukadumu..
Tukawe barua njema popote tupitapo na tukasome vyema..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Bwana mwenyewe ambaye ndiye chanzo cha amani, awajalieni amani siku zote kwa kila namna. Bwana awe nanyi nyote. Kwa mkono wangu mwenyewe naandika hivi: Salamu kutoka kwa Paulo! Hivi ndivyo ninavyotia sahihi kila barua; ndivyo ninavyoandika. Tunawatakieni nyote neema ya Bwana wetu Yesu Kristo.

Mungu wetu ukawaguse kwa mkono wako na ukawape neema
ya kujiombea wagonjwa ukawape uponyaji wa mwili na roho
wenye njaa ukawape chakula na kubariki mashamba yao..
wanaopitia magumu/majaribu baba ukawape njia ya kuvuka..
waliokatika vifungo mbali mbali vya yule mwovu Mungu wetu
ukawafungue na kuwaweka huru,ukawape amani moyoni na
ukawape neema ya kujua njia zako na kufuata ili wawe huru..
ee Mungu wetu ukasikie kilio cha watoto wako Baba ukawafute
machozi na ukawatendee kama inavyo kupendeza wewe..


Lakini nyinyi wapenzi wangu, kumbukeni yale mliyoambiwa hapo awali na mitume wa Bwana wetu Yesu Kristo. Waliwaambieni: “Siku za mwisho, watatokea watu watakaowadhihaki nyinyi, watu wafuatao tamaa zao mbaya.” Hao ndio wanaosababisha mafarakano, watu wa fikira za kidunia, wasio na Roho wa Mungu. Lakini nyinyi, wapenzi wangu, jijengeni wenyewe juu ya imani yenu takatifu kabisa. Salini kwa nguvu ya Roho Mtakatifu, na kudumu katika upendo wa Mungu, mkimngojea Bwana wetu Yesu Kristo ambaye, kwa huruma yake, atawajalieni uhai wa milele. Muwe na huruma kwa watu walio na mashaka; waokoeni kwa kuwanyakua kutoka motoni. Lakini kwa wengine muwe na huruma pamoja na tahadhari, mkichukia hata mavazi yao yenye madoa ya tamaa zao mbaya.

Sifa na Utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina...!

Asanteni sana wapendwa katika Bwana kwakuwa nami
Baba wa upendo aendelee kuwabariki na kuwatendea
sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda.


Nchi waliyopewa kabila la Simeoni

1Kura ya pili ilizipata koo za kabila la Simeoni na sehemu yao ya nchi ilikuwa imezungukwa na ile ya kabila la Yuda. 2Kabila la Simeoni lilipata miji ya Beer-sheba, Sheba, Molada 3Hasar-shuali, Bala, Esemu, 4Eltoladi, Bethuli, Horma, 5Siklagi, Beth-markabothi, Hasar-susa, 6Beth-lebaothi na Sharuheni. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake. 7Pia kulikuwa na miji ya En-rimoni, Etheri, na Ashani. Jumla ya miji waliyopewa ni minne pamoja na vijiji vyake. 8Taz 1Nya 4:28-33 Pamoja na vijiji vyote vilivyoizunguka miji hiyo hadi Baalath-beeri, (au Rama) ya Negebu. Hizo zote ni sehemu zilizopewa koo za kabila la Simeoni. 9Kwa vile eneo lililopewa kabila la Yuda lilikuwa kubwa kuliko kabila hilo lilivyohitaji, sehemu ya eneo lake lilipewa kabila la Simeoni.

Nchi waliyopewa kabila la Zebuluni

10Kura ya tatu ilizipata koo za kabila la Zebuluni. Eneo lao lilienea hadi Saridi. 11Kutoka huko mpaka wake ulikwenda magharibi hadi Mareali, ukapitia pembeni mwa Dabeshethi na kwenda kwenye kijito kilichoko mashariki ya Yokneamu. 12Kutoka Saridi, mpaka huo ulielekea mashariki hadi kwenye mpaka wa Kisloth-tabori, na kutoka huko ukapita Daberathi hadi Yafia. 13Kutoka Yafia uliendelea mashariki hadi Gath-heferi, Eth-kasini, na kuendelea hadi Rimoni ambako ulipanda kuelekea Nea. 14Upande wa kaskazini mpaka uligeuka kuelekea Hanathoni na kuishia kwenye bonde la Yiftaheli. 15Ukajumuisha miji ya Katathi, Nahalali, Shimroni, Yidala na Bethlehemu. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na miwili pamoja na vijiji vyake. 16Hiyo ndiyo sehemu zilizopewa koo za kabila la Zebuluni miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

Nchi ya kabila la Isakari

17Kura ya nne ilizipata koo za kabila la Isakari. 18Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya Yezreeli, Kesulothi, Shunemu, 19Hafaraimu, Shioni, Anaharathi, 20Rabithi, Kishioni, Ebesi, 21Remethi, En-ganimu, En-hada na Beth-pasesi. 22Kadhalika, mpaka wao ulifika Tabori, Shahasuma, Beth-shemeshi na kuishia kwenye mto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake. 23Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Isakari; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

Nchi ya kabila la Asheri

24Kura ya tano ilizipata koo za kabila la Asheri. 25Eneo la nchi yao lilikuwa na miji ya Helkathi, Hali, Beteni, Akshafi, 26Alameleki, Amadi na Mishali. Kwa upande wa magharibi mpaka uligusana na Karmeli na Shihor-libnathi. 27Kisha ukageuka kuelekea mashariki kwenda Beth-dagoni ambako unagusana na Zebuluni na bonde la Iftaheli. Halafu ukaendelea kaskazini hadi Beth-emeki, Neieli na kuzidi kuelekea kaskazini hadi Kabuli, 28Ebroni, Rehobu, Hamoni, Kana hadi Sidoni Kuu. 29Hapo, mpaka uligeuka kuelekea Rama na kufikia kwenye mji wa Tiro uliokuwa na ngome. Kisha ukageuka kuelekea Hosa na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. Miji mingine iliyokuwamo ni Maharabu, Akzibu, 30Uma, Afeka na Rehobu. Jumla ya miji waliyopewa ni ishirini na miwili pamoja na vijiji vyake. 31Sehemu hizo ndizo zilizopewa koo za kabila la Asheri; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

Nchi ya kabila la Naftali

32Kura ya sita ilizipata koo za kabila la Naftali. 33Mpaka wake ulianzia Helefu na mwaloni mwa Zaananimu, ukapita Adami-nekebu na Yabneeli hadi Lakumu na kuishia kwenye mto Yordani. 34Kutoka hapo mpaka ulikwenda magharibi kuelekea Aznoth-tabori; toka huko ukaenda Hukoki na kugusana na pembe ya kusini ya eneo la kabila la Zebuluni; kisha kugusana na eneo la kabila la Asheri upande wa magharibi, na kugusana na eneo la kabila la Yuda. Kwa upande wa mashariki mpaka ukiingilia kwenye mto Yordani.19:34 Yordani: Makala ya Kiebrania: Yuda mtoni Yordani. 35Miji yao iliyokuwa na ngome ni Zidimu, Zeri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi, 36Adama, Rama, Hazori, 37Kedeshi, Edrei, En-hazori, 38Yironi, Migdaleli, Horemu, Beth-anathi na Beth-shemeshi. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na tisa pamoja na vijiji vyake. 39Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Naftali; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

Nchi ya kabila la Dani

40Kura ya saba ilizipata koo za kabila la Dani. 41Eneo la nchi yao lilikuwa na miji ya Sora, Eshtaoli, Ir-shemeshi 42Shaalabini, Aiyaloni, Yithla, 43Eloni, Timna, Ekroni 44Elteke, Gibethoni, Baalathi, 45Yehudi, Bene-beraki, Gath-rimoni, 46Me-yarkoni na Rakoni na nchi iliyokuwa karibu na Yopa. 47Taz Amu 18:27-29 Watu wa kabila la Dani walipopoteza nchi yao, walikwenda na kuushambulia mji wa Leshemu. Waliushinda na kuuteka, na baada ya kuwaua wakazi wake wote, waliumiliki halafu wakabadili jina la mji huo kuwa Dani; jina ambalo lilikuwa ni la babu yao. 48Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Dani; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.

