Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Friday 12 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 31...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa mema yote aliyotutendea na anayoendelea kututendea..
Tunakushukuru Mungu wetu  kwa wema na fadhili zako, umetulinda usiku kucha na kutuamsha salama, Umetuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii..
Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..Mungu wetu, Nuru na mwanga wetu,Jehova nissi..!, Jehovah shammah..!, Jehovah rapha..!, Jehovah Shalom..!,Jehovah rohi..!,Jehovah jireh..!Mungu unayeponya, Mungu unayetenda, Mungu unayejibu, Mungu unayebariki na wewe ni Mungu wa Rehema..

Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe, kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua.
Baba nasi ukatupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea.

ukatupe macho ya rohoni tupate kutambua/kujitambua..tukawe na 
  hekima,busara,utuwema,upendo wa kweli na upole kiasi..
tuweze kuachilia na kuchukuliana..
Utuepeshe na chuki,hasira na kisasi, makwazo na kukwaza wengine..

Kisha, Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Haiwezekani kabisa kusitokee vikwazo vinavyosababisha dhambi; lakini ole wake mtu yule atakayevisababisha. Ingekuwa afadhali kwake kufungiwa shingoni jiwe kubwa la kusagia na kutoswa baharini, kuliko kumkwaza mmoja wa wadogo hawa. Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe. Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema, ‘Nimetubu,’ lazima umsamehe.”
Roho Mtakatifu akatuongoze na tukawe na kiasi..

Baba wa Mbinguni tunaiweka siku hii na maisha yetu mikononi mwako, tunaomba ukaibariki na kutubariki katika yote tunayoenda kufanya/kutenda, ukatuongoze na kutulinda, ukatutakase Miili yetu na Akili zetu na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba wa mbinguni ukavitakase kwa Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti.. Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Kwa imani na tumaini la kweli tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Sifa na utukufu ni wako Baba wa Mbinguni,Tunashukuru na kuku abudu siku zote za maisha yetu,,Ehh Mungu utuongoze..


Msifuni Mwenyezi-Mungu! Umsifu Mwenyezi-Mungu, ee nafsi yangu! Nitamsifu Mwenyezi-Mungu maisha yangu yote; nitamwimbia Mungu wangu muda wote niishipo. Msiwategemee wakuu wa dunia; hao ni binadamu tu, hawawezi kuokoa. Binadamu akitoa pumzi yake ya mwisho, anarudi mavumbini alimotoka; na hapo mipango yake yote hutoweka. Heri mtu anayesaidiwa na Mungu wa Yakobo, mtu aliyeweka tumaini lake kwa Mwenyezi-Mungu, Mungu wake, aliyeumba mbingu na dunia, bahari na vyote vilivyomo. Yeye hushika ahadi yake milele. Yeye huwapatia wanaoonewa haki zao, huwapa wenye njaa chakula. Mwenyezi-Mungu huwapa wafungwa uhuru, huwafungua macho vipofu. Mwenyezi-Mungu huwainua waliokandamizwa; huwapenda watu walio waadilifu. Mwenyezi-Mungu huwalinda wageni, huwategemeza wajane na yatima; lakini huipotosha njia ya waovu. Mwenyezi-Mungu atawala milele, Mungu wako, ee Siyoni, ni mfalme vizazi vyote! Msifuni Mwenyezi-Mungu!
                                           Amina..
Asanteni sana wote mnaotembelea hapa Mungu akawabariki katika yote..muwe salama Rohoni
Nawapenda.



Mafundi wa kutayarisha hema la mkutano

(Kut 35:30–36:1)

1Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 2“Mimi nimemteua Bezaleli, mwana wa Uri, mjukuu wa Huri, wa kabila la Yuda 3na kumjaza roho wangu. Nimempatia uzoefu na akili, maarifa na ufundi, 4ili abuni kazi za usanii na kufanya kazi za kufua dhahabu, fedha na shaba. 5Nimempatia ujuzi wa kuchonga mawe ya kupambia, kuchonga mbao, na ujuzi wa kila aina ya ufundi. 6Vilevile nimemteua Oholiabu mwana wa Ahisamaki, wa kabila la Dani, afanye kazi pamoja naye. Hali kadhalika nimewapa uwezo mkubwa watu wengine kwa ajili ya kazi mbalimbali, ili watengeneze vifaa vyote nilivyoagiza vifanywe: 7Hema la mkutano, sanduku la ushuhuda na kiti cha ushuhuda juu yake, pamoja na vifaa vyake vyote; 8meza na vyombo vyake, kinara safi cha taa na vyombo vyake, madhabahu ya kufukizia ubani, 9madhabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika la maji pamoja na tako lake, 10mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na wanawe ambao watafanya huduma ya ukuhani, 11mafuta ya kupaka na ubani wenye harufu nzuri kwa ajili ya mahali patakatifu. Vitu hivyo vyote vitatengenezwa kulingana kabisa na jinsi nilivyokuamuru.”

Siku ya kupumzika

12Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 13“Waambie Waisraeli hivi: Nyinyi mtaadhimisha Sabato zangu, kwa sababu hizo ni ishara kati yenu na mimi kwa vizazi vyote kwamba mimi ndimi ninayewatakasa. 14Mtaiadhimisha Sabato, nayo itakuwa kwenu siku takatifu. Yeyote atakayeitia unajisi siku hiyo lazima auawe. Na mtu atakayefanya kazi yoyote siku hiyo atatengwa mbali na watu wake. 15Taz Kut 20:8-11; 23:12; 34:21; 35:21; Lawi 23:3; Kumb 5:12-14 Mtafanya kazi zenu kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba ni siku rasmi ya mapumziko, ni siku yangu takatifu. Mtu yeyote atakayefanya kazi yoyote siku hiyo lazima atauawa. 16Kwa hiyo Waisraeli wataiadhimisha siku ya Sabato katika vizazi vyao vyote kama ishara ya agano la milele. 17Taz Kut 20:11 Jambo hili litakuwa ishara ya kudumu kati ya Waisraeli na mimi, maana mimi Mwenyezi-Mungu nilifanya mbingu na dunia kwa muda wa siku sita, lakini siku ya saba niliacha kufanya kazi, nikapumzika.”
18Mwenyezi-Mungu alipomaliza kuongea na Mose mlimani Sinai, alimpatia Mose vile vibao viwili vya mawe ambavyo yeye Mungu aliviandika zile amri kwa kidole chake mwenyewe.

Kutoka31;1-18

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 11 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 30...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu yeye atosha..
Mungu wetu, Baba yetu,Muumba wetu,Muumba Mbingu na Nchi, Muumba wa vyote, Vyote ni mali yako, hata sisi ni mali yako Baba wa Mbinguni,Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo, Muweza wa yote, Alfa na Omega, Yahweh..!Jehovah..!Baba wa upendo, Baba wa Amani,wewe ni Mwanzo na wewe ni mwisho..
Asante kwa ulinzi wako Baba umetulinda usiku mzima na kutuamsha tena, Umetupa Kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Si kwamba  sisi ni wema sana au wazuri sana.. hapana ni kwa Neema/Rehema zako tuu..
Tunakuja mbele zako Baba wa Mbinguni na tunajiachilia mikononi mwako tukijinyenyekeza na kuomba Mfalme wa Amani..
Utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..
Nasi tunaomba  utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Utuokoe na yule mwovu na kazi zake Baba wa mbinguni ututakase Miili yetu na Akili zetu, Utufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti Yeye aliteseka ili sisi tupate kupona..
Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..


Yahweh.. tunaiweka siku hii mikononi mwako tunaomba ukabariki kazi zetu,Biashara,Masomo, Vyombo vya usafiri, tuingiapo/tutokapo,tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..Ukabariki vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Jehovah.. ukavitakase..

