Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 18 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 35...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Haleluyah..!! Mungu wetu yu mwema sana..
Asante Baba wa Mbinguni kwa kutuamsha salama na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwa uwezo wetu wala nguvu zetu, si kwamba sisi ni wema sana na wazuri mno zaidi ya wengine walioshindwa kuamka leo hii..
Ni kwa Neema/Rehema zako tuu Mungu wetu..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe..kwa kuwaza,kwakunena, kwakutenda, kwakujua/kutojua..

Tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Tazama Jana imepita Baba wa Mbinguni Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..
Tunaomba ukaibariki siku hii..
 Utulinde  na ukatuokoe na yule mwovu na kazi zake ..


Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..


  Tunaomba ukabariki kazi zetu,Biashara, Masomo na ukabariki Vilaji/vinywaji,kuingia/kutoka kwetu, vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa mbinguni ukavitakase na kuvifunika kwa Damu Ya Bwana we Yesu Kristo...


Tazama wenye shida/tabu Baba wa mbinguni, wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali, wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao,waliokwenye vifungo mbalimbali Jehovah.. tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu, wakapate uponyaji na wasipungukiwe katika mahitaji yao na ukawape sawasawa na mapenzi yako..

Jehovah tuwaweka watoto wetu wanaondelea na mitihani na wanaojiandaa na mitihani, Yahweh ukawape ufahamu  na uelewa,wapate  kukumbuka yote waliyofundishwa..
 Baba ukawaongoze katika makuzi yao na maisha yao, ukawaokoe na vishawishi na kufuata mkumbo..wakujue Mungu na kufuata njia iliyo njema..wakue kimwili, kimo na kiimani pia..


Yesu anawabariki watoto wadogo
(Mat 19:13-15; Luka 18:15-17)
Watu walimletea Yesu watoto wadogo ili awaguse, lakini wanafunzi wakawakemea. Yesu alipoona hivyo, alikasirika akawaambia, “Waacheni hao watoto waje kwangu, wala msiwazuie, kwa maana ufalme wa Mungu ni kwa ajili ya watu walio kama watoto hawa. Nawaambieni kweli, mtu yeyote asiyeupokea ufalme wa Mungu kama mtoto mdogo hataingia humo.” Kisha akawapokea watoto hao, akawawekea mikono, akawabariki.
Asante kwa sababu wewe ni Mungu wetu na Mlinzi wetu Mkuu, Asante kwa wema na fadhili zako, Asante kwa ridhiki zetu, Asante kwa yote Jehovah..!Maisha yetu yapo nawe Mfalme wa Amani, Upendo upo kwako Yahweh..!Ufalme wa Mbinguni una wewe Baba wa Mbinguni, Amani ipo kwako, Furaha na Ushindi  vipo nawe Jehovah nissi..!Tumaini la kweli lipo kwako Yahweh..Sifa na utukufu tunakurudishia wewe..
Tunashukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu unayetosha..
Amina..!
Asanteni wote mnaopita hapa Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea sawasawa na mapenzi yake..

Nawapenda.


Kanuni za Sabato

1Mose alikusanya jumuiya yote ya Waisraeli, akawaambia, “Haya ndiyo mambo ambayo Mwenyezi-Mungu amewaamuru muyafanye: 2Taz Kut 20:8-11; 23:12; 31:15; 34:21; Lawi 23:3; Kumb 5:1-14 Kwa siku sita mtafanya kazi zenu; lakini siku ya saba ni Sabato siku ya mapumziko ambayo ni wakfu kwa Mwenyezi-Mungu. Yeyote atakayefanya kazi siku hiyo lazima auawe. 3Msiwashe hata moto katika makao yenu siku ya Sabato.”

Matoleo kwa ajili ya hema takatifu
(Kut 25:1-9)

4Mose aliiambia jumuiya yote ya Waisraeli, “Hili ndilo jambo ambalo Mwenyezi-Mungu amewaamuru mlifanye: 5Mtatoa katika mali zenu mchango wa kumpa Mwenyezi-Mungu. Kila mtu mwenye moyo mwema atamletea Mwenyezi-Mungu mchango: Dhahabu, fedha, shaba; 6sufu ya buluu, ya zambarau na nyekundu; kitani safi iliyosokotwa; manyoya ya mbuzi; 7ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, ngozi za mbuzi; mbao za mjohoro, 8mafuta kwa ajili ya taa, viungo kwa ajili ya mafuta ya kupaka na kwa ajili ya ubani wenye harufu nzuri; 9vito vya sardoniki na vito vingine kwa ajili ya mapambo ya kizibao na kifuko cha kifuani.

Vifaa vya hema takatifu
(Kut 39:32-43)

10“Kila mtu mwenye ujuzi wa kazi fulani miongoni mwenu atakuja kufanya vitu vyote alivyoamuru Mwenyezi-Mungu: 11Kutengeneza hema takatifu, kifuniko chake na pazia lake, kulabu zake, pau zake, vikalio vyake; 12sanduku la agano pamoja na mipiko yake, kiti cha rehema, pazia la mahali patakatifu sana; 13meza na mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, mikate iliyowekwa mbele ya Mwenyezi-Mungu; 14vinara vya taa pamoja na vyombo vyake vyote, taa zake na mafuta yake; 15madhabahu ya ubani na mipiko yake, mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri, pazia la mlango wa hema takatifu; 16madhabahu ya sadaka za kuteketezwa pamoja na wavu wa shaba, mipiko yake pamoja na vyombo vyake vyote, birika na tako lake; 17vyandarua vya ua, nguzo zake na vikalio vyake, pazia la mlango wa ua; 18vigingi vya hema takatifu na vya ua pamoja na kamba zake; 19mavazi yaliyofumwa vizuri kabisa kwa ajili ya huduma ya mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na ya wanawe, kwa ajili ya huduma yao ya ukuhani.”

Watu wanaleta matoleo yao

20Basi, jumuiya yote ya Waisraeli ikaondoka mbele ya Mose. 21Kila mtu aliyevutwa na kusukumwa moyoni mwake alimtolea Mungu mchango wake kwa ajili ya hema la mkutano, huduma zake zote na mavazi yake matakatifu. 22Hivyo wote wenye moyo mkarimu, wanaume kwa wanawake, wakaleta vipini, pete za mhuri, vikuku na kila aina ya vyombo vya dhahabu; kila mtu akamtolea Mwenyezi-Mungu kitu cha dhahabu. 23Kila mtu alileta chochote alichokuwa nacho kama vile sufu ya rangi ya buluu zambarau na nyekundu, au kitani safi, au manyoya ya mbuzi au ngozi ya kondoo iliyotiwa rangi nyekundu. 24Kila mtu aliyeweza kutoa fedha au shaba aliileta kwa Mwenyezi-Mungu kama toleo lake. Tena mtu yeyote aliyekuwa na mbao za mjohoro alileta pia. 25Wanawake wote waliokuwa na ujuzi wa kufuma walileta vitu walivyofuma kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. 26Na wanawake wote waliokuwa na ujuzi walisokota manyoya ya mbuzi. 27Viongozi walileta vito vya rangi na mawe mengine kwa ajili ya kizibao na kifuko cha kifuani; 28walileta pia viungo na mafuta kwa ajili ya taa, mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri. 29Waisraeli wote, wanaume kwa wanawake, ambao walivutwa moyoni mwao kuleta chochote kwa ajili ya kazi ambayo Mwenyezi-Mungu alikuwa amemwagiza Mose ifanyike, walileta vitu hivyo kwa hiari, kama mchango wa kumpa Mwenyezi-Mungu.