Ugawanyaji wa mwisho

49Walipomaliza kugawiana sehemu zote za nchi, Waisraeli walimpa Yoshua, mwana wa Nuni, sehemu yake katikati yao. 50Kulingana na amri ya Mwenyezi-Mungu walimpa mji ambao aliuchagua yeye mwenyewe, yaani Timnath-sera, ambao ulikuwa katika nchi ya milima ya Efraimu. Naye Yoshua akaujenga upya mji huo na kukaa humo.
51Basi, kuhani Eleazari na Yoshua, mwana wa Nuni, pamoja na viongozi wa makabila ya Waisraeli waligawa sehemu hizo kwa kura mbele ya Mwenyezi-Mungu mlangoni mwa hema la mkutano huko Shilo. Basi, wakakamilisha kuigawa nchi.

Yoshua 19;1-51

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 2 November 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 18...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Haleluyah Mungu wetu yu mwema sana tumshukuru na kumsifu..

Mungu wetu Baba yetu,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo..
Baba wa Mbinguni,Mfalme wa Amani,Baba wa huruma,Mungu wa
wajane,Baba wa yatima,Mponyaji wetu,Mlinzi wetu,Kimbilio letu..
Uhimidiwe Yahweh,Uabudiwe milele,Utukuzwe Baba wa Mbinguni,
Usifiwe Mungu wetu,Unastahili sifa,Mwimbieni Mungu sifa,Mwimbieni.!
Mwimbieni Mfalme wetu sifa Mwimbieni..!
Mshangilieni, Mwimbieni Mungu sifa,simulieni matendo yake ya ajabu..!
Uniwezeshe kusema, ee Bwana,
Midomo yangu itangaze sifa zako..!Imbeni juu ya Utukufu wa jina lake,
Mtoleeni sifa tukufu..!
Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,wakiimba
daima sifa zako..!!


Baada ya ndugu zake kwenda kwenye sikukuu, Yesu naye alikwenda, lakini hakuenda kwa hadhara bali kwa siri. Viongozi wa Wayahudi walikuwa wanamtafuta kwenye sikukuu hiyo; wakauliza, “Yuko wapi?” Kulikuwa na minongono mingi katika umati wa watu. Baadhi yao walisema, “Ni mtu mwema.” Wengine walisema, “La! Anawapotosha watu.” Hata hivyo hakuna mtu aliyethubutu kusema habari zake hadharani kwa kuwaogopa viongozi wa Wayahudi. Sikukuu hiyo ilipofikia katikati, Yesu naye alikwenda hekaluni, akaanza kufundisha. Basi, Wayahudi wakashangaa na kusema, “Mtu huyu amepataje elimu naye hakusoma shuleni?” Hapo Yesu akawajibu, “Mafundisho ninayofundisha si yangu, bali ni yake yeye aliyenituma. Mtu anayependa kufanya yale anayotaka Mungu, atajua kama mafundisho yangu yametoka kwa Mungu, au mimi najisemea tu mwenyewe. Yeye anayejisemea tu mwenyewe anatafuta sifa yake mwenyewe; lakini anayetafuta sifa ya yule aliyemtuma, huyo ni mwaminifu, na ndani yake hamna uovu wowote. Je, Mose hakuwapeni sheria? Hata hivyo, hakuna hata mmoja wenu anayeishika sheria. Kwa nini mnataka kuniua?” Hapo watu wakamjibu, “Una pepo wewe! Nani anataka kukuua?” Yesu akawajibu, “Kuna jambo moja nililofanya, nanyi mnalistaajabia. Mose aliwapeni ile desturi ya kutahiri. (Si kwamba desturi hiyo ilitoka kwa Mose, bali ilitoka kwa mababu). Sasa nyinyi humtahiri mtu hata siku ya Sabato. Ikiwa basi, mtu hutahiriwa hata siku ya Sabato kusudi sheria isivunjwe, mbona mnanikasirikia kwa sababu nimemfanya mtu kuwa mzima kabisa siku ya Sabato? Msihukumu mambo kwa nje tu; toeni hukumu ya haki.”

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na fadhili zako kwetu..
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea
kuiona leo hii..


Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha,na kujiachilia mikononi mwako Jehovah..
Yahweh tunaomba utusamehe makosa yetu yote tuliyoyafanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea..
Baba wa Mbinguni tunaomba utuepushe katika majaribu Yahweh
utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..
Jehovah tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Baba wa Mbinguni
utufunike kwa damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nzareti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Baadhi ya watu wa Yerusalemu walisema, “Je, yule mtu wanayemtafuta wamuue si huyu? Tazameni sasa! Anawaonya hadharani, wala hakuna mtu anayemwambia hata neno. Je, yawezekana kuwa viongozi wametambua kweli kwamba huyu ndiye Kristo? Kristo atakapokuja hakuna mtu atakayejua mahali alikotoka, lakini sisi tunajua alikotoka mtu huyu!” Basi, Yesu alipokuwa anafundisha hekaluni alipaza sauti na kusema, “Ati mnanijua; hata nilikotoka mnakujua! Hata hivyo, sikuja kwa mamlaka yangu mwenyewe; ila yeye aliyenituma mimi ni wa kweli, nanyi hamumjui. Lakini mimi namjua kwa sababu nimetoka kwake, naye ndiye aliyenituma.” Basi, watu wakataka kumtia nguvuni, lakini hakuna mtu aliyethubutu kumkamata kwa sababu saa yake ilikuwa haijafika bado. Wengi katika ule umati wa watu walimwamini, wakasema, “Je, Kristo akija atafanya ishara kubwa zaidi kuliko alizozifanya huyu?”

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu..
Yahweh ukatupe neema ya ubunifu,maarifa katika vyote
tunavyoenda kufanya/kutenda na tukatende kama inavyokupendeza wewe
Jehova tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo Yahweh
nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Baba wa Mbinguni tunaomba tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Yahweh ukatupe sawasawa na mapenzi yako..

Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba/ndoa zetu 
ukatupe neema ya uvumilivu,kusameheana,
kuchukuliana,kuhurumiana,kusaidiana,kuelimishana kwa amani,
Upendo ukadumu na kila mmoja akajue jukumu lake na kazi yake..
Baba wa Mbinguni tunawaweka mikononi mwako watoto,wazazi wetu
familia/ndugu na wote wanaotuzunguka..
Mungu wetu tunaomba ulinzi wako kwetu sisi na vyote tunavyovimiliki
Baba wa Mbinguni ukatawale katika maisha yetu,ukatamalaki na kutuatamia,tuka nene yaliyo yako Mungu wetu ukaonekane katika maisha yetu..
Baba wa Mbinguni ukatupe neema ya kusimamia neno lako Amri na sheria zako siku zote za maisha yetu..
Yahweh ukatufanye chombo chema nasi tukatumike kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Mafarisayo waliwasikia watu wakinongona maneno hayo juu ya Yesu. Basi, wao pamoja na makuhani wakuu wakawatuma walinzi wamtie nguvuni. Yesu akasema, “Bado niko nanyi kwa muda mfupi, kisha nitamwendea yule aliyenituma. Mtanitafuta lakini hamtaniona, na pale nitakapokuwa nyinyi hamwezi kufika.” Viongozi wa Wayahudi wakasema wao kwa wao, “Mtu huyu atakwenda wapi ambapo hatutaweza kumpata? Atakwenda kwa Wayahudi waliotawanyika kati ya Wagiriki, na kuwafundisha Wagiriki? Ana maana gani anaposema: ‘Mtanitafuta lakini hamtanipata, na pale nitakapokuwa nyinyi hamwezi kufika?’” Siku ya mwisho ya sikukuu hiyo ilikuwa siku maalumu. Yesu alisimama, akasema kwa sauti kubwa, “Aliye na kiu na aje kwangu anywe. Kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: ‘Anayeniamini mimi, mito ya maji ya uhai itatiririka kutoka moyoni mwake!’” (Alisema hayo kumhusu Roho ambaye wale waliomwamini yeye watampokea. Wakati huo Roho alikuwa hajafika kwa sababu Yesu alikuwa hajatukuzwa bado).