Baba ukabariki ridhi zetu ziingiazo/zitokazo zikawe baraka na tuweze kuwabariki wengine..
Tazama wenye Shida/Tabu wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali, wagonjwa wafiwa ukawe mfariji wao, waliokatika vifungo mbalimbali.. Baba wa mbinguni ukawaguse na mkono wako wenye nguvu, ukawaponye na kuwaokoa, wakapate kupona kimwili na kiroho pia..ukuu wako ukaonekane...

Baba wa Mbinguni utufungulie njia na kutuongoza, tukapate kutambua na kujitambua, kwa kila mmoja ukamuonyeshe na akatambue kazi yake uliyo mpa,ili tusipoteze muda kwa kufuata njia zisizo zetu,kama ni biashara, kama kuhudumia watu, kama ni mwalimu, kama ni kilimo na kila mmoja akatumie vyema karama yake na tukawe chombo chema tukatumike sawasawa na mapenzi yako.kwenye kila kazi tuzifanyazo Mungu ukaonekane kwa matendo na mwenendo wetu..


Wakili Mwema wa zawadi za Mungu


Mwisho wa vitu vyote umekaribia. Kwa hiyo mnapaswa kuwa na utaratibu na kukesha ili muweze kusali. Zaidi ya yote pendaneni kwa moyo wote, maana upendo hufunika dhambi nyingi. Muwe na ukarimu nyinyi kwa nyinyi bila kunung'unika. Kila mmoja anapaswa kutumia kipaji alichojaliwa na Mungu kwa faida ya wengine kama wakili mwema wa zawadi mbalimbali za Mungu. Anayesema kitu, maneno yake na yawe kama maneno ya Mungu; anayetumikia anapaswa kutumikia kwa nguvu anayojaliwa na Mungu, ili katika mambo yote, Mungu atukuzwe kwa njia ya Yesu Kristo ambaye utukufu na nguvu ni vyake milele na milele! Amina.

Tunayaweka haya yote mikononi mwako, kwakuwa ufalme ni wako na nguvu na utukufu hata milele..
Amina..!
Asanteni wote mnaopita hapa..Mungu akaonekane kwenye maisha yenu, na msipungukiwe katika mahitaji yenu, mpate sawasawa na Mapenzi ya Mungu.
Nawapenda.

Madhabahu ya kufukizia ubani

(Kut 37:25-28)

1“Utatengeneza madhabahu kwa mbao za mjohoro ili pawe mahali pa kufukizia ubani. 2Madhabahu hiyo iwe ya mraba, urefu na upana wake sentimita 45, na kimo chake sentimita 90. Pembe zake za juu zitatokeza zote zikiwa kitu kimoja na madhabahu yenyewe. 3Yote utaipaka dhahabu safi: Upande wake wa juu, pande zake zote za ubavuni na pembe zake; pia utaizungushia ukingo wa dhahabu. 4Utaitengenezea pete mbili za dhahabu na kuzitia chini ya ukingo wake kwenye pande mbili zinazokabiliana; hizo pete zitatumiwa kushikilia mipiko wakati wa kuibeba. 5Mipiko hiyo iwe ya mjohoro na ipakwe dhahabu. 6Madhabahu hiyo iwekwe mbele ya pazia kando ya sanduku la maamuzi, mbele ya kiti cha huruma ambapo nitakutana nawe. 7Kila siku Aroni anapoingia kuzitayarisha taa zilizopo hapo, atafukiza ubani wenye harufu nzuri juu ya madhabahu hiyo. 8Tena atafukiza ubani wakati wa jioni anapowasha taa. Tambiko hii ya ubani itatolewa daima bila kukatizwa katika vizazi vyenu vyote. 9Kwenye madhabahu hiyo, kamwe msifukize ubani usio mtakatifu, wala msitoe sadaka ya kuteketezwa, wala sadaka ya nafaka, wala kumimina juu yake sadaka ya kinywaji. 10Aroni hana budi kufanya upatanisho juu ya pembe za madhabahu hiyo mara moja kwa mwaka. Ataifanyia upatanisho kwa damu ya tambiko ya kuondolea dhambi mara moja kila mwaka katika vizazi vyenu vyote maana madhabahu hiyo ni takatifu kabisa kwangu mimi Mwenyezi-Mungu.”


Zaka za hema la mkutano

11Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 12“Kila utakapowahesabu Waisraeli, kila mmoja atalipa fidia kwa ajili ya nafsi yake mbele yangu ili pasiwe na maradhi mabaya miongoni mwao wakati wa kuhesabiwa. 13Taz Kut 38:25-26; Mat 17:24 Kila mmoja atakayehesabiwa ni lazima alipe kiasi cha fedha kulingana na vipimo vya hema la mkutano. Hii ni sadaka yake atakayonitolea. 14Kila mmoja atakayehesabiwa, tangu umri wa miaka ishirini na zaidi, atanitolea tambiko hiyo. 15Tajiri asitoe zaidi wala maskini asitoe chini ya nusu ya kiasi hicho cha fedha wakati mnaponitolea sadaka hiyo ili kufanya upatanisho. 16Wewe utaipokea fedha hiyo ya upatanisho kutoka kwa Waisraeli, nawe utaitumia kwa shughuli za kazi za hema takatifu, nayo iwe ni ukumbusho wa Waisraeli mbele yangu, fidia ya maisha yenu.”

Birika la shaba

17Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 18Taz Kut 38:8 “Utatengeneza birika la shaba la kutawadhia lenye tako la shaba, uliweke katikati ya hema la mkutano na madhabahu, na kutia maji ndani yake. 19Aroni na wanawe watatumia maji hayo kunawia mikono na miguu, 20kabla ya kuingia kwenye hema la mkutano au kukaribia madhabahu ili kunitolea tambiko mimi Mwenyezi-Mungu, tambiko zitolewazo kwa moto; watafanya hivyo wasije wakafa. 21Ni lazima wanawe mikono na miguu yao wasije wakafa. Hii itakuwa ni kanuni kwao daima, tangu Aroni na uzao wake, vizazi hata vizazi.”

Mafuta ya kupaka

22 Taz Kut 37:29 Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, 23“Utachukua viungo bora kabisa kama vifuatavyo: Manemane ya maji kilo sita, mdalasini wenye harufu nzuri kilo tatu, miwa yenye harufu nzuri kilo tatu, 24na aina nyingine ya mdalasini kilo 6 – vipimo hivyo vyote viwe kufuatana na vipimo vya hema takatifu; chukua pia lita 4 za mafuta. 25Kutokana na viungo hivyo utatengeneza mafuta matakatifu uyachanganye kama afanyavyo fundi wa manukato; hayo yatatumika kuweka vitu wakfu. 26Kisha utalimiminia mafuta hayo hema la mkutano, na sanduku la maamuzi; 27meza na vyombo vyake vyote; kinara cha taa na vyombo vyake, madhabahu ya kufukizia ubani, 28madhabahu ya sadaka za kuteketezwa na vyombo vyake vyote, birika na tako lake. 29Utaviweka wakfu, ili viwe vitakatifu kabisa. Chochote kitakachovigusa vifaa hivyo, kitakuwa kitakatifu. 30Kisha mpake mafuta Aroni na wanawe na kuwaweka wakfu ili wanitumikie kama makuhani. 31Waambie Waisraeli kwamba haya yatakuwa mafuta yangu matakatifu ya kupaka katika vizazi vyenu vyote. 32Mafuta haya kamwe yasimiminiwe mtu yeyote wa kawaida, wala yasitengenezwe mafuta mengine ya aina hii; haya ni mafuta matakatifu na ni lazima yawe daima matakatifu kwenu. 33Yeyote atakayetengeneza mafuta kama haya, au kumpaka mtu asiyestahili kupakwa mafuta haya, mtu huyo atatengwa mbali na watu wake.”