Mafundi kwa ajili ya hema la mkutano
(Kut 31:1-11)

30Mose aliwaambia Waisraeli; “Tazameni! Mwenyezi-Mungu amemteua Bezaleli, mwana wa Uri, mwana wa Huri, wa kabila la Yuda. 31Amemjaza roho yake, amempa ujuzi, akili, maarifa na ufundi, 32abuni michoro ya sanaa na kufanya kazi za kufua dhahabu, fedha na shaba; 33achonge mawe ya kupambia na mbao kwa ajili ya kazi nyingine zote za kifundi. 34Pia amemwongoza yeye na Oholiabu, mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani wawafundishe wengine. 35Amewapa ujuzi wa kufanya kila kazi ya ufundi au ifanywayo na watu wa sanaa au mafundi wa kutarizi kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa, kwa kutumia ufundi wowote wa msanii.

Kutoka35;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 17 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 34...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu...

Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na Fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako na kutuamsha salama, Asante kwa kutupa Kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tunakuja mbele zako Mungu wetu tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Baba Mungu tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe walio tukosea..
Roho mtakatifu akatuongoze tupate kutambua na kujitambua na tuwe na kiasi..
Baba tunaomba utulinde na kutuokoa na yule mwovu na kazi zake zote..ukatutakase Miili yetu na Akili zetu na utufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..

Tunajua kwamba kila aliye mtoto wa Mungu hatendi dhambi, kwa sababu Mwana wa Mungu humlinda salama, na yule Mwovu hawezi kumdhuru. Tunajua kwamba sisi ni wake Mungu ingawa ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu. Twajua pia kwamba Mwana wa Mungu amekuja, akatupa elimu ili tumjue Mungu wa kweli; tuishi katika muungano na Mungu wa kweli – katika muungano na Mwanae, Yesu Kristo. Huyu ndiye Mungu wa kweli, na huu ndio uhai wa milele. Watoto wangu, epukaneni na sanamu za miungu!

Asante Mungu wetu kwa Upendo wako kwetu ,Nasi ukatupe moyo wa upendo kwa wengine, tukawe na upendo wa kweli..

Wapenzi wangu, tupendane, maana upendo hutoka kwa Mungu. Kila mtu aliye na upendo ni mtoto wa Mungu, na anamjua Mungu. Mtu asiye na upendo hamjui Mungu, maana Mungu ni upendo. Na Mungu alionesha upendo wake kwetu kwa kumtuma Mwanae wa pekee ulimwenguni, ili tuwe na uhai kwa njia yake. Hivi ndivyo upendo ulivyo: Si kwamba sisi tulikuwa tumempenda Mungu kwanza, bali kwamba yeye alitupenda hata akamtuma Mwanae awe sadaka ya kutuondolea dhambi zetu. Wapenzi wangu, ikiwa Mungu alitupenda hivyo, basi, nasi tunapaswa kupendana.

Asante kwa ridhiki zetu Baba wa Mbinguni tunaomba ukazibariki nasi tuweze kuwabariki wengine wenye kuhitaji..
Asante kwa kazi zetu,Biashara,Masomo tunaviweka mikononi mwako Baba wa mbinguni tunaomba ukabariki na kutuongoza vyema..
Mfalme wa Amani ukabariki tuingiapo/tutokapo, vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..!
Vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Jehovah..! Ukavitakase kwa Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo..
Mfalme wa Amani tazama wenye shida/tabu, wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao,waliokwenye vifungo mbalimbali, wanaopitia magumu/majaribu yoyote Mungu wetu, Baba yetu, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.. Tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu na uponyaji..wakapate kupona kimwili na kiroho pia..ukaonekane kwenye mapito yao Baba..
Maisha yetu yapo mikononi mwako Baba wa Mbinguni hatuna Mungu mwingine, hakuna wa kuabudiwa ila ni wewe tuu Mfalme wa Amani.. wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho, wewe ni Alfa na Omega..Sifa na utukufu ni wako Jehovah Jireh...!!

Tunayaweka haya yote mikononi mwako, Tunashukuru na kukuabudu Mungu wetu..
Amina..!!

Asanteni kwakutembelea hapa..
Mungu aendelee kuwabariki na kubariki kazi zenu na familia zenu..

Awape sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda.

Vibao vipya vya agano

(Kumb 10:1-5)

1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Chonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza, nami nitayaandika maneno yale yaliyokuwa katika vile vibao vya kwanza ulivyovivunja. 2Uwe tayari kesho asubuhi, uje kukutana nami mlimani Sinai. 3Mtu yeyote asije pamoja nawe, wala asionekane popote mlimani; wala kondoo au ng'ombe wasilishwe karibu yake.” 4Basi, Mose akachonga vibao viwili vya mawe kama vile vya kwanza. Akaondoka asubuhi na mapema, akapanda mlimani Sinai, kama Mwenyezi-Mungu alivyomwamuru, akiwa na vile vibao viwili vya mawe mikononi mwake. 5Mwenyezi-Mungu akashuka katika wingu, akasimama pamoja na Mose, akalitaja jina lake, “Mwenyezi-Mungu.” 6Taz Kut 20:5-6; Hes 14:18; Kumb 5:9-10; 7:9-10 Kisha Mwenyezi-Mungu akapita mbele ya Mose akitangaza tena, “Mwenyezi-Mungu; mimi Mwenyezi-Mungu, ni Mungu mwenye huruma na neema; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili na uaminifu. 7Mimi nawafadhili maelfu,34:7 maelfu: Au Maelfu ya vizazi. nikiwasamehe uovu, makosa na dhambi; lakini kwa vyovyote vile sitaacha kumwadhibu mwenye hatia; nawapatiliza watoto na wajukuu uovu wa baba na babu zao, hata kizazi cha tatu na nne.”
8Mose akainama chini mara, akamwabudu Mungu. 9Kisha akasema, “Ee Bwana wangu, kwa vile umenijalia fadhili mbele zako, nakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na dhambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.”

Agano lafanywa upya

(Kut 23:14-19; Kumb 7:1-5; 16:1-17)

10Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Sasa ninafanya agano na watu wako. Nitatenda maajabu mbele yao ambayo hayajapata kutendwa duniani kote, wala katika taifa lolote. Na watu wote mnaoishi kati yao wataona matendo yangu makuu. Maana nitafanya jambo la ajabu kwa ajili yako.
11“Shikeni amri ninazowapa leo. Nitawafukuza mbele yenu Waamori, Wakanaani, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. 12Jihadharini msije mkafanya agano na wakazi wa nchi mnayoiendea, maana hilo litakuwa mtego miongoni mwenu. 13Taz Kumb 16:21 Lakini mtazibomoa madhabahu zao na kuzivunja nguzo zao za ibada na sanamu zao za Ashera.34:13 Ashera: Mungu wa kike aliyeabudiwa na wananchi wa Kanaani. 14Msiabudu mungu yeyote mwingine, maana mimi Mwenyezi-Mungu najulikana kwa jina: ‘Mwenye Wivu,’ mimi ni Mungu mwenye wivu. 15Msifanye mikataba yoyote na wakazi wa nchi hiyo, maana watakapoiabudu miungu yao ya uongo na kuitambikia, watawaalikeni, nanyi mtashawishiwa kula vyakula wanavyoitambikia miungu yao, 16nao wavulana wenu wakaoa binti zao, na hao binti wanaoabudu miungu yao, wakawashawishi wavulana wenu kufuata miungu yao.
17 Taz Kut 20:4; Lawi 19:4; Kumb 5:8; 27:15 “Msijifanyie miungu ya uongo ya chuma.
18 Taz Kut 12:14-20; Lawi 23:6-8; Hes 28:16-25 “Mtaiadhimisha sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu. Kwa muda wa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu wakati uliopangwa katika mwezi wa Abibu,34:18 mwezi wa Abibu: Ni kati ya Machi na Aprili katika kalenda yetu. kama nilivyowaamuru, kwa sababu katika mwezi huo wa Abibu mlitoka Misri. 19Taz Kut 13:2 Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume ni wangu, pamoja na wazaliwa wa kwanza wa kiume wa wanyama wako wote, wa ng'ombe na wa kondoo. 20Mzaliwa wa kwanza wa punda utamkomboa kwa kunitolea kondoo. Kama hutamkomboa utamvunja shingo. Watoto wenu wote wa kiume ambao ni wazaliwa wa kwanza mtawakomboa. Mtu yeyote asije mbele yangu mikono mitupu.
21“Siku sita mtafanya kazi zenu, lakini siku ya saba mtapumzika, hata ikiwa ni wakati wa kulima au kuvuna. 22Taz Kut 23:16 Mtaadhimisha sikukuu ya majuma34:22 majuma: Au Pentekoste. mwanzoni mwa majira ya mavuno ya ngano, na sikukuu ya kukusanya mavuno mwishoni mwa mwaka. 23Mara tatu kwa mwaka wanaume wote watakusanyika mbele yangu mimi Bwana Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli. 24Nitayafukuza mataifa mengine mbele yenu na kuipanua mipaka yenu. Hakuna mtu yeyote atakayeitamani nchi yenu wakati mnapokusanyika kuniabudu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu mara tatu kila mwaka.
25“Msinitolee damu ya tambiko yangu pamoja na chachu; wala tambiko ya sikukuu ya Pasaka isibakizwe mpaka asubuhi.
26 Taz Kumb 24:21; 26:2 “Mazao ya kwanza ya ardhi yako utayaleta nyumbani kwangu mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wako.
“Usimchemshe mwanakondoo au mwanambuzi katika maziwa ya mama yake.”
27Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Andika maneno haya, maana kulingana na maneno haya, ninafanya agano nawe na watu wa Israeli.” 28Mose alikaa huko mlimani pamoja na Mwenyezi-Mungu siku arubaini, mchana na usiku; hakula chakula wala kunywa maji. Aliandika maneno yote ya agano na zile amri kumi.

Mose anashuka kutoka mlimani Sinai

29 Taz 2Kor 3:7-16 Mose alipokuwa anashuka mlimani Sinai akiwa na vile vibao viwili vyenye maneno ya agano mikononi mwake, hakujua kuwa uso wake ulikuwa unangaa kwa sababu alikuwa ameongea na Mwenyezi-Mungu. 30Aroni na watu Waisraeli wote walipomwona waliogopa kumkaribia, kwani uso wake ulikuwa unangaa. 31Lakini Mose alimwita Aroni na viongozi wa jumuiya ya Waisraeli waende karibu naye, kisha akazungumza nao. 32Baadaye Waisraeli wote wakaja karibu naye, naye akawapa amri zote ambazo Mwenyezi-Mungu alimpa kule mlimani Sinai. 33Mose alipomaliza kuzungumza na watu aliufunika uso wake kwa kitambaa. 34Lakini ikawa kwamba kila mara Mose alipokwenda kuongea na Mwenyezi-Mungu katika hema la mkutano, alikiondoa kile kitambaa mpaka alipotoka nje. Na alipotoka nje aliwaambia Waisraeli mambo yote aliyoamriwa, 35nao Waisraeli waliuona uso wake unangaa. Ndipo Mose alipoufunika tena uso wake kwa kitambaa mpaka alipokwenda kuongea na Mwenyezi-Mungu.

Kutoka34;1-35

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 16 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 33...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu katika yote.
Asante Baba wa Mbinguni, Mungu wetu,Baba yetu,Muumba wetu,Muumba mbingu na Nchi, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo..Yahweh..!Jehovah..!El Shaddai..!Elohim..!Adonai..!
Asante kwa wema na Fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako na kutumsha salama..
Asante kwa kutuchagua na kutupa Kibali cha kuendelea kuiona Leo hii..
Tunashuka mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mungu wetu..

Tunaomba utusamehe pale tulipo kwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda, kwakujua/kutojua..
Baba tunaomba nasi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika kunena na kutenda,tukawe na kiasi na  tukawe chombo chema  tukatumike sawasawa na mapenzi yako..


Tunashukuru kwa uponyaji na ulinzi wako Mfalme wa Amani.. Asante kwa ridhiki zako Mungu wetu, Asante kwa kazi ulizotupa Baba wa Mbinguni, Asante kwa Biashara na Masomo pia..Asante kwa familia zetu na nyumba zetu Mfalme wa Amani..Asante kwa yote tuliyoyanena na tuliyoyaacha Baba wa Mbinguni unayajua na wewe unatujua vyema..
Tunaomba ukavibariki na kutubariki katika yote na tusipungukiwe katika mahitaji yetu na ukatupe sawasawa na mapenzi yako..
Baba ukawabariki na wengine wanaohitaji na wataabikao,wenye shida/Tabu,waliovifungoni,wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao, wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali Jehovha tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu.. ukawaponye na kuwainua, ukaonekane kwenye Taabu zao Baba wapate kupona kimwili na kiroho pia..

Jehovah..! Tunawaweka watoto wetu mikononi mwako, wewe ukawe mlinzi mkuu katika maisha yao, ukawaongoze katika masomo na ujana wao, makuzi yao na hatua zao za ukuaji ziwe nawe..wapate kukujua wewe katika maisha yao..Ukawabariki na wakawe Baraka kwa wazazi/walezi,Ndugu,walimu na jamii pia..



Mwanangu, moyo wako ukiwa wenye busara, moyo wangu pia utakuwa wenye furaha. Moyo wangu utashangilia, mdomo wako utakaposema maneno yaliyo sawa.


Baba ukatuongoze wazazi/walezi katika malezi yetu..tusipotoke na huu ulimwengu wa leo wenye mambo mengi ya kutisha tunayodhania ni maendeleo na usasa..ukatupe hekima na busara katika malezi,ukatupe kiasi,Upendo na upole kiasi..tukawe wasimamizi wema na mfano bora kwa watoto wetu..

Usiache kumrudi mtoto; ukimchapa kiboko hatakufa. Ukimtandika kiboko, utayaokoa maisha yake na kuzimu.
Asiyemwadhibu mtoto wake hampendi; lakini ampendaye mwanawe humrudi mapema.

Wazee huwaonea fahari wajukuu zao; watoto huwaonea fahari wazazi wao.
Eeh -Mungu wetu tunaomnba utuongoze..!!
Tunarudisha sifa na utukufu ni wako..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako Baba wa Mbinguni,Tukishukuru na kuamini kwako wewe yote yanawezekana..
Amina..!!
Asanteni wote mliopita/mnaondelea kupita hapa..
Mungu Baba akawabariki katika yote..
Nawapenda.


Mungu amwamuru Mose waanze safari

1 Taz Mwa 12:7; 26:3; 28:13 Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Anza safari uondoke hapa, wewe na watu hao uliowatoa nchini Misri, mwende katika nchi niliyomwapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, nikisema, ‘Nitawapa wazawa wenu nchi hii’. 2Nitamtuma malaika awaongoze; nitawafukuza Wakaanani, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi. 3Nendeni katika nchi hiyo inayotiririka maziwa na asali. Lakini kwa sababu nyinyi ni wenye vichwa vigumu sitakwenda pamoja nanyi, nisije nikawaangamiza njiani.”
4Watu walilia waliposikia habari hizi mbaya; wala hakuna aliyevaa mapambo yake. 5Walifanya hivyo kwani Mwenyezi-Mungu alikuwa amemwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Nyinyi ni watu wenye vichwa vigumu; nikienda pamoja nanyi kwa muda mfupi tu, nitawaangamiza. Hivyo vueni mapambo yenu ili nijue namna ya kuwatendea.’” 6Basi, Waisraeli waliyavua mapambo yao tangu walipoondoka mlimani Horebu.