Yahweh tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu wote
wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokata tamaa ukawape tunaini,wagonjwa ukawaponye,wenye njaa Baba ukawatendee
na kubariki kazi zao,mashamba na wakapate mahitaji ya kutosha na akiba...
walio katika vifungo mbalimbali vya yule mwovu Baba ukawafungue na kuwaweka huru,ukawape neema ya kuweza kujiombea,kufuata njia zako nazo ziwaweke huru..


Baadhi ya watu katika ule umati walisikia maneno hayo, wakasema, “Kweli mtu huyu ndiye yule nabii!” Wengine wakasema, “Huyu ndiye Kristo!” Lakini wengine walisema, “Je, yawezekana Kristo akatoka Galilaya? Maandiko Matakatifu yasemaje? Yanasema: ‘Kristo atatoka katika ukoo wa Daudi, na atazaliwa Bethlehemu, mji wa Daudi!’” Basi, kukatokea mafarakano juu yake katika ule umati wa watu. Baadhi ya watu walitaka kumtia nguvuni lakini hakuna aliyejaribu kumkamata. Kisha wale walinzi wakarudi kwa makuhani wakuu na Mafarisayo; nao wakawauliza, “Kwa nini hamkumleta?” Walinzi wakawajibu, “Hakuna mtu aliyepata kamwe kusema kama asemavyo mtu huyu!” Mafarisayo wakawauliza, “Je, nanyi pia mmedanganyika? Je, mmekwisha kumwona hata mmoja wa viongozi wa watu, au mmoja wa Mafarisayo aliyemwamini? Lakini umati huu haujui sheria ya Mose; umelaaniwa!” Mmoja wao alikuwa Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu. Basi, yeye akawaambia, “Je, sheria yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza na kujua anafanya nini?” Nao wakamjibu, “Je, wewe pia umetoka Galilaya? Haya, kayachunguze Maandiko Matakatifu nawe utaona kwamba Galilaya hakutoki kamwe nabii!” 
Sifa na utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!

Wapendwa katika Bwana asanteni kwakuwa nami
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea kama
inavyompendeza yeye..
Nawapenda..

Makabila mengine yanagawiwa nchi

1Baada ya kuishinda ile nchi, jumuiya yote ya Waisraeli ilikusanyika huko Shilo na kulisimika hema la mkutano. 2Yalikuwa yamebaki kati yao makabila saba ambayo hayakuwa yamegawiwa sehemu yao ya nchi. 3Kwa hiyo, Yoshua akawaambia Waisraeli, “Je, mtakawia mpaka lini kwenda kuimiliki nchi ile ambayo Mwenyezi-Mungu, Mungu wa babu zenu, amewapeni? 4Chagueni watu watatu kutoka kila kabila niwatume nchini kote wachunguze na kuchora ramani kulingana na makabila yao, kisha waniletee taarifa. 5Nao wataigawanya nchi hiyo sehemu saba. Kabila la Yuda litabaki na sehemu yake ya kusini na kabila la Yosefu kaskazini. 6Tayarisheni maelezo kamili juu ya sehemu zote saba na kuniletea. Hapo, nitapiga kura mbele ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu, kuhusu sehemu ya kila kabila lenu. 7Lakini Walawi hawatapata sehemu yoyote kati yenu, maana sehemu yao ni kuwa makuhani wa kumhudumia Mwenyezi-Mungu. Gadi, Reubeni na nusu ya kabila la Manase walikwisha pata sehemu yao upande wa mashariki wa mto Yordani. Walipewa sehemu hii na Mose, mtumishi wa Mwenyezi-Mungu.”
8Basi, watu hao wakaanza safari ya kwenda kuichunguza nchi. Kabla hawajaenda, Yoshua akawapa maagizo: “Nendeni nchini kote mkaandike maelezo kamili juu ya hiyo nchi, kisha mrudi mnieleze, nami nitapiga kura mbele ya Mwenyezi-Mungu hapa hapa Shilo kuhusu sehemu mtakayopewa.” 9Wanaume hao wakazunguka nchini kote, wakachora maelezo kamili juu ya sehemu zake saba pamoja na miji yake, kisha wakarudi kwa Yoshua kule kambini Shilo. 10Huko Shilo, Yoshua akazipigia kura sehemu hizo mbele ya Mwenyezi-Mungu, akawagawia Waisraeli; kila kabila na sehemu yake.

Nchi ya kabila la Benyamini

11Kura ya kwanza ililipata kabila la Benyamini kulingana na koo zake. Eneo walilopewa watu hao lilikuwa katikati ya lile la kabila la Yuda na lile la kabila la Yosefu. 12Mpaka wake wa kaskazini ulianzia mto Yordani na kupitia kaskazini mwa Yeriko na nchi ya milima ukaelekea magharibi hadi kwenye nyika ya Beth-aveni. 13Kutoka huko, mpaka wake ulikwenda kusini kuelekea Luzu kupitia upande wa kusini wa Luzu (yaani Betheli) hadi Ataroth-adari, kwenye mlima ulioko kusini mwa Beth-horoni ya Chini. 14Upande wa magharibi wa mlima huo ulio kusini mwa Beth-horoni mpaka uligeuka ukaelekea kusini hadi Kiriath-baali, uitwao pia Kiriath-yearimu, mji ambao ni mali ya kabila la Yuda. Huu ndio uliokuwa mpaka wake upande wa magharibi. 15Upande wa kusini mpaka wake ulianzia kwenye viunga vya mji wa Kiriath-yearimu, ukafika Efroni na kwenda hadi kwenye chemchemi ya maji ya Neftoa. 16Kisha ulielekea chini kupitia pembeni mwa mlima ulioko karibu na bonde la mwana wa Hinomu, ambalo lilikuwa katika sehemu ya kaskazini zaidi ya bonde la Warefai. Halafu mpaka uliteremka kuelekea bonde la Hinomu, kusini mwa kilima cha Wayebusi, ukaendelea kuteremka hadi En-rogeli. 17Huko, mpaka uligeuka kwenda kaskazini kuelekea En-shemeshi, ukapitia Gelilothi unaokabili mwinuko wa Adumimu na kuteremka hadi kwenye jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 18Kutoka hapo, mpaka ulizunguka kaskazini kwenye ukingo wa juu wa Araba na kuishia huko Araba. 19Tena, ukaendelea kwa upande wa kaskazini wa kilima cha Beth-hogla na kuishia kaskazini kabisa ya ghuba ya Bahari ya Chumvi, mahali unapoingilia mto Yordani. Huu ni mpaka wake kwa upande wa kusini. 20Mto Yordani ndio uliokuwa mpaka wake upande wa mashariki. Ndivyo zilivyowekewa mipaka nchi zilizopewa koo za kabila la Benyamini.
21Miji ya koo za kabila la Benyamini ni Yeriko, Beth-hogla, Emek-kesisi, 22Beth-araba, Zemaraimu, Betheli, 23Avimu, Para, Ofra, 24Kefar-amoni, Ofni na Geba. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na miwili pamoja na vijiji vyake. 25Miji mingine ni Gibeoni, Rama, Beerothi, 26Mizpa, Kefira, Moza, 27Rekemu, Irpeeli, Tarala, 28Zela, Ha-elefu, Yebusi, yaani Yerusalemu, Gibea na Kiriath-yearimu. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na minne pamoja na vijiji vyake. Hiyo yote ni sehemu waliyopewa watu wa kabila la Benyamini na koo zao.