Ubani

34Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose, “Utachukua vipimo vinavyolingana vya viungo vitamu vifuatavyo: Utomvu wa natafi, utomvu wa shekelethi, utomvu wa kelbena na ubani safi. 35Utatumia vitu hivyo kutengenezea ubani kama utengenezwavyo na fundi manukato, utiwe chumvi upate kuwa safi na mtakatifu. 36Kisha utasagwa na kufanya unga laini, upate kutumiwa ndani ya hema la mkutano na kulipaka sanduku la agano, mahali nitakapokutana nawe; huo utakuwa ubani mtakatifu kabisa kwenu. 37Kamwe msifanye ubani wa mchanganyiko huo kwa matumizi yenu wenyewe kwani ubani huo utakuwa mtakatifu mbele yangu. 38Yeyote atakayejitengenezea ubani wa aina hiyo na kuutumia kama manukato yake binafsi, atatengwa mbali na watu wake.”
Kutoka30;1-38


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Wednesday 10 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 29...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu wetu..
Asante Baba wa Mbinguni kwa wema na Fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako usiku wote na umetuamsha salama..Tunarudisha sifa na Utukufu kwako..
Tunashuka mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..
Tunaomba utusamehe pale tulipoenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua/kutojua..

Nasi utupe neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..
Ukatuokoe na yule mwovu na kazi zake,Ukatutakase Miili yetu na Akili zetu,Ukatufunike na Damu ya mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Roho Mtakatifu akatuongoze kwenye kunena/kutenda na tukawe na kiasi..
Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..

Yahweh..! Tunaomba ukatubariki katika kazi zetu, Biashara,Masomo na ukabariki kuingia kwetu na kutoka kwetu,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe,vilaji/vinywaji na vyote tunavyoenda kugusa/kutumia Baba ukavitakase..
Baba wa mbinguni tunaomba ukabariki Mji huu na Nchi tunayoishi na utubariki watu wote tunaoishi hapa,ukatuongoze na kutulinda na mabaya yote,Mfalme wa Amani tunaiweka Tanzania mikononi mwako, tunaomba ukaibariki na kuwabariki watu wake popote walipo..
Afrika yote na Dunia nzima ikawe mikononi mwako Jehovah..! Ukawe mtawala mkuu na uwaongoze wanaotuongoza wakatuongoze katika haki na kweli..

Jehovah..! Tazama wenye shida/tabu,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokata tamaa,waliokataliwa,wenyehofu/mashaka,waliokatika vifungo mbalimbali  Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu, ukawafungue na kuwaponya, wakapate tumaini na wasimame tena,wakapone kimwili na kiroho pia..Baba ukaonekane kwenye magumu na mapito yao..

kwako wewe hakuna linaloshindikana.. uponyaji  wa kweli upo nawe, Upendo wa kweli unapatikana kwako, Faraja ya kweli ina wewe,Sifa na Utukufu tunakurudishia wewe Mungu wetu, Baba yetu, Mwokozi wetu, Mlinzi mkuu,Muweza wa yote, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo..
wewe ni Alfa na Omega, wewe ni mwanzo na wewe ni mwisho..hakuna kama wewe na hatokuwepo..Tumaini la kweli na unatosha Mungu wetu..
Tunayaweka haya yote mikononi mwako Mungu wetu,Tunakusifu na kukushukuru katika yote..Tukiamini na wewe ni Mungu wetu na Mlinzi mkuu..
Amina..!!
Asanteni sana kwa wote mnaotembelea hapa Mungu awabariki na kuwaongoza,msipungukiwe katika mahitaji yenu sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda. 

Maagizo ya kuwaweka wakfu Aroni na wanawe

(Lawi 8:1-36)

1“Haya ndiyo mambo utakayowafanyia Aroni na wanawe ili kuwaweka wakfu wanitumikie kama makuhani. Utachukua ndama dume na kondoo madume wawili wasio na dosari, 2mikate isiyotiwa chachu, maandazi yasiyotiwa chachu yaliyokandwa kwa mafuta, na mikate myembamba isiyotiwa chachu, lakini iliyopakwa mafuta. Vyote hivi viwe vimetengenezwa kwa unga laini wa ngano. 3Kisha iweke hiyo mikate ndani ya kikapu kimoja na kunitolea wakati mmoja na yule ndama dume na wale kondoo dume wawili.
4“Kisha wapeleke Aroni na wanawe mlangoni pa hema la mkutano na kuwatawadha. 5Kisha utachukua yale mavazi ya kikuhani umvike Aroni: Joho, kanzu, kizibao, kifuko cha kifuani, na kumfunga ule mshipi uliofumwa kwa ustadi. 6Tena utamvika kile kilemba kichwani na kuweka juu ya hicho kilemba ile taji takatifu. 7Baada ya kufanya hivyo, utachukua yale mafuta ya kupaka, ummiminie Aroni kichwani mwake kumweka wakfu.
8“Kisha utawaleta wana wa Aroni na kuwavika vizibao. 9Utawafunga mishipi viunoni na kuwavisha kofia zao. Hivyo ndivyo utakavyowaweka wakfu Aroni na wanawe kuwa makuhani. Hao watakuwa makuhani daima.
10“Kisha utamleta yule ndama dume mbele ya hema la mkutano. Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa cha ndama huyo 11na kumchinja mbele ya Mwenyezi-Mungu, mlangoni pa hema la mkutano. 12Utachukua kiasi cha damu na kuipaka kwenye pembe za madhabahu kwa kidole chako, na damu yote inayosalia utaimwaga chini ya madhabahu. 13Halafu utatwaa mafuta yote yanayofunika matumbo, sehemu bora ya maini pamoja na figo mbili na mafuta yake, uviteketeze vyote juu ya madhabahu. 14Lakini nyama ya fahali huyo pamoja na ngozi na mavi yake utavichukua na kuviteketeza nje ya kambi yenu. Hii itakuwa sadaka ya kuondoa dhambi.
15“Kisha utamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumwambia Aroni na wanawe waweke mikono yao juu ya kichwa chake. 16Nawe utamchinja na damu yake utairashia madhabahu pande zake zote. 17Halafu utamkata huyo kondoo vipandevipande; utaosha matumbo yake na miguu yake, uviweke vyote pamoja na kichwa na vipande vingine. 18Taz Efe 5:2; Fili 4:18 Kisha utamteketeza kondoo mzima juu ya madhabahu ili kunitolea sadaka ya kuteketezwa; harufu ya sadaka inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Mwenyezi-Mungu.
19“Utamchukua yule kondoo mwingine, naye Aroni na wanawe wataweka mikono yao juu ya kichwa chake. 20Nawe utamchinja na kuchukua kiasi cha damu na kumpaka Aroni na wanawe kwenye ncha za masikio yao ya kulia na vidole gumba vya mikono yao ya kulia, na vidole gumba vya miguu yao ya kulia. Damu inayobaki utairashia madhabahu pande zake zote. 21Kisha utachukua kiasi cha damu iliyoko juu ya madhabahu pamoja na yale mafuta ya kupaka umnyunyizie Aroni na mavazi yake, uwanyunyizie pia wanawe na mavazi yao. Aroni na wanawe watakuwa wamewekwa wakfu kwangu pamoja na mavazi yao yote.
22“Kisha utachukua mafuta ya huyo kondoo dume: Mkia wake, mafuta yanayofunika matumbo na sehemu bora ya maini, figo zake mbili na mafuta yake, pamoja na paja la kulia. (Kondoo huyo ni kondoo wa kuweka wakfu.) 23Kutoka katika kile kikapu cha mikate isiyotiwa chachu kilicho mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu, utachukua mkate mmoja na andazi moja lililotiwa mafuta na mkate mwembamba mmoja. 24Vyote hivi utamkabidhi Aroni na wanawe nao wataviinua juu kuwa ishara ya kunitolea tambiko mimi Mwenyezi-Mungu. 25Kisha utavichukua tena kutoka mikononi mwao na kuviteketeza juu ya madhabahu pamoja na ile sadaka ya kuteketezwa, viwe harufu nzuri itakayonipendeza mimi Mwenyezi-Mungu. Hiyo ni sadaka inayotolewa kwa moto.
26“Kisha utachukua kidari cha huyo kondoo wa kumweka wakfu Aroni, na kufanya ishara ya kunitolea mimi Mwenyezi-Mungu. Nacho kitakuwa sehemu yako. 27Kuhani anapowekwa wakfu, kidari na paja la kondoo dume wa kuwekea wakfu vitaletwa na kuwekwa wakfu mbele yangu kwa kufanya ishara ya kunitolea, navyo vitakuwa vya Aroni na wanawe. 28Hivyo Waisraeli daima watachukua sehemu hizo kutoka katika sadaka zao za amani wanazonitolea mimi Mwenyezi-Mungu na kumpa Aroni na wanawe. Hiyo ni sadaka yao kwa Mwenyezi-Mungu.
29“Baada ya kufa kwake Aroni, mavazi yake matakatifu yatakabidhiwa wazawa wake, nao watayavaa siku yao ya kupakwa mafuta na kuwekewa mikono. 30Mwana wa Aroni atakayekuwa kuhani mahali pa baba yake atayavaa mavazi hayo siku saba katika hema la mkutano, ili kuhudumu katika mahali patakatifu.
31“Utachukua nyama ya huyo kondoo wa kuwaweka wakfu na kuichemshia katika mahali patakatifu. 32Kisha utawapa Aroni na wanawe, nao wataila mlangoni pa hema la mkutano pamoja na ile mikate iliyosalia kapuni. 33Watavila vitu hivyo vilivyotumika kuwaweka wakfu na kwa ajili ya kuwafanyia upatanisho, lakini mtu mwingine asiruhusiwe kuvila kwani ni vitakatifu. 34Kama nyama yoyote au mikate hiyo itasalia mpaka asubuhi yake, basi utaiteketeza kwa moto; isiliwe maana ni kitu kitakatifu.
35“Hivyo ndivyo utakavyowatendea Aroni na wanawe kufuatana na yote yale niliyokuamuru; utawaweka wakfu kwa muda wa siku saba, 36na kila siku utatoa fahali awe sadaka ya kuondolea dhambi ili kufanya upatanisho, na kwa kufanya hivyo utaitakasa madhabahu; kisha utaimiminia mafuta ili kuiweka wakfu. 37Kwa siku saba utaifanyia madhabahu upatanisho na kuiweka wakfu. Baada ya hayo, madhabahu itakuwa takatifu kabisa na chochote kitakachoigusa kitakuwa kitakatifu.