Hema la mkutano

7Mose alikuwa na desturi ya kulichukua lile hema na kulisimika nje ya kambi. Hema hilo alilipa jina, Hema la Mkutano. Mtu yeyote aliyetaka shauri kwa Mwenyezi-Mungu alikwenda kwenye hema la mkutano nje ya kambi. 8Kila mara Mose alipotoka kwenda kwenye hema hilo, kila mtu alisimama penye mlango wa hema lake na kumwangalia Mose mpaka alipoingia ndani ya hilo hema. 9Wakati Mose alipoingia ndani ya hilo hema, mnara wa wingu ulitua kwenye mlango wa hema, na Mwenyezi-Mungu akaongea naye. 10Watu wote walipouona ule mnara wa wingu umesimama mlangoni mwa hema, kila mmoja wao alisimama na kuabudu mlangoni mwa hema lake. 11Hivyo ndivyo Mwenyezi-Mungu alivyokuwa akiongea na Mose uso kwa uso, kama mtu na rafiki yake. Kisha Mose alirudi tena kambini. Naye kijana Yoshua mwana wa Nuni ambaye alikuwa mtumishi wake hakuondoka hemani.

Mwenyezi-Mungu aahidi kuwa na watu wake

12Mose akamwambia Mwenyezi-Mungu, “Tazama! Wewe waniambia, ‘Waongoze watu hawa,’ lakini hujanijulisha ni nani utakayemtuma anisaidie. Hata hivyo umesema kwamba unanijua kwa jina na pia kwamba nimepata fadhili mbele zako. 13Sasa basi, nakusihi, kama kweli nimepata fadhili mbele yako, nioneshe sasa njia zako, ili nipate kukujua na kupata fadhili mbele zako. Naomba ukumbuke pia kwamba taifa hili ni watu wako.”
14Mungu akasema, “Mimi mwenyewe nitakwenda pamoja nawe, na nitakupa faraja.” 15Mose akasema, “Kama wewe binafsi hutakwenda pamoja nami, basi, usituondoe mahali hapa. 16Maana nitajuaje kuwa nimepata fadhili mbele zako, mimi na watu wako kama usipokwenda pamoja nasi? Ukienda pamoja nasi itatufanya mimi na watu wako kuwa watu wa pekee miongoni mwa watu wote duniani.”
17Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kwa kuwa umepata fadhili mbele yangu, nami nakujua kwa jina lako, jambo hilihili ulilolisema nitalifanya.” 18Mose akasema, “Nakusihi unioneshe utukufu wako.” 19Taz Rom 9:15 Mwenyezi-Mungu akamjibu, “Nitapita mbele yako na kukuonesha wema wangu wote nikilitangaza jina langu, ‘Mwenyezi-Mungu’. Mimi nitamrehemu yule ninayependa kumrehemu, na kumhurumia yule ninayependa kumhurumia. 20Lakini hutaweza kuniona uso maana hakuna mwanadamu yeyote atakayeniona na kuishi.” 21Kisha Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Kuna mahali karibu nami ambapo utasimama juu ya mwamba; 22na utukufu wangu utakapokuwa unapita, nitakutia katika pango mwambani na kukufunika kwa mkono wangu, mpaka nitakapokuwa nimepita. 23Halafu nitauondoa mkono wangu nawe utaniona nyuma, lakini uso wangu hutauona.”Kutoka33;1-23


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 15 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 32...


Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu katika yote...
Mtakatifu..!Mtakatifu..!Mtakatifu..! Baba wa Mbinguni, Baba yetu,Mungu wetu, Muumba wetu, Muumba mbingu na Nchi, Na vyote vilivyomo, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo..

Asante kwa wema na fadhili zako,Asante kwa  ulinzi wako usiku mzima na kutuamsha salama, Asante kwa kutuchagua  na kutupa kibali cha kuendelea kuiona Wiki/siku hii..
si kwa uwezo wetu, Nguvu zetu/utashi wetu, si kwamba sisi ni wema sana na tumetenda mazuri sana, si kwamba sisi ni wajuaji na wenye sifa zote, si kwamba sisi ni wazuri mno.. Hapana Baba wa Mbinguni ni kwa Neema/Rehema zako tuu sisi kuendelea kuiona leo hii..


Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Baba wa Mbinguni, Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena, kwakutenda, kwakujua/kutojua..

Baba tunaomba utupe nasi Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea na kuachilia kabisa..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Ukatupe kutambua na kujitambua..
Tazama Jana imepita Yahweh..! Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..Mfalme wa Amani tunaomba ukatawale maisha yetu,Ukabariki ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo nasi tukaweze kuwabariki wengine wenye kuhitaji..
Ukabariki kuingia kwetu na kutoka kwetu, vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe..
Ukabariki Kazi zetu,Biashara, Masomo na ukabariki vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Jehovah ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..


Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu... Ukatamalaki na ukaonekane katika maisha yetu..
Ukatuokoe na kutulinda na yule mwovu na kazi zake, ukatufunike na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo,Ukatuponye rohoni Baba wa Mbinguni na tukawe barua njema tukasomoke sawasawa na mapenzi yako..


Ukabariki familia zetu na tunaziweka Ndoa zetu mikononi mwako Mfalme wa Amani...
Ukawabariki Yatima na Wajane Mfalme wa Amani na ukawabariki na kuwakugusa na mkono wako wenye nguvu wote wanaopitia magumu/majaribu,vifungo mbalimabali,wagonjwa, wafiwa ukawe mfariji wao..
Baba tazama waliokata tamaa, wenye hofu/mashaka,waliokataliwa na waliokwama katika maisha yao, maisha  hayaendi iwe kazi, iwe masomo,Biashara,watoto watukutu/hawasikii, Amani kwenye nyumba/maisha yao imepotea..Baba ukawape kupona kiroho na ukawaongoze na wakapate tumaini na ukaonekane kwenye maisha yao ukawaonyeshe njia..
Ndugu yangu unayepita kweye Magumu/Majaribu usisite kumpa Yesu maisha yako,mtafute Mungu anapatikana, Fanya bidii ya kumjua yeye naye atakuinua..


mkabidhi kazi zako, maisha yako,masomo yako na kabla ya kufanya vyote hivyo muulize Mungu unachofanya ndicho chako?yeye akakuongoze, fanya bidii katika unalolifanya na Mungu akawe kiongozi wako..

Mtafuteni Mwenyezi-Mungu wakati bado anapatikana, mwombeni msaada wakati yupo bado karibu. Waovu na waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamrudie Mwenyezi-Mungu apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe. Maana, Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Mawazo yangu si kama mawazo yenu, wala njia zangu si kama njia zenu. Kama vile mbingu zilivyo mbali na dunia, ndivyo njia zangu zilivyo mbali na zenu, na mawazo yangu mbali na mawazo yenu. “Kama vile mvua na theluji ishukavyo toka mbinguni, wala hairudi huko bali huinywesha ardhi, ikaifanya ichipue mimea ikakua, ikampatia mpanzi mbegu na kuwapa watu chakula, vivyo hivyo na neno langu mimi: Halitanirudia bila mafanikio, bali litatekeleza matakwa yangu, litafanikiwa lengo nililoliwekea.

Tunakushuru Mungu wetu na tunayaweka haya yote mikononi mwako..
tukiamini na kukusifu daima..
Amina..!!
Niwashukuru wote mnaopita hapa..
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea makuu,
Nawapenda.