Yoshua 18;1-28

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 1 November 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 17...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?
Ni siku/mwezi Mwingine tena Mungu wetu ametuchagua na kutupa
kibali cha kuendelea kuiona leo hii...
Tumempa nini Mungu?Tumetenda wema gani?Tumekuwa wazuri sana?
Tumekuwa wenye nguvu/utashi ndiyo maana ametutendea haya?
Tumetenda yote yanayompendeza Mungu?Tumekuwa kiroho?
Hapana si kwamba sisi si wakosaji au wema sana zaidi ya wengine
ambao leo hii hawakuweza kuiona siku hii,na wengine wapo hoi
vitandani hawawezi hata kujigeuza,wengine hawana kauli ya hata kumuita
Mungu na kutubu,Mimi na wewe ni nani na jee tumechukuliaje Neema/rehema hii? kwa maana ni kwa mapenzi yake sisi kuwa hivi
tulivyo leo,Kwake yeye yote yanawezekana,tuwe tayari hatujui
muda wala siku Mwana wa Mungu yuaja...

“Muwe tayari mmejifunga mkanda kiunoni, na taa zenu ziwe zinawaka; muwe kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka harusini, ili wamfungulie mara atakapobisha. Heri yao watumishi wale ambao bwana wao atakaporudi atawakuta wanakesha! Nawaambieni hakika, huyo bwana atajifunga mkanda kiunoni, atawaketisha mezani na kuwahudumia. Hata kama atarudi usiku wa manane au alfajiri na kuwakuta wanakesha, heri yao watumishi hao! Jueni kwamba, kama mwenye nyumba angejua saa ambayo mwizi atakuja, angekesha, wala hangeiacha nyumba yake ivunjwe. Nanyi, kadhalika muwe tayari, maana Mwana wa Mtu atakuja saa msiyoitazamia.”


Asante Baba wa Mbinguni kwa  wema na fadhili zako kwetu
Asante kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Utukuzwe ee Mungu wetu,Usifiwe ee Baba wa Mbinguni,Unastahili
kuabudiwa Jehovah,Unastahili kuheshimiwa Yahweh,Unastahili
kuhimidiwa Mungu wetu,Unatosha Baba wa Mbinguni,Matendo yako
ni makuu mno,Matendo yako ni ya ajabu...!!

Haleluya! Msifuni Mwenyezi-Mungu! Mshukuruni Mwenyezi-Mungu kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake zadumu milele! Ni nani awezaye kutaja matendo ya Mwenyezi-Mungu? Ni nani awezaye kumsifu kama anavyostahili? Heri wale wanaotekeleza haki, wanaotenda daima mambo yaliyo sawa. Unikumbuke ee Mwenyezi-Mungu unapowafadhili watu wako; unisaidie wakati unapowaokoa; ili niweze kuona fanaka ya wateule wako, nipate kufurahia furaha ya taifa lako, na kuona fahari pamoja na watu wako.

Tazama jana imepita Mungu wetu leo ni siku mpya na kesho ni
siku nyingine Baba wa Mbinguni tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza,
tukijishusha,tujiachilia mikononi mwako Jehovah..
Tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizo zifanya kwakuwaza,
kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua...
Baba wa Mbinguni tunaomba nasi utupe neema ya kuweza
kuwasamehe wale wote waliotukosea..
Mungu wetu tunaomba utuepushe  katika majaribu Baba na utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote...
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Jehovah
tunaomba
  utufunike kwa damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..

Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaotumikia bado katika hema la Wayahudi hawana haki ya kula vitu vyake. Kuhani mkuu wa Kiyahudi huleta damu ya wanyama katika Mahali Patakatifu na kuitoa tambiko kwa ajili ya dhambi; lakini nyama za hao wanyama huteketezwa nje ya kambi. Ndiyo maana Yesu pia, kusudi apate kuwatakasa watu kwa damu yake mwenyewe, aliteswa na kufa nje ya mji. Basi, tumwendee huko nje ya kambi tukajitwike laana yake. Maana hapa duniani hatuna mji wa kudumu; lakini tunautafuta ule unaokuja. Basi, kwa njia ya Yesu, tumtolee Mungu tambiko ya sifa daima, yaani sifa zinazotolewa kwa midomo inayoliungama jina lake.

Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu,Biashara,
mashamba,masomo na yote tunayoenda kufanya/kutenda
Mungu wetu tukatende sawasawa na mapenzi yako..
Yahweh tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Jehova nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki
wenye kuhitaji..

Jishughulishe na biashara hata kama kwa kubahatisha; yawezekana baadaye ukapata chochote kile. Wagawie watu saba hata wanane sehemu yako, maana, hujui balaa litakalofika duniani. Mawingu yakijaa maji, mvua hunyesha; mti ukiangukia kusini au kaskazini, hapo uangukiapo ndipo ulalapo. Anayengoja upepo hatapanda mbegu, anayesubiri mawingu yatoweke, hatavuna kitu. Usivyojua jinsi uhai unavyoingia katika mifupa ya mtoto tumboni mwa mamake, kadhalika huwezi kuelewa matendo ya Mungu, ambayo hufanya kila kitu. Panda mbegu asubuhi na jioni usiache kupanda, maana, hujui zipi zitaota; za asubuhi, za jioni, au zote zitakuwa nzuri. Mwanga wafaa, na kuliona jua kwapendeza macho. Mtu akiishi miaka mingi, na aifurahie miaka hiyo yote; lakini akumbuke kuwa siku za giza zitakuwa nyingi, na kwamba yote yatakayofuata ni bure.


Baba wa Mbinguni tusipungukiwe katika mahitaji yetu
Yahweh ukatupe kama inavyo kupendeza wewe..
Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na
wote wanaotuzunguka,Baba wa Mbinguni tunaomba ulinzi
wako kwetu na vyote tunavyovimiliki,Yahweh ukatamalaki na kutuatamia
Jehovah ukatupe neema ya kusimamia Neno lako,amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu,Baba wa mbinguni tukawe na shauku/kiu
ya kusoma Neno lako,kufuata njia zako na ukatupe neema
ya kukumbushana/kuelimishana kwa upendo,amani katika mioyo yetu,
tuka nene yaliyo yako,tukapate kutambua/kujitambua..

Kisha, nilitoa maagizo kuwa sote tufike karibu na mto Ahava ili tufunge na kujinyenyekeza mbele za Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu. Ingekuwa aibu kubwa kwangu kumwomba mfalme kikosi cha askari na wapandafarasi wa kutulinda na adui njiani maana nilikuwa nimekwisha mwambia kuwa Mungu wetu huwabariki wote wanaomtafuta, lakini huwachukia na kuwaadhibu wote wanaomwacha. Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu atulinde, naye aliyasikia maombi yetu.

Ee Baba tunaomba upokee sala/maombi yetu..
Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse kwa mkono wako
wenye nguvu na uponyaji,Yahweh tunaomba ukawaponye wagonjwa,
Baba wa Mbinguni ukawatendee na kuwapa maarifa wenye njaa
Jehovah tunaomba ukawafungue walio katika vifungo mbalimbali
vya yule mwovu,Yahweh ukwape tunaini wale wote walikata tamaa..
Baba wa Mbinguni ukawaponye kiro/mwili na ukasikie kulia kwao
Yahweh ukawafute machozi ya watoto wako ukapokee sala/maombi
yao na ukawape neema ya kujiombea,wakasimamie njia zako
Nuru ikaangaze katika maisha yao..
Kwa imani tunayaweka haya yote mikononi mwako Jehovah..
Sifa na utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na utukufu hata Milele..
Amina..!!

Asanteni sana wapendwa katika Bwana kwa kuwa nami
Amani ikatawale katika maisha yenu,Baraka na upendo,
Na Mungu aendelee kuwatendea katika yote yampendezayo yeye
Nawapenda..