Tambiko za kila siku

38“Kila siku, wakati wote ujao, utatolea sadaka juu ya madhabahu: Wanakondoo wawili wenye umri wa mwaka mmoja. 39Mwanakondoo mmoja utamtoa sadaka asubuhi na mwingine jioni. 40Pamoja na mwanakondoo wa kwanza, utatoa kilo moja ya unga laini uliochanganywa na lita moja ya mafuta safi, na lita moja ya divai kama sadaka ya kinywaji. 41Hali kadhalika na yule mwanakondoo mwingine wa jioni utamtolea tambiko pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji kama ulivyofanya asubuhi; harufu ya tambiko hiyo inayotolewa kwa moto itanipendeza mimi Mwenyezi-Mungu. 42Sadaka hii ya kuteketezwa itatolewa daima, kizazi hata kizazi, mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu, mbele ya mlango wa hema la mkutano ambapo mimi nitakutana nanyi na kuongea nanyi. 43Hapo ndipo nitakapokutana na Waisraeli na utukufu wangu utapafanya pawe patakatifu. 44Hema la mkutano na madhabahu nitavifanya vitakatifu; vilevile Aroni na wanawe nitawaweka wakfu ili wanitumikie kama makuhani. 45Nitaishi kati ya Waisraeli, nami nitakuwa Mungu wao. 46Hapo ndipo watakapotambua kuwa mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao, niliyewaleta kutoka nchi ya Misri, ili niishi kati yao. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wao.
Kutoka29;1-46

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Tuesday 9 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 28...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu katika yote..
Mtakatifu.. Mtakatifu..Mtakatifu...! Baba wa Mbinguni, Tunasema asante kwa wema na fadhili zako, Asante kwakutulinda usiku mzima na kutuamsha tena na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..

Tunakuja mbele zako Baba wa Mbinguni  tukijinyenyekeza na tukijiachilia mikononi mwako Mfalme wa Amani..
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe Baba wa mbinguni, kwakuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua, kutojua..
Nasi tunaomba utupe Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..

Yahweh..! Tunaomba utuokoe na yule mwovu na kazi zake..
Ututakase Miili yetu na Akili zetu, utufunike na Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Roho Mtakatifu akatuongoze  katika yote tupate kutambua na kujitambua Baba na tukawe na kiasi ..

Jehovah..! Tunaomba ukaibariki siku hii na ukatubariki katika Kazi zetu,Biashara,Masomo,Vilaji/vinywaji,Tuingiapo/Tutokapo,Vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe..

Baba wa Mbinguni tunawaweka watoto wetu wanaofanya mitihani na wanaojiandaa na mitihani.. ukawaongoze vyema na kuwalinda wapate kuelewa na kukumbuka yote waliyofundishwa..ukawaondoe hofu na mashaka..
Mfalme wa Amani Tazama Yatima na wajane,wenye shida/Tabu, wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,wanaopitia magumu/majaribu, waliokwenye vifungo mbalimbali Baba wa Mbinguni tunaomba ukawaguse na mkono wako wako wenye nguvu, ukawaponye na kuwaokoa, ukawafunike na Damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, Wapate kupona kimwili na kiroho pia..



Baba wa Mbinguni ukawafariji wote wanaopitia wakati mgumu wa kuondokewa na wapendwa wao,Mungu wetu  ukawaguse na kuwafariji ukawape nguvu na uvumilivu katika wakati huu mgumu kwao, ukaonekane Yahweh.. na ukawaponye rohoni na wakawe na matumaini tena..wapitishe salama katika jaribu hili Baba kwani kwa binadamu ni kipindi kigumu mno..lakini kwa Neema yako na watavuka salama..

Mwenyezi-Mungu akujibu uwapo taabuni; jina la Mungu wa Yakobo likulinde. Akupelekee msaada kutoka hekaluni mwake; akutegemeze kutoka mlima Siyoni. Azikumbuke sadaka zako zote; azikubali tambiko zako za kuteketezwa. Akujalie unayotamani moyoni mwako, aifanikishe mipango yako yote. Tutashangilia kwa ajili ya ushindi wako; tutatweka bendera kulitukuza jina la Mungu wetu. Mwenyezi-Mungu akutimizie maombi yako yote! Najua Mwenyezi-Mungu atamsaidia mfalme aliyemteua, atamjibu kutoka patakatifu pake mbinguni; kwa mkono wake wa kulia atamjalia ushindi mkubwa. Wengine hujigamba kwa magari ya vita; wengine hujigamba kwa farasi wao. Lakini sisi twajivunia Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu. Hao watajikwaa na kuanguka; lakini sisi tutainuka na kusimama imara. Umjalie mfalme ushindi, ee Mwenyezi-Mungu; utujibu wakati tunapokuomba.



Asante Baba wa Mbinguni tunayaweka haya yote mikononi mwako tukisifu na kushukuru katika yote..
Amina..!!

Asanteni sana wote  kwa kutembelea hapa..
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea sawasawa na mapenzi yake..
Nawapenda.