Sanamu ya ndama wa dhahabu

(Kumb 9:6-29)

1 Taz Mate 7:40,41; 1Fal 12:28 Watu walipoona kuwa Mose amechelewa kurudi kutoka mlimani, walikusanyika mbele ya Aroni na kumwambia, “Haya! Tutengenezee miungu itakayotuongoza maana hatujui lililompata huyo Mose aliyetutoa nchini Misri.” 2Aroni akawajibu, “Chukueni vipuli vya dhahabu masikioni mwa wake zenu, wana wenu na binti zenu, mniletee.” 3Basi, watu wote wakatoa vipuli vyote vya dhahabu masikioni mwao, wakamletea Aroni. 4Naye akavichukua akaviyeyusha, akatengeneza ndama wa kusubu. Watu wakapaza sauti, “Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa nchini Misri.”
5Kisha Aroni akamjengea huyo ndama madhabahu, halafu akatangaza, “Kesho kutakuwa na sikukuu kwa ajili ya Mwenyezi-Mungu.” 6Taz 1Kor 10:7 Kesho yake watu waliamka mapema wakatoa sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani. Watu wakaketi chini kula na kunywa; kisha wakasimama na kucheza.
7Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Teremka chini kwa maana watu wako uliowaleta kutoka nchini Misri wamejipotosha wenyewe; 8wameiacha mara moja njia niliyowaamuru, wakajifanyia ndama wa kusubu, nao wamemwabudu na kumtolea tambiko wakisema, ‘Ee Israeli, huyu ndiye mungu wetu aliyetutoa nchini Misri!’ 9Nawafahamu watu hawa; wao wana vichwa vigumu. 10Sasa, usijaribu kunizuia. Niache niwaangamize kwa ghadhabu kali; kisha kutokana nawe nitaunda taifa kubwa.”
11 Taz Hes l4:13-19 Lakini Mose akamsihi Mwenyezi-Mungu, Mungu wake, akisema, “Ee Mwenyezi-Mungu, kwa nini hasira yako inawaka vikali dhidi ya watu wako uliowatoa nchini Misri kwa uwezo mkuu na mkono wenye nguvu? 12Ukifanya hivyo, hakika Wamisri watasema, ‘Aliwatoa kwa nia mbaya ili kuwaulia mlimani na kuwateketeza kabisa duniani.’ Ee Mwenyezi-Mungu, tuliza hasira yako kali na kuacha jambo hilo baya ulilokusudia kufanya dhidi ya watu wako. 13Taz Mwa 22:16-17; 17:8 Wakumbuke watumishi wako, Abrahamu, Isaka na Israeli, ambao uliwaapia kwa nafsi yako mwenyewe, ukisema, ‘Nitawazidisha wazawa wenu kama nyota za mbinguni na nchi yote hii niliyowaahidia nitawapa vizazi vyenu wairithi milele.’” 14Basi, Mwenyezi-Mungu akaacha kuwafanyia watu wake lile jambo baya alilokuwa amesema.
15Kisha Mose akashuka kutoka mlimani akiwa na vibao viwili vya mawe mikononi mwake, vimeandikwa amri za Mungu pande zote. 16Vibao hivyo vilikuwa kazi yake Mungu mwenyewe na maandishi hayo aliyachora Mungu mwenyewe.
17Yoshua aliposikia kelele za watu, akamwambia Mose, “Kuna kelele za vita kambini.” 18Lakini Mose akamjibu, “Si kelele ya ushindi au kushindwa, bali kelele ninayosikia ni kelele ya watu wanaoimba.” 19Mara tu walipoikaribia kambi walipomwona yule ndama na watu wakicheza; hapo hasira ya Mose ikawaka kama moto, akavitupa chini vile vibao kutoka mikononi mwake na kuvivunja pale chini ya mlima. 20Basi, akamchukua yule ndama akamchoma moto, akamsaga mpaka akawa unga, akaukoroga unga huo katika maji na kuwalazimisha Waisraeli wanywe.
21Mose akamwuliza Aroni, “Walikufanya nini watu hawa hata ukawaingiza katika dhambi kubwa hivyo?” 22Aroni akamjibu, “Nakuomba ee bwana wangu hasira yako isiniwakie mimi mtumishi wako. Unawafahamu jinsi watu hawa walivyo tayari kutenda maovu. 23Walikuja wakaniambia, ‘Tufanyie miungu ambayo itatuongoza kwani huyo Mose aliyetutoa nchini Misri hatujui lililompata’. 24Nami nikawaambia, kila mmoja aliye na vito vya dhahabu na avilete. Basi, wakaniletea, nami nikaviyeyusha motoni na huyu ndama akatokea.”
25Basi, Mose alipoona kuwa watu wameasi na kufanya wapendavyo (kwa kuwa Aroni aliwafanya waasi na kufanya wapendavyo, na kujiletea aibu mbele ya adui zao), 26Mose akasimama mbele ya lango la kambi na kuuliza, “Ni nani aliye upande wa Mwenyezi-Mungu? Na aje kwangu.” Wana wote wa Lawi wakakusanyika pamoja mbele yake. 27Akawaambia, “Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Kila mtu na ajifunge upanga wake kiunoni, azunguke kila mahali kambini, kutoka lango moja hadi lingine, na kila mmoja amuue ndugu yake, rafiki yake na jirani yake.’” 28Wana wa Lawi wakafanya kama Mose alivyowaagiza. Siku hiyo waliuawa watu wapatao 3,000. 29Mose akasema, “Leo mmejiweka wakfu32:29 Leo … wakfu: Makala ya Kiebrania: Jiwekeni wakfu leo au Mmewekwa wakfu leo. nyinyi wenyewe kumhudumia Mwenyezi-Mungu, kwa vile hamkusita hata kuwaua watoto wenu au ndugu zenu. Mungu awajalie baraka leo hii.”

Mose anawaombea Waisraeli

30Kesho yake Mose akawaambia watu, “Mmetenda dhambi kubwa! Sasa nitamwendea Mwenyezi-Mungu juu mlimani; labda nitafanya upatanisho kwa ajili ya dhambi yenu.” 31Hivyo Mose akarudi kwa Mwenyezi-Mungu, akamwambia, “Nasikitika! Watu hawa wametenda dhambi kubwa; wamejifanyia wenyewe miungu ya dhahabu. 32Taz Zab 69:28; Ufu 3:5 Lakini sasa, nakuomba uwasamehe dhambi yao. Ikiwa hutawasamehe, nakusihi unifute mimi katika kitabu chako ulichowaandika watu wako.” 33Lakini Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Nitamfuta katika kitabu changu mtu yeyote aliyenitendea dhambi. 34Lakini sasa nenda ukawaongoze watu mpaka mahali nilipokuambia. Tazama, malaika wangu atakutangulia. Hata hivyo, siku nitakapowajia, nitawaadhibu kwa sababu ya dhambi yao.”
35Mwenyezi-Mungu akawapelekea watu ugonjwa wa tauni, kwa kuwa walimwomba Aroni awafanyie yule ndama wa dhahabu.
Kutoka32;1-35


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Friday 12 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 31...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa mema yote aliyotutendea na anayoendelea kututendea..
Tunakushukuru Mungu wetu  kwa wema na fadhili zako, umetulinda usiku kucha na kutuamsha salama, Umetuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..Mungu wetu, Nuru na mwanga wetu,Jehova nissi..!, Jehovah shammah..!, Jehovah rapha..!, Jehovah Shalom..!,Jehovah rohi..!,Jehovah jireh..!Mungu unayeponya, Mungu unayetenda, Mungu unayejibu, Mungu unayebariki na wewe ni Mungu wa Rehema..

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe, kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua.
Baba nasi ukatupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea.

ukatupe macho ya rohoni tupate kutambua/kujitambua..tukawe na 
  hekima,busara,utuwema,upendo wa kweli na upole kiasi..
tuweze kuachilia na kuchukuliana..
Utuepeshe na chuki,hasira na kisasi, makwazo na kukwaza wengine..

Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha. Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa. Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe. Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema, ‘Nimetubu,’ lazima umsamehe.”
Roho Mtakatifu akatuongoze na tukawe na kiasi..

Baba wa Mbinguni tunaiweka siku hii na maisha yetu mikononi mwako, tunaomba ukaibariki na kutubariki katika yote tunayoenda kufanya/kutenda, ukatuongoze na kutulinda, ukatutakase Miili yetu na Akili zetu na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa mbinguni ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti.. Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Kwa imani na tumaini la kweli tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Sifa na utukufu ni wako Baba wa Mbinguni,Tunashukuru na kuku abudu siku zote za maisha yetu,,Ehh Mungu utuongoze..


Msifuni Mwenyezi-Mungu! Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu! Nitamsifu Mwenyezi-Mungu maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu muda wote niishipo. Msiwategemee wakuu wa dunia; hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa. Binadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi mavumbini alimotoka; na hapo mipango yake yote hutoweka. Heri mtu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mtu aliyeweka tumaini lake kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wake, aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo. Yeye hushika ahadi yake milele. Yeye huwapatia wanaoonewa haki zao, huwapa wenye njaa chakula. Mwenyezi-Mungu huwapa wafungwa uhuru, huwafungua macho vipofu. Mwenyezi-Mungu huwainua waliokandamizwa; huwapenda watu walio waadilifu. Mwenyezi-Mungu huwalinda wageni, huwategemeza wajane na yatima; lakini huipotosha njia ya waovu. Mwenyezi-Mungu atawala milele, Mungu wako, ee Siyoni, ni mfalme vizazi vyote! Msifuni Mwenyezi-Mungu!
                                           Amina..
Asanteni sana wote mnaotembelea hapa Mungu akawabariki katika yote..muwe salama Rohoni
Nawapenda.



Mafundi wa kutayarisha hema la mkutano

(Kut 35:30–36:1)

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 2“Mimi nimemteua Bezaleli, mwana wa Uri, mjukuu wa Huri, wa kabila la Yuda 3na kumjaza roho wangu. Nimempatia uzoefu na akili, maarifa na ufundi, 4ili abuni kazi za usanii na kufanya kazi za kufua dhahabu, fedha na shaba. 5Nimempatia ujuzi wa kuchonga mawe ya kupambia, kuchonga mbao, na ujuzi wa kila aina ya ufundi. 6Vilevile nimemteua Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, afanye kazi pamoja naye. Hali kadhalika nimewapa uwezo mkubwa watu wengine kwa ajili ya kazi mbalimbali, ili watengeneze vifaa vyote nilivyoagiza vifanywe: 7Hema la mkutano, sanduku la ushuhuda na kiti cha ushuhuda juu yake, pamoja na vifaa vyake vyote; 8meza na vyombo vyake, kinara safi cha taa na vyombo vyake, madhabahu ya kufukizia ubani, 9madhabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika la maji pamoja na tako lake, 10mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na wanawe ambao watafanya huduma ya ukuhani, 11mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri kwa ajili ya mahali patakatifu. Vitu hivyo vyote vitatengenezwa kulingana kabisa na jinsi nilivyokuamuru.”

Siku ya kupumzika

12Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 13“Waambie Waisraeli hivi: Nyinyi mtaadhimisha Sabato zangu, kwa sababu hizo ni ishara kati yenu na mimi kwa vizazi vyote kwamba mimi ndimi ninayewatakasa. 14Mtaiadhimisha Sabato, nayo itakuwa kwenu siku takatifu. Yeyote atakayeitia unajisi siku hiyo lazima auawe. Na mtu atakayefanya kazi yoyote siku hiyo atatengwa mbali na watu wake. 15Taz Kut 20:8-11; 23:12; 34:21; 35:21; Lawi 23:3; Kumb 5:12-14 Mtafanya kazi zenu kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba ni siku rasmi ya mapumziko, ni siku yangu takatifu. Mtu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo lazima atauawa. 16Kwa hiyo Waisraeli wataiadhimisha siku ya Sabato katika vizazi vyao vyote kama ishara ya agano la milele. 17Taz Kut 20:11 Jambo hili litakuwa ishara ya kudumu kati ya Waisraeli na mimi, maana mimi Mwenyezi-Mungu nilifanya mbingu na dunia kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba niliacha kufanya kazi, nikapumzika.”
18Mwenyezi-Mungu alipomaliza kuongea na Mose mlimani Sinai, alimpatia Mose vile vibao viwili vya mawe ambavyo yeye Mungu aliviandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.

Kutoka31;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 11 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 30...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu yeye atosha..
Mungu wetu, Baba yetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi, Muumba wa vyote, Vyote ni mali yako, hata sisi ni mali yako Baba wa Mbinguni,Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Muweza wa yote, Alfa na Omega, Yahweh..!Jehovah..!Baba wa upendo, Baba wa Amani,wewe ni Mwanzo na wewe ni mwisho..
Asante kwa ulinzi wako Baba umetulinda usiku mzima na kutuamsha tena, Umetupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwamba  sisi ni wema sana au wazuri sana.. hapana ni kwa Neema/Rehema zako tuu..
Tunakuja mbele zako Baba wa Mbinguni na tunajiachilia mikononi mwako tukijinyenyekeza na kuomba Mfalme wa Amani..
Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Nasi tunaomba  utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Utuokoe na yule mwovu na kazi zake Baba wa mbinguni ututakase Miili yetu na Akili zetu, Utufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Yahweh.. tunaiweka siku hii mikononi mwako tunaomba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo, Vyombo vya usafiri, tuingiapo/tutokapo,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..Ukabariki vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Jehovah.. ukavitakase..

Baba ukabariki ridhi zetu ziingiazo/zitokazo zikawe baraka na tuweze kuwabariki wengine..
Tazama wenye Shida/Tabu wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali, wagonjwa wafiwa ukawe mfariji wao, waliokatika vifungo mbalimbali.. Baba wa mbinguni ukawaguse na mkono wako wenye nguvu, ukawaponye na kuwaokoa, wakapate kupona kimwili na kiroho pia..ukuu wako ukaonekane...

Baba wa Mbinguni utufungulie njia na kutuongoza, tukapate kutambua na kujitambua, kwa kila mmoja ukamuonyeshe na akatambue kazi yake uliyo mpa,ili tusipoteze muda kwa kufuata njia zisizo zetu,kama ni biashara, kama kuhudumia watu, kama ni mwalimu, kama ni kilimo na kila mmoja akatumie vyema karama yake na tukawe chombo chema tukatumike sawasawa na mapenzi yako.kwenye kila kazi tuzifanyazo Mungu ukaonekane kwa matendo na mwenendo wetu..


Wakili Mwema wa zawadi za Mungu


Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na kukesha ili muweze kusali. Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi. Muwe na ukarimu nyinyi kwa nyinyi bila kunung'unika. Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine kama wakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu. Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumikia anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina.

Tunayaweka haya yote mikononi mwako, kwakuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu hata milele..
Amina..!
Asanteni wote mnaopita hapa..Mungu akaonekane kwenye maisha yenu, na msipungukiwe katika mahitaji yenu, mpate sawasawa na Mapenzi ya Mungu.
Nawapenda.