1Watu wa kabila la Manase ambaye alikuwa mzaliwa wa kwanza wa Yosefu, pia walipewa eneo lao kwa kura. Makiri, mzaliwa wa kwanza wa Manase na baba yake Gileadi, alikwishapewa kwa kura miji ya Gileadi na Bashani, maana alikuwa hodari vitani. 2Wengine waliobaki wa kabila la Manase walipewa sehemu yao kwa kura kulingana na koo zao. Koo hizo zilikuwa zile za Abiezeri, Heleki, Asrieli, Shekemu, Heferi na Shemida ambao wote walikuwa wazawa wa kiume wa Manase mwana wa Yosefu.
3Lakini Selofehadi mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, hakuwa na watoto wa kiume, bali alikuwa na watoto wa kike tu, nao walikuwa: Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirza. 4Taz Hes 27:1-7 Mabinti hao wakamjia kuhani Eleazari na Yoshua, mwana wa Nuni, na viongozi wengine wakawaambia, “Mwenyezi-Mungu alimwamuru Mose atugawie na sisi sote nchi kama wagawiwavyo wanaume wa kabila letu.” Basi kufuatana na amri ya Mwenyezi-Mungu, Yoshua akawapatia sehemu yao kama alivyowapa wanaume wa kabila lao. 5Kwa hiyo kabila la Manase liliongezewa sehemu mbili zaidi yaani nchi ya Gileadi na Bashani iliyoko upande mwingine wa mto Yordani, 6kwa sababu binti za Manase waligawiwa sehemu zao kama walivyogawiwa wanaume wa kabila lao. (Nchi ya Gileadi walipewa wazawa wengine wa Manase).
7Eneo la kabila la Manase lilianzia Asheri na kwenda hadi Mikmethathi mashariki ya Shekemu; halafu mpaka wao ukaendelea kusini hadi kwenye nchi ya wakazi wa En-tapua. 8Nchi ya Tapua ilikuwa mali yake Manase, lakini mji wa Tapua, ambao ulikuwa mpakani, ulikuwa mali ya wazawa wa Efraimu. 9Mpaka huo uliendelea hadi kijito cha Kana. Miji iliyokuwa kusini ya Kana ilikuwa ya Waefraimu hata ingawa ilikuwa katika nchi ya kabila la Manase. Halafu mpaka ukapita kaskazini ya kijito Kana na kuishia bahari ya Mediteranea. 10Eneo la kusini lilikuwa la kabila la Efraimu na eneo la kaskazini lilikuwa la kabila la Manase, mpaka wake ukiwa bahari ya Mediteranea kwa upande wa magharibi. Kabila la Asheri lilikuwa kaskazini-magharibi ya eneo la Manase na kaskazini-mashariki lilikuwa kabila la Isakari. 11Vilevile katika nchi ya kabila la Isakari na kabila la Asheri, kabila la Manase lilipatiwa miji ya Beth-sheani na Ibleamu pamoja na vijiji vyake, na miji ya Dori, En-dori, Taanaki na Megido pamoja na wakazi na vijiji vyake; na pia theluthi ya Nafathi.17:11 makala ya Kiebrania si dhahiri. 12Taz Amu 1:27-28 Lakini wazawa wa Manase hawakuweza kuwafukuza wakazi wa miji hiyo, Wakanaani wakaendelea kuishi humo, 13ingawa hata baada ya Waisraeli kuwa na nguvu zaidi, hawakuweza kuwafukuza ila tu waliwafanyisha kazi za kulazimishwa.
14Watu wa kabila la Yosefu walimwendea Yoshua, wakamwambia, “Kwa nini umetugawia sehemu moja tu ya nchi sisi ambao Mwenyezi-Mungu ametubariki hata akatufanya tuwe wengi sana?” 15Yoshua akawajibu, “Kama mmekuwa wengi hivyo, hata nchi ya milima ya Efraimu haiwatoshi tena, basi nendeni msituni katika nchi ya Waperizi na ya Warefai, mkaufyeke msitu huo na kufanya makao yenu huko.” 16Nao wakamjibu, “Ni kweli kwamba nchi hii ya milima haitutoshi; hata hivyo wale Wakanaani wote wanaokaa kwenye tambarare wana magari ya chuma, vilevile wale wote wanaokaa Beth-sheani pamoja na vijiji vyake, na wale wanaoishi katika Bonde la Yezreeli.”
17Basi, Yoshua akawaambia wazawa wa Yosefu, yaani kabila la Efraimu na Manase, “Kweli nyinyi mmekuwa wengi na wenye uwezo mkubwa. Haifai mpate sehemu moja tu, 18bali pia nchi ya milima itakuwa yenu. Ingawa sasa ni msitu, mtaifyeka na kuimiliki yote toka upande huu hadi upande mwingine. Mtawaondoa Wakanaani, hata kama wana magari ya chuma na ni wenye nguvu.”


Yoshua 17;1-17

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 31 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 16...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Tusalimiane na kukumbushana wema wa Mungu na fadhili zake..

Jee unamkumbuka Ndugu yako katika Kristo katika lipi?
kwa wema wake?kujitoa katika kazi ya Mungu /kanisa?
kujitoa kwa wapendwa wengine ndani na nje ya kanisa?
Hekima,Busara,uvumilivu,upatanishi,uongozi bora,Upendo,ucheshi,
unyenyekevu,amani,ukweli,uimbaji wake? na vingine vingi unaweza kusema ambavyo mimi sikuviweka...

Jee asipokuwepo kunakuwa na pengo,upweke,kupwaya na kuhisi
kunaupungufu kidogo?

Au unamkumbuka Ndugu yako katika Kristo kwa baya lipi?
Makwazo,ugombanishi,uongo,uzushi,ukorofi,kisirani,unafiki?na vingine
vingi unavyoona vibaya ambavyo mimi sikuviweka wewe unaviju..

Jee umechukua hatua gani? Umemsifia kwa mema/mazuri
 anayoyafanya na kumuombea aendelee kusimamia hayo na
Mungu aendelee kumuongoza katika yote yampendezayo?

Jee kwa mabaya pia umechukua hatua gani?
Au unaendeleza nawe ubaya na kusengenya pembeni?
Umejaribu kumshauri hiyo njia siyo?na kumuonya/kumuelisha
kwa upendo,hekima na busara?

Jee unampenda?au unamdanganya na unajidanganya mwenyewe
kwa sababu upendo wa kweli ni kumwambia ukweli naye anaweza
kujirudi hata kama kwa wakati ule alihamaki lakini atajifikiria
na kuchukua hatua....

Ebu tujaribu leo kwa watu 2 wa karibu yako iwe kwa mazuri yao
au mabaya yao,unaweza kufikiri kwamba alikuwa anatenda
vibaya kwa jambo unaloliona wewe lakini kumbe anasababu na anaweza
kukupa sababu ya kufanya hivyo..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote tunayoenda kufanya/kutenda,
kunena na tukanene yaliyo yake..
Mungu ni pendo apenda watu...
Nakupenda..
Tuendelee...