Mavazi ya makuhani

(Kut 39:1-7)

1“Nawe Mose umlete kwangu Aroni ndugu yako, pamoja na wanawe: Nadabu, Abihu, Eleazari na Ithamari utawateua miongoni mwa Waisraeli, ili wanitumikie kama makuhani. 2Utamshonea ndugu yako Aroni mavazi matakatifu ili apate kuonekana mwenye utukufu na mzuri. 3Waagize mafundi wote ambao nimewapa maarifa wamtengenezee Aroni mavazi ili awekwe wakfu kwa ajili ya kazi ya ukuhani. 4Waambie wamtengenezee vitu vifuatavyo: Kifuko cha kifuani, kizibao,28:4 kizibao: Kiebrania: Efodi; kizibao kitakatifu kilichovaliwa na kuhani mkuu. Juu yake kilibandikwa kifuko cha kifuani. kanzu, joho iliyonakshiwa, kilemba na mshipi. Aroni nduguyo na wanawe watayavaa ili wanitumikie kama makuhani. 5Hao mafundi watatumia sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na nyuzi za dhahabu na kitani safi iliyosokotwa.

Kizibao cha kuhani
6“Watakitengeneza kizibao cha kuhani kwa nyuzi za dhahabu na sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kukitarizi vizuri. 7Kitakuwa na kamba mbili za kukifungia mabegani zilizoshonewa kwenye ncha zake mbili. 8Mkanda wa kukishikia utatengenezwa kwa vifaa hivyohivyo: Kwa nyuzi za dhahabu, sufu ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa na kuwa kitu kimoja na kizibao hicho.
9“Kisha utachukua mawe mawili ya sardoniki ambayo utachora juu yake majina ya wana wa Israeli.28:9 Israeli: Israeli hapa ni sawa na Yakobo. 10Majina sita katika jiwe la kwanza, na majina sita yaliyobakia katika jiwe la pili; majina yafuatane kadiri ya kuzaliwa kwao. 11Utayachora majina hayo juu ya hayo mawe kama vile sonara achoravyo mhuri, kisha uyatie nakshi na kuyaingiza katika vijalizo vya dhahabu. 12Mawe hayo mawili yatawekwa juu ya kanda za kizibao kama kumbukumbu ya makabila kumi na mawili ya Israeli. Hivyo Aroni atavaa majina hayo mabegani mwake mbele yangu mimi Mwenyezi-Mungu kama ukumbusho. 13Utayatengenezea vijalizo viwili vya dhahabu, 14na mikufu miwili ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba. Utaifunga mikufu hiyo kwenye hivyo vijalizo.

Kifuko cha kifuani
(Kut 39:8-21)


15“Utatengeneza kifuko cha kifuani cha kauli28:15 kifuko cha kifuani cha kauli: Namna ya kifuko kilichobandikwa juu ya kizibao chenye mawe matakatifu (aya 30) ambayo yalitumiwa na kuhani kujulisha matakwa ya Mungu. cha maamuzi; kitengenezwe kwa ustadi sawa kama kilivyotengenezwa kile kizibao: Kwa dhahabu, kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa. 16Kifuko hicho ambacho kimekunjwa kitakuwa cha mraba, sentimita 22. 17Kitapambwa kwa safu nne za mawe ya thamani: Safu ya kwanza itakuwa ya akiki, topazi na almasi nyekundu; 18safu ya pili itakuwa ya zumaridi, johari ya rangi ya samawati na almasi; 19safu ya tatu itakuwa ya yasintho, akiki nyekundu na amethisto; 20na safu ya nne itakuwa ya zabarajadi, shohamu na yaspi; yote yatatiwa kwenye vijalizo vya dhahabu. 21Basi, patakuwa na mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama mhuri, ili kuwakilisha makabila yale kumi na mawili. 22Kwa ajili ya kifuko hicho cha kifuani, utatengeneza mikufu ya dhahabu safi iliyosokotwa kama kamba. 23Vilevile utatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya kifuko cha kifuani na kuzitia kwenye ncha mbili za kifuko hicho, 24na mikufu miwili ya dhahabu uifunge kwenye pete hizo za kifuko cha kifuani. 25Zile ncha mbili za mkufu wa dhahabu utazishikamanisha kwenye vile vijalizo viwili vya kile kibati ili zishikamane na kipande cha mabegani cha kizibao upande wa mbele. 26Pia utatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzitia kwenye ncha mbili za chini upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kizibao. 27Kisha utatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzitia mbele katika ncha za chini za vipande vya kizibao, mahali kizibao kinapoungana na mkanda uliofumwa kwa ustadi. 28Kifuko cha kifuani kitafungwa kwenye kizibao kwa kufunganisha pete zake na kizibao kwa kamba ya rangi ya buluu, ili kifuko hicho cha kifuani kisilegee ila kikalie ule mkanda uliofumwa kwa ustadi.
29“Aroni anapoingia mahali patakatifu, atavaa kifuko cha kauli kimechorwa majina ya makabila ya wana wa Israeli; kwa namna hiyo mimi Mwenyezi-Mungu sitawasahau nyinyi kamwe. 30Taz Hes 27:21; Kumb 33:8; Ezra 2:63; Neh 7:65 Kwenye kifuko hicho utatia mawe ya kauli28:30 mawe ya kauli: Kiebrania: Urimu na Thumimu; yalikuwa mawe matakatifu yaliyotumika hapo awali kujua matakwa ya Mungu, taz. Hes 27:21; 1Sam 14:41; 28:6; Ezra 2:63; Neh 7:65. yaninginie kifuani mwa Aroni kila anapokuja mbele yangu. Nyakati hizo ni lazima kila mara kuvaa kifuko hicho, ili aweze kutambua matakwa yangu kuhusu Waisraeli.

Mavazi mengine ya kikuhani

(Kut 39:22-31)

31“Utashona kanzu ya kuvalia kizibao kwa sufu ya rangi ya buluu. 32Itakuwa na nafasi ya kupitishia kichwa katikati, na nafasi hiyo itazungushiwa utepe uliofumwa ili isichanike. 33Taz Sira 45:9 Kwenye upindo wake wa chini, kuzunguka pande zote, itapambwa kwa makomamanga ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, kutakuwa pia na njuga za dhahabu kati ya hayo makomamanga: 34Komamanga, njuga, komamanga, njuga, kuizunguka kanzu yote. 35Aroni atavaa kanzu hiyo kutekeleza huduma yake ya ukuhani na sauti yake itasikika wakati anapoingia mahali patakatifu mbele yangu na wakati anapotoka, njuga hizo zitasikika, naye hatauawa.
36“Kisha, utatengeneza kibati cha dhahabu safi na kuchora juu yake kama mtu achoravyo mhuri, ‘Wakfu kwa Mwenyezi-Mungu.’28:36 Wakfu kwa Mwenyezi-Mungu: Au Mtakatifu kwa Mwenyezi-Mungu. 37Kibati hicho utakifunga mbele ya kilemba kwa ukanda wa buluu. 38Aroni atakivaa kibati hicho kwenye paji la uso wake; kwa hicho kibati atachukua lawama ya makosa ambayo Waisraeli wanaweza kuwa wameyafanya katika kunitolea tambiko takatifu, nami nitazikubali tambiko zao. 39Utamtengenezea Aroni joho iliyonakshiwa kwa kitani safi na kumfumia kilemba cha kitani safi na ukanda ulionakshiwa vizuri.
40“Utawatengenezea wana wa Aroni majoho, mishipi na kofia ili waonekane wana utukufu na uzuri. 41Utamvalisha ndugu yako Aroni na wanawe mavazi hayo, kisha uwapake mafuta na kuwawekea mikono ili kuwaweka wakfu wanitumikie kama makuhani. 42Vilevile utawashonea suruali za kitani zitakazowafunika tangu kiunoni mpaka mapajani, ili wafunike uchi wao. 43Aroni na wanawe watavaa suruali hizo kila wanapoingia katika hema la mkutano, au wanapokaribia kwenye madhabahu, kufanya huduma za makuhani katika mahali patakatifu. Kwa njia hiyo hawataonesha uchi wao na kuwa na hatari ya kuuawa. Hiyo itakuwa kanuni ya kudumu kwa Aroni na wazawa wake.Kutoka28;1-40


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Monday 8 May 2017

Neno la Faraja;Mungu atupe uvumilivu Ndugu/Familia yangu kwa kuondokewa na Ndugu yetu Christopher-Hamisi Mbegete na Watanzania kwa kuondokewa na Watoto wetu wanafunzi wa Lucky Vicent..