Madhabahu ya kufukizia ubani

(Kut 37:25-28)

1“Utatengeneza madhabahu kwa mbao za mjohoro ili pawe mahali pa kufukizia ubani. 2Madhabahu hiyo iwe ya mraba, urefu na upana wake sentimita 45, na kimo chake sentimita 90. Pembe zake za juu zitatokeza zote zikiwa kitu kimoja na madhabahu yenyewe. 3Yote utaipaka dhahabu safi: Upande wake wa juu, pande zake zote za ubavuni na pembe zake; pia utaizungushia ukingo wa dhahabu. 4Utaitengenezea pete mbili za dhahabu na kuzitia chini ya ukingo wake kwenye pande mbili zinazokabiliana; hizo pete zitatumiwa kushikilia mipiko wakati wa kuibeba. 5Mipiko hiyo iwe ya mjohoro na ipakwe dhahabu. 6Madhabahu hiyo iwekwe mbele ya pazia kando ya sanduku la maamuzi, mbele ya kiti cha huruma ambapo nitakutana nawe. 7Kila siku Aroni anapoingia kuzitayarisha taa zilizopo hapo, atafukiza ubani wenye harufu nzuri juu ya madhabahu hiyo. 8Tena atafukiza ubani wakati wa jioni anapowasha taa. Tambiko hii ya ubani itatolewa daima bila kukatizwa katika vizazi vyenu vyote. 9Kwenye madhabahu hiyo, kamwe msifukize ubani usio mtakatifu, wala msitoe sadaka ya kuteketezwa, wala sadaka ya nafaka, wala kumimina juu yake sadaka ya kinywaji. 10Aroni hana budi kufanya upatanisho juu ya pembe za madhabahu hiyo mara moja kwa mwaka. Ataifanyia upatanisho kwa damu ya tambiko ya kuondolea dhambi mara moja kila mwaka katika vizazi vyenu vyote maana madhabahu hiyo ni takatifu kabisa kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.”


Zaka za hema la mkutano

11Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 12“Kila utakapowahesabu Waisraeli, kila mmoja atalipa fidia kwa ajili ya nafsi yake mbele yangu ili pasiwe na maradhi mabaya miongoni mwao wakati wa kuhesabiwa. 13Taz Kut 38:25-26; Mat 17:24 Kila mmoja atakayehesabiwa ni lazima alipe kiasi cha fedha kulingana na vipimo vya hema la mkutano. Hii ni sadaka yake atakayonitolea. 14Kila mmoja atakayehesabiwa, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, atanitolea tambiko hiyo. 15Tajiri asitoe zaidi wala maskini asitoe chini ya nusu ya kiasi hicho cha fedha wakati mnaponitolea sadaka hiyo ili kufanya upatanisho. 16Wewe utaipokea fedha hiyo ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli, nawe utaitumia kwa shughuli za kazi za hema takatifu, nayo iwe ni ukumbusho wa Waisraeli mbele yangu, fidia ya maisha yenu.”

Birika la shaba

17Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 18Taz Kut 38:8 “Utatengeneza birika la shaba la kutawadhia lenye tako la shaba, uliweke katikati ya hema la mkutano na madhabahu, na kutia maji ndani yake. 19Aroni na wanawe watatumia maji hayo kunawia mikono na miguu, 20kabla ya kuingia kwenye hema la mkutano au kukaribia madhabahu ili kunitolea tambiko mimi Mwenyezi-Mungu, tambiko zitolewazo kwa moto; watafanya hivyo wasije wakafa. 21Ni lazima wanawe mikono na miguu yao wasije wakafa. Hii itakuwa ni kanuni kwao daima, tangu Aroni na uzao wake, vizazi hata vizazi.”

Mafuta ya kupaka

22 Taz Kut 37:29 Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 23“Utachukua viungo bora kabisa kama vifuatavyo: Manemane ya maji kilo sita, mdalasini wenye harufu nzuri kilo tatu, miwa yenye harufu nzuri kilo tatu, 24na aina nyingine ya mdalasini kilo 6 – vipimo hivyo vyote viwe kufuatana na vipimo vya hema takatifu; chukua pia lita 4 za mafuta. 25Kutokana na viungo hivyo utatengeneza mafuta matakatifu uyachanganye kama afanyavyo fundi wa manukato; hayo yatatumika kuweka vitu wakfu. 26Kisha utalimiminia mafuta hayo hema la mkutano, na sanduku la maamuzi; 27meza na vyombo vyake vyote; kinara cha taa na vyombo vyake, madhabahu ya kufukizia ubani, 28madhabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika na tako lake. 29Utaviweka wakfu, ili viwe vitakatifu kabisa. Chochote kitakachovigusa vifaa hivyo, kitakuwa kitakatifu. 30Kisha mpake mafuta Aroni na wanawe na kuwaweka wakfu ili wanitumikie kama makuhani. 31Waambie Waisraeli kwamba haya yatakuwa mafuta yangu matakatifu ya kupaka katika vizazi vyenu vyote. 32Mafuta haya kamwe yasimiminiwe mtu yeyote wa kawaida, wala yasitengenezwe mafuta mengine ya aina hii; haya ni mafuta matakatifu na ni lazima yawe daima matakatifu kwenu. 33Yeyote atakayetengeneza mafuta kama haya, au kumpaka mtu asiyestahili kupakwa mafuta haya, mtu huyo atatengwa mbali na watu wake.”

Ubani

34Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Utachukua vipimo vinavyolingana vya viungo vitamu vifuatavyo: Utomvu wa natafi, utomvu wa shekelethi, utomvu wa kelbena na ubani safi. 35Utatumia vitu hivyo kutengenezea ubani kama utengenezwavyo na fundi manukato, utiwe chumvi upate kuwa safi na mtakatifu. 36Kisha utasagwa na kufanya unga laini, upate kutumiwa ndani ya hema la mkutano na kulipaka sanduku la agano, mahali nitakapokutana nawe; huo utakuwa ubani mtakatifu kabisa kwenu. 37Kamwe msifanye ubani wa mchanganyiko huo kwa matumizi yenu wenyewe kwani ubani huo utakuwa mtakatifu mbele yangu. 38Yeyote atakayejitengenezea ubani wa aina hiyo na kuutumia kama manukato yake binafsi, atatengwa mbali na watu wake.”
Kutoka30;1-38


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 10 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 29...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu..
Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na Fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako usiku wote na umetuamsha salama..Tunarudisha sifa na Utukufu kwako..
Tunashuka mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..
Tunaomba utusamehe pale tulipoenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..

Nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Ukatuokoe na yule mwovu na kazi zake,Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu,Ukatufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda na tukawe na kiasi..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Yahweh..! Tunaomba ukatubariki katika kazi zetu, Biashara,Masomo na ukabariki kuingia kwetu na kutoka kwetu,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe,vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase..
Baba wa mbinguni tunaomba ukabariki Mji huu na Nchi tunayoishi na utubariki watu wote tunaoishi hapa,ukatuongoze na kutulinda na mabaya yote,Mfalme wa Amani tunaiweka Tanzania mikononi mwako, tunaomba ukaibariki na kuwabariki watu wake popote walipo..
Afrika yote na Dunia nzima ikawe mikononi mwako Jehovah..! Ukawe mtawala mkuu na uwaongoze wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..

Jehovah..! Tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokata tamaa,waliokataliwa,wenyehofu/mashaka,waliokatika vifungo mbalimbali  Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu, ukawafungue na kuwaponya, wakapate tumaini na wasimame tena,wakapone kimwili na kiroho pia..Baba ukaonekane kwenye magumu na mapito yao..

kwako wewe hakuna linaloshindikana.. uponyaji  wa kweli upo nawe, Upendo wa kweli unapatikana kwako, Faraja ya kweli ina wewe,Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Mungu wetu, Baba yetu, Mwokozi wetu, Mlinzi mkuu,Muweza wa yote, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo..
wewe ni Alfa na Omega, wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho..hakuna kama wewe na hatokuwepo..Tumaini la kweli na unatosha Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako Mungu wetu,Tunakusifu na kukushukuru katika yote..Tukiamini na wewe ni Mungu wetu na Mlinzi mkuu..
Amina..!!
Asanteni sana kwa wote mnaotembelea hapa Mungu awabariki na kuwaongoza,msipungukiwe katika mahitaji yenu sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda. 