Napenda kumjulisha kwenu dada yetu Foibe ambaye ni mtumishi katika kanisa la Kenkrea. Mpokeeni kwa ajili ya Bwana kama iwapasavyo watu wa Mungu. Mpeni msaada wowote atakaohitaji kutoka kwenu, maana yeye amekuwa mwema sana kwa watu wengi na kwangu pia. Salamu zangu ziwafikie Priska na Akula, wafanyakazi wenzangu katika utumishi wa Kristo Yesu. Wao walihatarisha maisha yao kwa ajili yangu. Wanastahili shukrani; si tu kutoka kwangu, bali pia kutoka kwa makanisa yote ya watu wa mataifa mengine. Salamu zangu pia kwa kanisa linalokutana nyumbani kwao. Salamu zangu zimfikie rafiki yangu Epaineto ambaye ni wa kwanza katika mkoa wa Asia kumwamini Kristo. Nisalimieni Maria ambaye amefanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu. Salamu zangu kwa Androniko na Yunia, wananchi wenzangu waliofungwa gerezani pamoja nami; wao wanajulikana sana kati ya mitume; tena walikuwa Wakristo kabla yangu mimi. Salamu zangu kwa Ampliato, rafiki yangu katika kuungana na Bwana. Salamu zangu zimfikie Urbano, mfanyakazi mwenzangu katika utumishi wa Kristo; salamu zangu pia kwa rafiki yangu Staku. Nisalimieni Apele ambaye uaminifu wake kwa Kristo umethibitishwa. Salamu zangu kwa wote walio nyumbani mwa Aristobulo. Salamu zangu kwa Herodiana, mwananchi mwenzangu; na kwa jamaa yote ya Narkisi iliyojiunga na Bwana. Nisalimieni Trufena na Trufosa wanaofanya kazi katika utumishi wa Bwana, na rafiki yangu Persi ambaye amefanya mengi kwa ajili ya Bwana. Nisalimieni Rufo, mtu hodari sana katika kazi ya Bwana, na mama yake ambaye ni mama yangu pia. Nisalimieni Asunkrito, Flegoni, Herme, Patroba, Herma na ndugu wote walio pamoja nao. Nisalimieni Filologo na Yulia, Nerea na dada yake, na Olimpa, pamoja na watu wote wa Mungu walio pamoja nao. Salimianeni nyinyi kwa nyinyi kwa ishara ya upendo. Salamu kwenu kutoka kwa makanisa yote ya Kristo.
Tumshukuru Mungu wetu kwa wema na fadhili zake kwetu..
Asante Baba wa Mbinguni kwa ulinzi wako wakati wote..
Asante kwakutuchagua tena na kutupa kibali cha kuendelea
kuina leo hii..Si kwamba sisi tumetenda mema sana,wala si kwa
nguvu/utashi wetu sisi kuwa hivi tulivyo ni kwa neema/rehema
zako Mungu wetu ni kwa mapenzi yako...

Ukuu ni wako, ee Mwenyezi-Mungu, una nguvu, utukufu, ushindi na enzi. Vyote vilivyoko mbinguni na duniani ni vyako. Ee Mwenyezi-Mungu, ufalme ni wako, nawe umetukuzwa, u mkuu juu ya vitu vyote. Utajiri na heshima hutoka kwako, vyote wavitawala. Uwezo na nguvu vimo mkononi mwako, nawe wawakuza uwapendao, na huwaimarisha wote. Sasa ee Mungu wetu, tunakushukuru na kulisifu jina lako tukufu.

Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza,tukijishusha
na kujiachlia mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Yahweh tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Mungu wetu nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe
wale wote waliotukosea..
Jehovah tunaomba utuepushe katika majaribu Baba utuokoe
na yule mwovu na kazi zake zote..
Yahweh tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu
Jehovah 
utufunikekwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Ndugu zangu, nawasihi mwafichue wote wanaosababisha mafarakano na kuwafanya watu wengine waanguke, kinyume cha mafundisho mliyofundishwa. Jiepusheni na watu hao, maana watu wa namna hiyo hawamtumikii Kristo Bwana wetu, bali wanayatumikia matumbo yao wenyewe. Kwa maneno yao matamu na hotuba za kubembeleza hupotosha mioyo ya watu wanyofu. Kila mtu amesikia juu ya utii wenu katika mambo mema, na bila hatia kuhusu mambo mabaya. Naye Mungu aliye chanzo cha amani hatakawia kumponda Shetani chini ya miguu yenu. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi. Timotheo, mfanyakazi mwenzangu, anawasalimu. Hali kadhalika Lukio, Yasoni, na Sosipateri, wananchi wenzangu, wanawasalimu. Nami Tertio, ninayeandika barua hii, nawasalimuni kwa jina la Bwana. Gayo, mwenyeji wangu, pamoja na kanisa lote linalokutana kwake, anawasalimu. Erasto, mweka hazina wa mji huu, pamoja na Kwarto, wanawasalimu. [ Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi nyote. Amina.]
Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu
vyote tunavyoenda kufanya/kutenda Yahweh tukatende
kama inavyo kupendeza wewe..
Jehovah tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo
Baba wa Mbinguni nasi tunaomba utupe neema ya kuweza
kuwabariki wenye kuhitaji..
Yahweh tusipungukiwe katika mahitaji yetu Mungu wetu ukatupe
sawasawa na mapenzi yako..

Mfalme wa Amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba/ndoa zetu,watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na
wote wanaotuzunguka Yahweh tunaomba ulinzi wako,
Baba tunaomba ukatamalaki na kutuatamia,ukatubariki,
Baba wa Mbinguni tukawe na kiu/shauku ya kujua/kufuata njia zako,
 kusoma Neno lako na likawe taa na Nuru kwenye maisha yetu
Ukatupe neema ya kusimamia Neno lako amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu..
Tukawe barua njema na tukasomeke kama inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote tukawe na kiasi...
Ee Baba ukasikie kuomba kwetu na ukapokee maombi/sala zetu..

Basi, sasa na tumsifu Mungu! Yeye anaweza kuwaimarisheni katika ile Habari Njema niliyohubiri juu ya Yesu Kristo, na katika ile siri iliyofunuliwa na ambayo ilikuwa imefichika kwa karne nyinyi zilizopita. Lakini, sasa ukweli huo umefunuliwa kwa njia ya maandiko ya manabii; na kwa amri ya Mungu wa milele umedhihirishwa kwa mataifa yote ili wote waweze kuamini na kutii. Kwake Mungu aliye peke yake mwenye hekima, uwe utukufu kwa njia ya Yesu Kristo, milele na milele! Amina.

Tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wenye njaa,walio
katika vifungo mbalimbali,wanaopitia magumu/majaribu,
waliokata tamaa Baba wa Mbinguni ukawape tumaini
Yahweh ukawape neema ya kujiombea,kusimamia njia zako
ukawaguse na mkono wako wenye nguvu Yahweh wakapate
kupona kimwili na kiroho pia,ukawape ubunifu katika kazi,kilimo,
biashara na ukawatendee sawasawa na mapenzi yako..
Sifa na utukufu tunakurudishia Mungu wetu..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!

Wapendwa katika Bwana asanteni kwakuwa pamoja nami
Mungu wa Upendo akadumu katika maisha yenu...
aendelee kuwabariki nanyi mkawe baraka kwa wengine..
Nawapenda.

Nchi ya Efraimu na ya Manase

1Sehemu waliyogawiwa wazawa wa Yosefu kwa kura ilianzia karibu na mto Yordani, mashariki ya chemchemi ya Yeriko, na kupitia jangwani, hadi kwenye sehemu za milima mpaka Betheli. 2Kutoka Betheli mpaka ulielekea Luzu ukapita Atarothi ambako waliishi Waarki. 3Kisha ukashuka magharibi katika nchi ya Wayafleti hadi Beth-horoni ya Chini na Gezeri na kuishia kwenye bahari ya Mediteranea. 4Wazawa wa Yosefu, yaani kabila la Manase na kabila la Efraimu, walipewa nchi hiyo kuwa milki yao.

Nchi ya kabila la Efraimu

5Watu wa kabila la Efraimu kulingana na jamaa zao walipata sehemu yao ambayo mpaka wake upande wa mashariki ulipita Ataroth-adari hadi Beth-horoni ya Juu, 6na kuishia bahari ya Mediteranea. Kwa upande wa kaskazini mpaka ulipita Mikmethathi na kwa mashariki yake ulizunguka na kuelekea Taanath-shilo ambako ulipita upande wa mashariki hadi Yanoa. 7Kutoka Yanoa ulikwenda hadi Atarothi na Naara, hata kufika Yeriko, ambako uliishia katika mto Yordani. 8Kutoka Tapua, mpaka ulikwenda magharibi hadi kijito cha Kana na kuishia bahari ya Mediteranea. Hii ndiyo nchi waliyopewa watu wa kabila la Efraimu kulingana na jamaa zao, 9pamoja na miji na vijiji ambavyo waliongezewa kutoka kwenye nchi ya kabila la Manase. 10Taz Amu 1:29 Waefraimu hawakuwafukuza Wakanaani walioishi Gezeri. Wakanaani hao waliendelea kukaa miongoni mwa watu wa Efraimu mpaka leo, wakiwa watumwa wa kuwafanyia kazi za kulazimishwa.