Pichani ni ndugu yetu,Kaka na Mpendwa wetu Christopher-Hamisi Mbegete
Naungana na Ndugu/ familia yangu huko nyumbani kwa wakati huu mgumu sana kwa kuondokewa na mpenzi ndugu yetu..
Daima tutakukumbuka, Sina Neno zuri  la kuweza kusema zaidi ya kumshukuru Mungu kwa maisha yako na kuwa nasi na sasa umetangulia..Mungu akatupe faraja na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu..Mungu akawasimamie na kuwaongoza  wote wanaoshiriki katika maandalizi ya kuulaza mwili wako.Na akawabariki na kuwaongezea zaidi ya walipojitoa, kwa Muda, Faraja na yote..
Ulale kwa Amani.


Niungane na familia, wanafunzi /walimu  na Watanzania wenzangu huko nyumbani na popote walipo kwa wakati huu mgumu kwenye Taifa letu
kwakuondokewa na watoto wetu,wadogo zetu wapendwa wetu Walimu na Wafanya kazi..
Mungu Baba akawape nguvu na uvumilivu kwa wakati huu mgumu,Poleni sana wazazi/ndugu na Watanzania..
Mungu akawafariji na kuwaongoza katika yote.
Mlale kwa Amani malaika  wetu,watoto wetu wapendwa..
ni kipindi kigumu sana lakini tumshukuru Mungu katika yote..






Shukrani kwa Mungu
3Atukuzwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba mwenye huruma na Mungu mwenye kuleta faraja yote. 4Yeye hutufariji sisi katika taabu zetu zote, ili nasi tupate kuwafariji wengine katika kila taabu kwa faraja hiyohiyo tunayopokea kutoka kwa Mungu. 5Naam, kadiri mateso ya Kristo yanavyozidi ndani yetu, ni kadiri hiyohiyo tunazidi kufarijiwa naye. 6Ikiwa tunapata taabu, basi ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu. Tukifarijika, ni kwa ajili ya kuwafariji nyinyi na kuwaunga mkono mpate nguvu ya kustahimili mateso yaleyale tunayoteseka sisi. 7Tena, matumaini tuliyo nayo kwa ajili yenu ni imara; tunajua kwamba mkishiriki mateso yetu, mtashiriki pia faraja yetu.[2wakorintho 1;3-7]






Bwana anakuja
13Ndugu, twataka mjue ukweli kuhusu wale ambao wamekwisha fariki dunia, ili msipatwe na huzuni kama watu wengine wasio na matumaini. 14Sisi tunaamini kwamba Yesu alikufa, akafufuka; na hivyo sisi tunaamini kwamba Mungu atawaleta pamoja na Yesu wale wote waliofariki wakiwa wanamwamini.
15Hili tunalowaambieni ni fundisho la Bwana, kwamba sisi tulio hai, ambao tutakuwa tumebaki wakati Bwana atakapokuja, hakika hatutawatangulia wale waliokwisha fariki dunia. 16Maana patatolewa amri, sauti ya malaika mkuu, sauti ya tarumbeta ya Mungu, naye Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni. Ndipo wale waliokufa wakiwa wanamwamini Kristo watafufuliwa kwanza. 17Kisha sisi tulio hai wakati huo tutakusanywa pamoja nao katika mawingu kumlaki Bwana hewani. Na hivyo tutakuwa daima pamoja na Bwana. 18Basi, farijianeni kwa maneno haya.[1Wathesalonike 4;13-18]


Wapendwa/Waungwana leo tuungane na wenzetu katika kuombeleza Msiba huu..
Mniwie Radhi kesho kwa Neema ya Mungu tutaendelea.
Muwe na wakati mwema na msisahau kuwaweka katika maombi/sala/dua wote wanaopitia mapito haya.

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe sana.

Friday 5 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 27...



Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Tumshukuru Mungu kwa wema na fadhili zake kwetu..
Mungu wetu, Baba yetu, Muumba wetu, Muumba Mbingu na Nchi, Muumba wa vyote vilivyopo, Mume wa Wajane, Baba wa Yatima,Mungu wa Abrahamu,Isaka na Yakobo, Yahweh..!! Jehovah nissi..!, Jejovah rapha..!, Jehovah shalom..! Jehovah jireh..! Jehovah Shammah..!Jehovah Rohi..!!
Asante Baba kwa wema na fadhili zako, Asante kwa ulinzi wako usiku mzima,Asante kwakutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona siku hii Baba wa Mbinguni..

Tunakuja mbele zako tukijinyenyekeza na kuomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua,kutojua Mfalme wa Amani tunaomba na sisi utupe Neema ya kuweza kuwasamehe wale waliotukosea..
Baba tunaomba utuokoe na Mwovu na kazi zake zote, zikashindwe na ututakase  Miili yetu na Akili zetu na Utufunike  kwa Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..
Baba ukatuponye rohoni na Roho mtakatifu akatuongoze katika yote na tupate kutambua/kujitambua na tukawe na kiasi..

Tukapendane na kusaidiana katika kweli,tusiwe watu wa kujikweza na kujitapa,tusiwe wenye kuhukumu, tusiwe watu wa kisasi,tusiwe wenye kiburi na kukoseana adabu.

Tukawe chombo chema na tukatumike sawasawa na mapenzi yako..
Tukawe na Imani na kuwaombea wengine, Tukawe wavumilivu na wenye kushukuru..



Kwa hiyo, ndugu zangu, maadamu Mungu ni mwenye huruma nyingi, nawasihi kwa moyo wote: Mtoleeni Mungu miili yenu kama tambiko iliyo hai, takatifu na yenye kupendeza. Hii ndiyo njia yenu halisi ya kumwabudu. Msiige mitindo ya ulimwengu huu, bali Mungu afanye mabadiliko ndani yenu kwa kuzigeuza fikira zenu. Hapo ndipo mtakapoweza kuyajua mapenzi ya Mungu na kutambua jambo lililo jema, linalompendeza na kamilifu. Kutokana na neema aliyonijalia Mungu, nawaambieni nyinyi nyote: Msijione kuwa ni kitu zaidi kuliko mnavyopaswa kuwa. Fikira zenu na ziwe na kiasi kadiri ya kipimo cha imani Mungu aliyomgawia kila mmoja.

Mfalme wa Amani tunaomba ukawaguse na mkono wako wenye nguvu wote wanaopitia magumu/majaribu,shida/tabu,waliokwenyevifungo mbalimbali,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao, wanaotafuta watoto,wanaotafuta mume/mke,waliokata tamaa,wenye hofu na mashaka,wanaugua rohoni,waliokataliwa na walio njia panda hawaelewi waanzie wapi waishie wapi..maisha yamekuwa magumu hawana kazi wala biashara Baba ukawape ubunifu, Maarifa na ukawape hekima na busara kwenye maamuzi...

Mfalme wa Amani tunaomba ukabariki ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo, ukabariki tuingiapo/tutokapo,vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri na tutembeapo hatua zetu ziwe nawe Yahweh..
Ukamguse kila mmoja na kumbariki naye aweze kumbariki mwingine, iwe kwa chakula, iwe kwa kumuombea mwinzie, iwe kwa pesa, iwe kwa kumtakia maneno ya baraka na kumsamehe kabisa yule aliye mkosea na alikuwa kikwazo kwenye moyo wake..

Baba ukatende na kuponya mioyo yao, ukamalize kabisa uchungu moyoni, ukawape neema ya kupendana na kutakiana amani ya moyo..na wakawe na kiasi ili wasije kukwazana tena..

Ndugu yangu mpendwa yakabidhi hayo mapito yako kwa Mungu na umuombe akupe neema ya kutua hiyo mizigo uliyobeba..yanini kujitesa na mizigo mizito na yupo awezaye kukutua?Yanini kujitafutia mateso na kuugua rohoni na mponyaji yupo?
Mkabidhi Mungu nawe uwe huru na mwepesi..
Mungu wetu atupenda na alimtoa mwanawe mpendwa Bwana wetu Yesu Kristo aliteseka ili sisi tupate kupona..