Maagizo ya kuwaweka wakfu Aroni na wanawe

(Lawi 8:1-36)

1“Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Aroni na wanawe ili kuwaweka wakfu wanitumikie kama makuhani. Utachukua ndama dume na kondoo madume wawili wasio na dosari, 2mikate isiyotiwa chachu, maandazi yasiyotiwa chachu yaliyokandwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyotiwa chachu, lakini iliyopakwa mafuta. Vyote hivi viwe vimetengenezwa kwa unga laini wa ngano. 3Kisha iweke hiyo mikate ndani ya kikapu kimoja na kunitolea wakati mmoja na yule ndama dume na wale kondoo dume wawili.
4“Kisha wapeleke Aroni na wanawe mlangoni pa hema la mkutano na kuwatawadha. 5Kisha utachukua yale mavazi ya kikuhani umvike Aroni: Joho, kanzu, kizibao, kifuko cha kifuani, na kumfunga ule mshipi uliofumwa kwa ustadi. 6Tena utamvika kile kilemba kichwani na kuweka juu ya hicho kilemba ile taji takatifu. 7Baada ya kufanya hivyo, utachukua yale mafuta ya kupaka, ummiminie Aroni kichwani mwake kumweka wakfu.
8“Kisha utawaleta wana wa Aroni na kuwavika vizibao. 9Utawafunga mishipi viunoni na kuwavisha kofia zao. Hivyo ndivyo utakavyowaweka wakfu Aroni na wanawe kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani daima.
10“Kisha utamleta yule ndama dume mbele ya hema la mkutano. Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha ndama huyo 11na kumchinja mbele ya Mwenyezi-Mungu, mlangoni pa hema la mkutano. 12Utachukua kiasi cha damu na kuipaka kwenye pembe za madhabahu kwa kidole chako, na damu yote inayosalia utaimwaga chini ya madhabahu. 13Halafu utatwaa mafuta yote yanayofunika matumbo, sehemu bora ya maini pamoja na figo mbili na mafuta yake, uviteketeze vyote juu ya madhabahu. 14Lakini nyama ya fahali huyo pamoja na ngozi na mavi yake utavichukua na kuviteketeza nje ya kambi yenu. Hii itakuwa sadaka ya kuondoa dhambi.
15“Kisha utamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumwambia Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake. 16Nawe utamchinja na damu yake utairashia madhabahu pande zake zote. 17Halafu utamkata huyo kondoo vipandevipande; utaosha matumbo yake na miguu yake, uviweke vyote pamoja na kichwa na vipande vingine. 18Taz Efe 5:2; Fili 4:18 Kisha utamteketeza kondoo mzima juu ya madhabahu ili kunitolea sadaka ya kuteketezwa; harufu ya sadaka inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Mwenyezi-Mungu.
19“Utamchukua yule kondoo mwingine, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake. 20Nawe utamchinja na kuchukua kiasi cha damu na kumpaka Aroni na wanawe kwenye ncha za masikio yao ya kulia na vidole gumba vya mikono yao ya kulia, na vidole gumba vya miguu yao ya kulia. Damu inayobaki utairashia madhabahu pande zake zote. 21Kisha utachukua kiasi cha damu iliyoko juu ya madhabahu pamoja na yale mafuta ya kupaka umnyunyizie Aroni na mavazi yake, uwanyunyizie pia wanawe na mavazi yao. Aroni na wanawe watakuwa wamewekwa wakfu kwangu pamoja na mavazi yao yote.
22“Kisha utachukua mafuta ya huyo kondoo dume: Mkia wake, mafuta yanayofunika matumbo na sehemu bora ya maini, figo zake mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Kondoo huyo ni kondoo wa kuweka wakfu.) 23Kutoka katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu kilicho mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu, utachukua mkate mmoja na andazi moja lililotiwa mafuta na mkate mwembamba mmoja. 24Vyote hivi utamkabidhi Aroni na wanawe nao wataviinua juu kuwa ishara ya kunitolea tambiko mimi Mwenyezi-Mungu. 25Kisha utavichukua tena kutoka mikononi mwao na kuviteketeza juu ya madhabahu pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri itakayonipendeza mimi Mwenyezi-Mungu. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto.
26“Kisha utachukua kidari cha huyo kondoo wa kumweka wakfu Aroni, na kufanya ishara ya kunitolea mimi Mwenyezi-Mungu. Nacho kitakuwa sehemu yako. 27Kuhani anapowekwa wakfu, kidari na paja la kondoo dume wa kuwekea wakfu vitaletwa na kuwekwa wakfu mbele yangu kwa kufanya ishara ya kunitolea, navyo vitakuwa vya Aroni na wanawe. 28Hivyo Waisraeli daima watachukua sehemu hizo kutoka katika sadaka zao za amani wanazonitolea mimi Mwenyezi-Mungu na kumpa Aroni na wanawe. Hiyo ni sadaka yao kwa Mwenyezi-Mungu.
29“Baada ya kufa kwake Aroni, mavazi yake matakatifu yatakabidhiwa wazawa wake, nao watayavaa siku yao ya kupakwa mafuta na kuwekewa mikono. 30Mwana wa Aroni atakayekuwa kuhani mahali pa baba yake atayavaa mavazi hayo siku saba katika hema la mkutano, ili kuhudumu katika mahali patakatifu.
31“Utachukua nyama ya huyo kondoo wa kuwaweka wakfu na kuichemshia katika mahali patakatifu. 32Kisha utawapa Aroni na wanawe, nao wataila mlangoni pa hema la mkutano pamoja na ile mikate iliyosalia kapuni. 33Watavila vitu hivyo vilivyotumika kuwaweka wakfu na kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho, lakini mtu mwingine asiruhusiwe kuvila kwani ni vitakatifu. 34Kama nyama yoyote au mikate hiyo itasalia mpaka asubuhi yake, basi utaiteketeza kwa moto; isiliwe maana ni kitu kitakatifu.
35“Hivyo ndivyo utakavyowatendea Aroni na wanawe kufuatana na yote yale niliyokuamuru; utawaweka wakfu kwa muda wa siku saba, 36na kila siku utatoa fahali awe sadaka ya kuondolea dhambi ili kufanya upatanisho, na kwa kufanya hivyo utaitakasa madhabahu; kisha utaimiminia mafuta ili kuiweka wakfu. 37Kwa siku saba utaifanyia madhabahu upatanisho na kuiweka wakfu. Baada ya hayo, madhabahu itakuwa takatifu kabisa na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.

Tambiko za kila siku

38“Kila siku, wakati wote ujao, utatolea sadaka juu ya madhabahu: Wanakondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja. 39Mwanakondoo mmoja utamtoa sadaka asubuhi na mwingine jioni. 40Pamoja na mwanakondoo wa kwanza, utatoa kilo moja ya unga laini uliochanganywa na lita moja ya mafuta safi, na lita moja ya divai kama sadaka ya kinywaji. 41Hali kadhalika na yule mwanakondoo mwingine wa jioni utamtolea tambiko pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji kama ulivyofanya asubuhi; harufu ya tambiko hiyo inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Mwenyezi-Mungu. 42Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa daima, kizazi hata kizazi, mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu, mbele ya mlango wa hema la mkutano ambapo mimi nitakutana nanyi na kuongea nanyi. 43Hapo ndipo nitakapokutana na Waisraeli na utukufu wangu utapafanya pawe patakatifu. 44Hema la mkutano na madhabahu nitavifanya vitakatifu; vilevile Aroni na wanawe nitawaweka wakfu ili wanitumikie kama makuhani. 45Nitaishi kati ya Waisraeli, nami nitakuwa Mungu wao. 46Hapo ndipo watakapotambua kuwa mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, niliyewaleta kutoka nchi ya Misri, ili niishi kati yao. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.
Kutoka29;1-46

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.