Yoshua 16;1-10

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 30 October 2017

Kikombe Cha Asubuhi ;Yoshua 15...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje?

Ni wiki/siku nyingine tena Mungu wetu ametuchagua na
ametupa kibali chakuendelea kuona leo hii..
Tumshukuru Mungu wetu kwa wema na fadhili zake kwetu..

Asante Mungu wetu kwa ulinzi wako kwetu wakati wote..
Asante kwa pumzi/uzima,afya na kutuamsha salama na tukiwa
tayari kwa majukumu yetu..

Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu,Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu juu
ya Mbinguni,Utukufu  wako uenee duniani kote..
Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu utufundishe masharti yako..
Utukuzwe ee Mwenyezi-Mungu kwasababu ya nguvu yako!
Tutaimba na kuusifu uwezo wako..
Sio sisi, ee Mwenyezi-Mungu ,Sio sisi, bali wewe peke yako Utukuzwe,
Kwa ajili ya fadhili zako na uaminifu wako..
Utukuzwe milele na milele ee Mwenyezi-Mungu Mungu wa Abrahamu,
Isaka na Yakobo,Baba yetu,Muumba wetu,Unatosha Baba wa Mbinguni..


Mshukuruni Mwenyezi-Mungu, tangazeni ukuu wake; yajulisheni mataifa mambo aliyotenda! Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa; simulieni matendo yake ya ajabu! Jisifieni jina lake takatifu; wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi. Tafuteni msaada kwa Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu; mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima. Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda, miujiza yake na hukumu alizotoa, enyi wazawa wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake; Yeye ndiye Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu; hukumu zake zina nguvu duniani kote. Yeye hulishika agano lake milele, hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu. Hushika agano alilofanya na Abrahamu, na ahadi aliyomwapia Isaka. Alimthibitishia Yakobo ahadi yake, alimhakikishia Israeli agano hilo la milele. Alisema: “Nitawapeni nchi ya Kanaani, nayo itakuwa mali yenu wenyewe.”
Sifa na utukufu tunakurudishia wewe ee Mungu wetu..

Tazama jana imepita Mungu wetu Leo ni siku mpya Jehovah na
 kesho ni siku nyingine Yahweh..!
Tunakuja mbele zako tukijinyeyekeza,tukijishusha na kujiachilia
mikononi mwako Baba wa Mbinguni..
Yahweh tunaomba utusamehe dhambi zetu zote tulizozifanya
kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Jehovah nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwasamehe wote
waliotukosea..
Baba wa Mbimnguni tunaomba utuepushe katika majaribu Yahweh
utuokoe na yule mwovu na kazi zake zote..

Kisha Yesu akaenda pamoja nao bustanini Gethsemane, akawaambia wanafunzi wake, “Kaeni hapa nami niende pale mbele kusali.” Akawachukua Petro na wana wawili wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko. Hapo akawaambia, “Nina huzuni kubwa moyoni hata karibu kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami.” Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi, akasali: “Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki kinipite; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe.” Akawaendea wale wanafunzi, akawakuta wamelala. Akamwambia Petro, “Ndio kusema hamkuweza kukesha pamoja nami hata saa moja? Kesheni na kusali ili msije mkaingia katika majaribu. Roho inataka lakini mwili ni dhaifu.” Akaenda tena mara ya pili akasali: “Baba yangu, kama haiwezekani kikombe hiki kipite bila mimi kukinywa, basi, utakalo lifanyike.” Akawaendea tena, akawakuta wamelala, maana macho yao yalikuwa yamebanwa na usingizi. Basi, akawaacha, akaenda tena kusali mara ya tatu kwa maneno yaleyale. Kisha akawaendea wale wanafunzi, akawaambia, “Je, mngali mmelala na kupumzika? Tazameni! Saa yenyewe imefika, na Mwana wa Mtu atatolewa kwa watu wenye dhambi. Amkeni; twendeni zetu. Tazameni! Anakuja yule atakayenisaliti.”

Mungu wetu tunaomba ututakase miili yetu na akili zetu Jehovah
tunaomba utufunike kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na
 Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Yeye aliteseka kwanza ili sisi tupate kupona..


Mungu wetu tunaomba ukabariki kazi za mikono yetu na vyote
tunavyoenda kufanya kutenda Mungu wetu tukatende kama inavyokupendeza wewe..
BABA tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo/zitokazo Yahweh
nasi tunaomba utupe neema ya kuweza kuwabariki wenye kuhitaji..
Jehovah tunaomba tusipungukiwe katika mahitaji yetu,Yahweh
ukatupe sawasawa na mapenzi yako..


Mungu wetu tuyaweka maisha yetu mikononi mwako..
Mfalme wa amani tunaomba amani yako ikatawale katika
nyumba/ndoa zetu, watoto,wazazi wetu,familia/ndugu na wote
wanaotuzunguka...
Mungu wetu ukatamalaki na kutuatamia,Baba tunamba ulinzi wako
Yahweh tunaomba utupe neema ya hekima,busara,utu wema na fadhili..
Jehovah utupe neema ya kusimamia Neno lako Amri na sheria zako
siku zote za maisha yetu..
Ukatufanye chombo chema Mungu wetu nasi tukatumike kama
inavyokupendeza wewe..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..

Ee Bwana, tangu vizazi vyote, wewe umekuwa usalama wetu. Kabla ya kuwapo milima, kabla hujauumba ulimwengu; wewe ndiwe Mungu, milele na milele. Wamwambia binadamu, “Rudi mavumbini!” Naye binadamu hurudi mavumbini alimotoka! Kwako miaka elfu ni kama siku moja tu, ni kama jana ambayo imekwisha pita; kwako ni kama mkesha mmoja wa usiku! Wawafutilia mbali watu kama ndoto! Binadamu ni kama nyasi zinazochipua asubuhi: Asubuhi huchipua na kuchanua, jioni zimekwisha nyauka na kukauka. Hasira yako inatuangamiza; tunatishwa na ghadhabu yako. Maovu yetu umeyaweka mbele yako; dhambi zetu za siri ziko wazi mbele yako. Kwa hasira yako maisha yetu yatoweka, yanaisha kama pumzi. Miaka ya kuishi ni sabini, au tukiwa wenye afya, themanini; lakini yote ni shida na taabu! Siku zapita mbio, nasi twatoweka mara! Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayejali matokeo ya ghadhabu yako? Utufundishe ufupi wa maisha yetu ili tuweze kuwa na hekima. Urudi, ee Mwenyezi-Mungu! Utakasirika hata lini? Utuonee huruma sisi watumishi wako. Utushibishe fadhili zako asubuhi, tushangilie na kufurahi maisha yetu yote. Utujalie sasa miaka mingi ya furaha, kama ulivyotupa miaka mingi ya shida na taabu. Utuoneshe matendo yako sisi watumishi wako; uwaoneshe wazawa wetu uwezo wako mtukufu. Utufadhili ee Bwana, Mungu wetu; uzitegemeze kazi zetu, uzifanikishe shughuli zetu.
Baba tunaomba ukawaguse kwa mkono wako wenye nguvu
na ukawape uponyaji wa mwili na roho wote wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,wagonjwa,walio katika
vifungo vya yule mwovu Yahweh tunaomba ukawafungue na wakawe
huru,Baba tazama wenye njaa tunaomba ukawatendee katika
mapito yao,ukabariki mashamba yao,kazi zao,biashara na ukawape
ubunifu katika utendaji wao..Baba ukawape neema ya kujiombea
na kufuata njia zako,Nuru yako ikaangaze katika maisha yao..
Baba ukapokee sala/maombi ya watoto wako wote wanaokuomba
na kukutafuta kwa bidii,Imani/kuamini Mungu wetu mwenye huruma
tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Kwakuwa Ufalme ni wako Nguvu na Utukufu hata Milele..
Amina..!!

Wapendwa/waungwana asanteni sana kwakuwa nami
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea sawasawa
na mapenzi yake..
sina neno zuri la kusema zaidi yakusema..
Nawapenda.