Matafuteni Bwana maadam anapatikana..
Kwa Mungu yote yanawezekana...
Sifa na utukufu tumrudishie Mungu wetu, Tunakushuru Mungu wetu na tunayaweka haya yote mikononi mwako..
Amina..!
Asante kwa wote mnaotembelea hapa
Mungu aendelee kuwabariki na kuwatendea zaidi..
Nawapenda.

Madhabahu

(Kut 38:1-7)

1“Utatengeneza madhabahu kwa mbao za mjohoro. Madhabahu hiyo itakuwa ya mraba, urefu wake mita27:1 mita: Vipimo hivyo awali ni dhiraa, urefu wa kutoka kiwiko cha mkono hadi ncha ya kidole cha kati. mbili na robo, na upana wake mita mbili na robo; kimo chake kitakuwa mita moja na robo. 2Katika kila pembe ya madhabahu hiyo utatengeneza upembe ambao utakuwa umeundwa kutokana na madhabahu yenyewe. Madhabahu hiyo yote utaipaka shaba. 3Utaitengenezea vyombo vyake: Vyungu vya majivu, sepetu, na mabirika, na nyuma na visahani vya kuchukulia moto. Vyombo vyake vyote utavitengeneza kwa shaba. 4Kisha utatengeneza wavu wa shaba wenye pete nne za shaba kwenye pembe zake nne. 5Wavu huo utauweka kwenye ukingo wa madhabahu upande wa chini ili ufike katikati ya madhabahu. 6Utatengeneza pia mipiko ya mjohoro ya kuibebea madhabahu; nayo utaipaka shaba. 7Mipiko hiyo itaingizwa kwenye zile pete kila upande wa madhabahu, wakati wa kuibeba. 8Utaitengeneza madhabahu kwa mbao, na iwe yenye mvungu ndani, kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.

Kitalu cha hema la mkutano

(Kut 38:9-20)
9“Utatengeneza ua wa hema la mkutano. Upande wa kusini wa ua kutakuwa na vyandarua vilivyotengenezwa kwa kitani safi iliyosokotwa ambavyo vitakuwa na urefu wa mita 44 kwa upande mmoja. 10Vyandarua hivyo vitashikiliwa na nguzo ishirini za shaba zenye vikalio vya shaba. Lakini kulabu za nguzo hizo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha. 11Hali kadhalika upande wa kaskazini, urefu wa chandarua utakuwa mita 44, na nguzo zake 20 za shaba, lakini kulabu za nguzo na vitanzi vyake vitakuwa vya fedha. 12Upande wa magharibi wa ua utakuwa na chandarua chenye urefu wa mita 22, na nguzo zake 10 na vikalio vyake 10. 13Upande wa mashariki kuliko na mlango, ua utakuwa na upana wa mita 22. 14Chandarua cha upande mmoja wa mlango kitakuwa na upana wa mita 6.5, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu. 15Vilevile katika upande wa pili wa mlango chandarua kitakuwa mita 6.5, pamoja na nguzo tatu na vikalio vyake vitatu. 16Mlango wenyewe wa ua utakuwa na pazia zito lenye urefu wa mita 9, lililotengenezwa kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kutariziwa vizuri. Pazia hilo litashikiliwa na nguzo nne zenye vikalio vinne. 17Nguzo zote kuuzunguka ua zitashikamanishwa kwa fito za fedha, kulabu zake zitakuwa za fedha na vikalio vyake vitakuwa vya shaba. 18Ua huo utakuwa na urefu wa mita 44, upana wa mita 22, na kimo cha mita 2.25. Vyandarua vyake vitakuwa vya kitani safi na vikalio vyake vya shaba. 19Vyombo vyote vya hema takatifu vya matumizi ya kila aina, pamoja na vigingi vyote na hata vile vya ua vitakuwa vya shaba.

Taa
(Lawi 24:1-4)

20“Utawaamuru Waisraeli wakuletee mafuta safi kwa ajili ya taa, kuwe na taa inayowaka daima. 21Hiyo itakuwa ndani ya hema la mkutano nje ya pazia hilo mbele ya sanduku la maamuzi27:21 maamuzi: Au agano; Kiebrania: Eduti. na Aroni na wanawe wataitunza mbele yangu tangu jioni mpaka asubuhi. Agizo hili sharti lifuatwe daima na Waisraeli wote, kizazi hata kizazi.
Kutoka27;1-21


Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.

Thursday 4 May 2017

Kikombe Cha Asubuhi;Kutoka 26...

Shalom,Habari za Asubuhi,Hamjambo,Mmeamkaje Wapendwa/Waungwana?
Mungu wetu yu mwema sana..Tumshukuru na kulisifu jina lake..
kwa maana pasipo yeye sisi si kitu kabisa..

Asante Baba wa Mbinguni kwa kutulinda usiku mzima na kutuamsha salama..Asante kwa kutuchagua na kutupa kibali cha kuendelea kuiona leo hii..
Tazama Jana imepita Baba Leo ni siku mpya na Kesho ni siku nyingine..
Tunashuka mbele zako tukijinyenyekeza na kujiachilia mikononi mwako Jehovah...!
Tunaomba utusamehe pale tulipokwenda kinyume nawe kwa kuwaza,kwakunena,kwakutenda,kwakujua au kutojua Mfalme wa Amani..

Tunaomba utupe nasi Neema ya kuweza kuwasamehe waliotukosea..

Yahweh..! Tunaomba utulinde na kutuokoa na yule mwovu na kazi zake zote..

Roho Mtakatifu akatuongoze katika yote na tukawe na kiasi..
Tunaomba ututakase Miili yetu na Akili zetu na kutufunika na Damu ya Mwanao mpendwa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo wa Nazareti..


Jehovah..! Tunaomba ukabariki Ridhiki zetu ziingiazo na zitokazo..zikawe baraka na tuweze kuwabariki na wengine wenye kuhitaji..
Mungu wetu tunaomba ukabariki Kazi zetu,Biashara,Masomo,Vilaji/vinywaji,vyombo vya usafiri, tuingiapo/tutokapo,na tumbeapo hatua zetu ziwe nawe Jehovah..!!


Baba tazama Yatima,Wajane,wenye shida/tabu,wanaopitia magumu/majaribu mbalimbali,waliokata tamaa,waliokataliwa,wenye hofu na mashaka,wanaogua rohoni,wagonjwa,wafiwa ukawe mfariji wao,waliokatika vifungo mbalimbali Baba tunaomba ukawafungue na kuwagusa na mkono wako wenye nguvu,ukawaponye kimwili na kiroho pia,ukaonekane kwenye shida zao Jehovah..!Ukasikie kulia kwao na ukapokee maombi yao,ukawanyanyue na kuwaongoza, ukawabariki na kuwafariji Yahweh..!!

Ndugu yangu mpendwa makabidhi Mungu shida zako yeye hatokuacha kamwe,Yeye anakujua zaidi ya yeyote,hakuna lililogumu kwakwe, Yeye hachoki binadamu anaweza kukuchoka na kukusimanga, binadamu anaweza kukuumiza zaidi,binadamu anaweza kukukwamisha zaidi,binadamu anaweza asikuelewe na kukuona mzigo,binadamu anaweza kukukatisha tamaa zaidi, binadamu anaweza asipende kuona maendeleo yako,Yupo mponyaji wa kweli, yeye anayependa na kufurahia maendeleo yako,yeye hufurahi zaidi ukimrudia na husamehe kabisa, Ukimwamini Mungu yote yanawezekana..Mtafute anapatikana,Mwite ataitika,Muombe atajibu, Muite atasikia..Kwa Mkono wake wenye nguvu atakugusa na kukubariki..


Tumtukuze Mungu wetu kwa nafasi tuliyonayo..
Kama muimbaji Muimbie na kumsifu kupitia uimbaji wako,kama mfinyanzi finyanga vyungu vya kuwekea maua tukapambe nyumba yake,Mungu ametupa vipawa tofauti, hakuna kidogo mbele zake..
hivyo ulivyo kuna karama Mungu amekupa, kwako unaweza  kuona ni ndogo lakini mbele za Mungu ni fahari na anamakusudi yake..Itumie vyema na kwa hiyari yako pasipo kulazimishwa..

Mwili una viungo vingi, kila kimoja na kazi yake. Hali kadhalika ingawa sisi ni wengi, tu mwili mmoja kwa kuungana na Kristo, na kila mmoja ni kiungo cha mwenzake. Basi, tunavyo vipaji mbalimbali kadiri ya neema tuliyopewa. Mwenye kipaji cha unabii na akitumie kadiri ya imani yake. Mwenye kipaji cha utumishi na atumikie. Mwenye kipaji cha kufundisha na afundishe. Mwenye kipaji cha kuwafariji wengine na afanye hivyo. Mwenye kumgawia mwenzake alicho nacho na afanye hivyo kwa ukarimu. Msimamizi na asimamie kwa bidii; naye mwenye kutenda jambo la huruma na afanye hivyo kwa furaha.

Tukawe barua njema na tusomeke vyema..sawasawa na mapenzi yake..
Sifa na utukufu tumrudishie Mungu wetu,Tunayaweka haya yote mikononi mwako Baba wa Mbinguni..

Tukishukuru na kuamini wewe ni Mungu wetu Leo na hata milele..
Amina..!

Mungu akawaguse na kuwatendea sawasawa na mapenzi yake,msipungukiwe katika mahitaji yenu na muweze kuwabariki na wengine..
Asanteni sana kwakupita hapa Mungu awabariki mno..
Nawapenda.



Hema la mkutano

(Kut 36:8-38)

1“Zaidi ya hayo yote, utatengeneza hema takatifu kwa mapazia kumi ya kitani safi iliyosokotwa, na kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu. Mapazia hayo utayapamba kwa michoro ya viumbe wenye mabawa waliotariziwa. 2Kila pazia litakuwa na urefu wa mita 12 na upana wa mita 2. Mapazia hayo yawe ya kipimo kimoja. 3Utaunganisha mapazia matano yawe kipande kimoja na mapazia mengine matano yawe kipande cha pili. 4Utashonea vitanzi vya buluu upindoni mwa pazia la mwisho la kipande cha kwanza, hali kadhalika utashonea vitanzi mwishoni mwa pindo la nje la kipande kingine cha pazia. 5Utatia vitanzi hamsini katika pazia moja na vitanzi vingine hamsini kwenye utepe wa pazia la pili; vitanzi vyote vielekeane. 6Kisha utatengeneza kulabu hamsini za dhahabu ili kuunganishia vile vipande viwili vya mapazia, hivyo hema litakuwa kitu kimoja.
7“Pia utatengeneza kifuniko cha hema kwa mapazia kumi na moja ya manyoya ya mbuzi. 8Kila pazia litakuwa na urefu wa mita 13, na upana wa mita 2. Mapazia yote hayo 11 yatakuwa na kipimo kilekile. 9Utaunga mapazia matano pamoja, na mapazia sita pamoja. Pazia la sita utalikunja mara mbili mbele ya hema. 10Kisha utafanya vitanzi hamsini upindoni mwa pazia la mwisho la kipande cha kwanza, na vitanzi hamsini upindoni mwa pazia la mwisho la kipande cha pili. 11Utatengeneza kulabu hamsini za shaba na kuziingiza katika vile vitanzi hamsini ili kuunganishia vile vipande viwili vya mapazia na hivyo kufanya pazia moja la hema. 12Ile nusu ya pazia iliyobaki utaitundika upande wa nyuma wa hema. 13Nusu mita ya urefu wa mapazia iliyo ya ziada utaikunja ininginie pande zote mbavuni mwa hema ili kulifunika. 14Utatengeneza pia kifuniko kingine cha hema kilichofanywa kwa ngozi laini ya kondoo dume na ngozi laini ya mbuzi.
15“Utatengeneza mbao za mjohoro za kusimama wima kwa ajili ya hema. 16Kila ubao utakuwa na urefu wa mita 4, na upana wa sentimita 66. 17Kila ubao utakuwa na ndimi mbili za kuunganishia. Utazifanyia mbao zote ndimi mbili. 18Basi, utatengeneza hizo mbao za hema hivi: Mbao ishirini kwa ajili ya upande wa kusini, 19na vikalio arubaini vya fedha chini ya hizo mbao ishirini, vikalio viwili chini kwa kila ubao ili kushikilia zile ndimi zake mbili na vikalio viwili viwe chini ya ubao mwingine ili kushikilia zile ndimi zake mbili. 20Upande wa kaskazini wa hema, utatengeneza mbao ishirini, 21na vikalio vyake arubaini vya fedha, vikalio viwili chini ya kila ubao. 22Kwa upande wa nyuma, ulio magharibi ya hema, utatengeneza mbao sita. 23Utatengeneza pia mbao mbili kwa ajili ya pembe za hema upande wake wa nyuma. 24Mbao hizo za pembeni ziachane chini lakini zishikamanishwe kwa juu kwenye pete ya kwanza. Mbao zote za pembeni zifanywe vivyo hivyo ili zifanye pembe mbili. 25Hivyo kutakuwa na mbao nane pamoja na vikalio vyake kumi na sita vya fedha: Vikalio viwili chini ya kila mbao na vikalio viwili chini ya ubao mwingine.
26“Utatengeneza pau za mjohoro; pau tano kwa ajili ya mbao za upande mmoja wa hema, 27na pau tano kwa ajili ya upande wa pili wa hema, na pau tano kwa ajili ya mbao za upande wa nyuma wa hema, ulio magharibi. 28Upau wa katikati uliofika nusu ya jengo la hema utapenya katikati toka mwisho huu hadi mwisho mwingine wa hema. 29Mbao zote utazipaka dhahabu na kuzifanyia pete za dhahabu zitakazoshikilia hizo pau, ambazo pia utazipaka dhahabu. 30Hivyo utalitengeneza hema hilo kulingana na mfano niliokuonesha mlimani.
31“Utatengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, zambarau na nyekundu na kitani safi iliyosokotwa. Pazia hilo utalitarizi kwa ustadi kwa viumbe wenye mabawa. 32Utalitundika pazia kwenye nguzo nne za mjohoro zilizopakwa dhahabu, zenye kulabu za dhahabu na vikalio vinne vya fedha. 33Taz Ebr 6:19; 9:3-5 Utalitundika pazia hilo kwenye vifungo, kisha ulilete lile sanduku la ushuhuda humo ndani kukiwa na vibao viwili vya mawe, nyuma ya pazia hilo. Pazia hilo litatenga mahali patakatifu na mahali patakatifu sana. 34Ndani ya mahali patakatifu utakiweka kile kiti cha rehema juu ya sanduku la maamuzi. 35Ile meza ya mjohoro utaiweka upande wa nje wa pazia hilo, na kile kinara cha taa utakiweka upande wa kusini wa hema, mkabala wa meza. Meza hiyo itakuwa upande wa kaskazini.
36“Kwa ajili ya mlango wa hema utatengeneza pazia zito kwa sufu ya rangi ya buluu, zambarau na nyekundu, na kitani safi iliyosokotwa, na kutariziwa vizuri. 37Vilevile utatengeneza nguzo tano za mjohoro na kuzipaka dhahabu. Nguzo hizo zitakuwa na kulabu za dhahabu, na kila moja itakuwa na tako la shaba.

Kutoka26;1-37

Biblia Habari Njema kwa Watu Wote(BHN)

"Swahili Na Waswahili"Mbarikiwe.