Eneo walilopewa watu wa Yuda

1Eneo la nchi waliyopewa kwa kura watu wa kabila la Yuda kulingana na jamaa zake lilienea tangu kusini-mashariki hadi mpakani mwa Edomu. Sehemu ya kusini kabisa ilikuwa jangwa la Sini. 2Mpaka wao upande wa kusini ulianza pembe ya kusini ya Bahari ya Chumvi, 3ukaendelea kusini hadi mwinuko wa Akrabimu, ukapitia kando ya Sini, na kusini ya Kadesh-barnea, ukipitia Hesroni hadi Adari na kisha ukageuka kuelekea Karka. 4Kutoka hapo ulipita karibu na Asmoni na kufuata kijito cha Misri hadi kufikia kwenye bahari ya Mediteranea. Hapo ndipo ulipopita mpaka wa kusini wa Yuda. 5Mpaka wao wa upande wa mashariki ni Bahari ya Chumvi hadi pale mto Yordani unapoingilia baharini. Na mpaka wao upande wa kaskazini ulipita kutoka pembe ya Bahari ya Chumvi mahali ambapo mto Yordani unaingilia baharini. 6Mpaka huo ukapita Bethi-hogla na kaskazini ya Beth-araba hadi kwenye jiwe la Bohani mwana wa Reubeni. 7Kutoka hapo, uliendelea hadi Debiri kwenye bonde la Akori na kaskazini kuelekea Gilgali, ulio karibu na mwinuko wa Adumimu ambao uko kusini mwa kijito, kisha ukaelekea kwenye chemchemi za En-shemeshi na kuishia En-rogeli. 8Kisha, mpaka huo ulipitia kwenye Bonde la Hinomu, upande wa kusini mwa kilima cha Wayebusi, yaani Yerusalemu, kuelekea kilele cha mlima ulio magharibi ya bonde la Hinomu na kufika mwishoni mwa bonde la Refaimu. 9Kutoka hapo, ulielekea mlimani hadi chemchemi za Neftoa, mpaka kwenye miji ya mlima wa Efroni. Hapo mpaka uligeuka na kuelekea Baala, yaani Kiriath-yearimu, 10ambako ulipinda magharibi kuelekea Mlima Seiri; ukapita kaskazini ya mlima wa Yerimu, yaani Kesaloni, na kuteremka hadi Beth-shemeshi ambapo ulipita karibu na Timna. 11Kisha ukaendelea upande wa kaskazini wa Ekroni, ukazunguka kuelekea Shikroni ambapo ulipita karibu na mlima Baala hadi Yabneeli ukaishia katika bahari ya Mediteranea. 12Mpaka wa magharibi ulikuwa bahari ya Mediteranea. Ndivyo ilivyokuwa mipaka ya eneo walilopewa watu wa kabila la Yuda kulingana na koo zao.

Watu wa Kalebu wanamiliki eneo la Hebroni

13 Taz Amu 1:20 Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya nchi ya Yuda kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriath-arba au mji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Mji huo sasa unaitwa Hebroni. 14Kalebu alizifukuza kutoka mji huo koo tatu za Anaki yaani ukoo wa Sheshai, ukoo wa Ahimani na ukoo wa Talmai. 15Kutoka Hebroni alikwenda kuwashambulia wakazi wa Debiri, mji ambao hapo awali uliitwa Kiriath-seferi. 16Kalebu akatangaza kwamba atamwoza binti yake Aksa kwa mwanamume yeyote atakayeuteka mji wa Kiriath-seferi. 17Basi, Othnieli, mwana wa Kenazi, nduguye Kalebu, akauteka mji huo, naye Kalebu akamwoza bintiye. 18Katika siku yao ya harusi, Aksa alimwambia Othnieli amwombe Kalebu shamba. Aksa alikuwa amepanda punda, na alipokuwa anashuka chini, Kalebu akamwuliza, “Unataka nikupe nini?” 19Aksa akamjibu, “Nipe zawadi; nipe sehemu yenye maji kwa kuwa huko Negebu ulikonipa ni kukavu.” Basi, Kalebu akampa chemchemi za maji zilizokuwa kwenye nyanda za juu na za chini.
20Hii ndiyo nchi waliyopewa watu wa kabila la Yuda kulingana na koo zake. 21Miji iliyokuwa upande wa kusini kabisa wa nchi ya Yuda kuelekea mpaka wa Edomu ilikuwa: Kabseeli, Ederi, Yaguri, 22Kina, Dimona, Adada, 23Kedeshi, Hazori, Ithnani, 24Zifu, Telemu, Bealothi, 25Hazor-hadata, Kerioth-hezroni (yaani Hazori), 26Amamu, Shema, Molada, 27Hasar-gada, Heshmoni, Beth-peleti, 28Hasar-shuali, Beer-sheba, Biziothia, 29Baala, Iyimu, Ezemu, 30Eltoladi, Kesili, Horma, 31Siklagi, Madmana, Sansana, 32Lebaothi, Shilhimu, Aini na Rimoni. Jumla ya miji waliyopewa ni ishirini na tisa pamoja na vijiji vyake.
33Miji iliyokuwa kwenye tambarare ilikuwa: Eshtaoli, Sora, Ashna, 34Zanoa, Enganimu, Tapua, Enamu, 35Yarmuthi, Adulamu, Soko, Azeka, 36Shaaraimu, Adithaimu, Gedera na Gederothaimu. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na minne pamoja na vijiji vyake.
37Walipewa pia miji ya Senani, Hadasha, Migdal-gadi, 38Dileani, Mizpa, Yoktheeli, 39Lakishi, Boskathi, Egloni, 40Kaboni, Lahmamu, Kithlishi, 41Gederothi, Beth-dagoni, Naama na Makeda. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake. 42Tena walipewa miji ya Libna, Etheri, Ashani, 43Yifta, Ashna, Nezibu, 44Keila, Akzibu na Maresha. Jumla ya miji waliyopewa ni tisa pamoja na vijiji vyake. 45Vilevile walipewa Ekroni pamoja na miji yake midogo na vijiji, 46miji yote na vijiji vilivyokuwa karibu na Ashdodi kati ya Ekroni na bahari, 47Ashdodi na Gaza pamoja na miji na vijiji vyake, mpaka kijito cha Misri hadi pwani ya bahari ya Mediteranea.
48Miji iliyokuwa kwenye eneo la milimani ni Shamiri, Yatiri, Soko, 49Dana, Kiriath-sana (yaani Debiri), 50Anabu, Eshtemoa, Animu, 51Gosheni, Holoni na Gilo. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na mmoja pamoja na vijiji vyake. 52Walipewa pia miji ya Arabu, Duma, Eshani, 53Yanimu, Beth-tapua, Afeka, 54Humta, Kiriath-arba (yaani Hebroni) na Siori. Jumla ya miji waliyopewa ni tisa pamoja na vijiji vyake. 55Pia walipewa miji ya Maoni, Karmeli, Zifu, Yuta, 56Yezreeli, Yokdeamu, Zanoa, 57Kaini, Gibea na Timna. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi pamoja na vijiji vyake. 58Vilevile miji ya Halhuli, Beth-suri, Gedori, 59Maarathi, Beth-anothi na Eltekoni. Jumla ya miji waliyopewa ni sita pamoja na vijiji vyake. 60Kadhalika walipewa Kiriath-baali, uitwao pia Kiriath-yearimu, na Raba. Jumla ya miji waliyopewa ni miwili pamoja na vijiji vyake.
61Miji ya nyikani ilikuwa Beth-araba, Midini, Sekaka, 62Nibshani, Mji wa Chumvi na Engedi. Jumla ya miji waliyopewa ni sita pamoja na vijiji vyake.
63 Taz Amu 1:21; 2Sam 5:6; 1Nya 11:4 Lakini watu wa Yuda hawakuweza kuwafukuza Wayebusi, ambao ndio waliokuwa wenyeji wa Yerusalemu, na mpaka leo Wayebusi bado wanaishi mjini humo pamoja na watu wa Yuda.


Yoshua 15;1-63

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.