Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 10 September 2015

Kipindi cha JUKWAA LANGU.....Sep 7 2015 (Part One)


JUKWAA LANGU ni kipindi ambacho kitakuwa kikikujia kila Jumatatu, kujadili mambo mbalimbali yanayotokea nchini Tanzania, na zaidi kuhusu Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu.

 Hii ni sehemu ya kwanza ya kipindi cha Septemba 7, 2017 ambapo studioni tulitembelewa na Shamis Abdul, kuwezesha mjadala.

Pia, kulikuwa na washiriki kwa njia ya simu, toka pande mbalimbali za dunia

Monday 7 September 2015

Bin'adam "TENA"....Na maisha KINYUMENYUME. Apumzikaye kusherehekea SIKU YA KAZI


Na Mubelwa Bandio

 Ni SIKU YA KAZI hapa Marekani. Ama niseme kuthamini kazi. Ama siku ya wafanyakazi. Lakini vyovyote iwavyo, ni siku ambayo wengi wetu hapa Marekani tunakuwa na "siku ya mapumziko". NDIO, DAY OFF katika kusherehekea SIKU YA KAZI.

Mmmmmhhh!!! Umeona eeee?


Nilishaandika kuhusu kinyumenyume cha Bin-adamu katika kutenda, kunena na kuwaza. Kuwa kwanini tuwazishwe vitu kwa namna nyingine?


Kwanini nchi nyingi Afrika zisherehekee UHURU kwa staili ya gwaride kama la WAKOLONI WALIOTUTAWALA?


Kwanini siku ya wakulima isherehekewe mjini, na wapatao "day off" ni wale wasio wakulima ilhali wakulima hawapati sherehe yoyote siku hiyo?


Ni kwenye muendelezo huu wa KWANINI, najikuta naleta MASWALI YAFUATAYO, ambayo nilitumiwa na rafiki yangu, na si mawazo yangu.


TUMUWAZE BIN'ADAM NA UNAFIKI WA MAWAZO YA KIMATENDO.


Soma kisha uwaze, "bin'adamu anawaza nini kutenda atendayo?" Japo nilitumiwa NICHEKE, lakini yaliniwazisha pia


-Why do supermarkets make the sick walk all the way to the back of the store to get their prescriptions while healthy people can buy cigarettes at the front?


-Why do people order double cheeseburgers, large fries, and a diet coke.


-Why do banks leave vault doors open and then chain the pens to the counters.


-Why do we leave cars worth thousands of dollars in our driveways and put our useless junk in the garage.




EVER WONDER .......



-Why
the sun lightens our hair, but darkens our skin?


-Why can't women put on mascara with their mouth closed?


-Why don't you ever see the headline 'Psychic Wins Lottery'?


-Why is 'abbreviated' such a long word?


-Why is it that doctors call what they do 'practice'?


-Why is lemon juice made with artificial flavoring, and dish washing liquid made with real lemons?


-Why is the man who invests all your money called a broker?


-Why is the time of day with the slowest traffic called rush hour?


-Why isn't there mouse-flavored cat food?


-Why didn't Noah swat those two mosquitoes?


-Why do they sterilize the needle for lethal injections?


You know that indestructible black box that is used on airplanes? Why don't they make the whole plane out of that stuff?!


-Why don't sheep shrink when it rains?


-Why are they called apartments when they are all stuck together?


If flying is so safe, why do they call the airport the terminal?




HIVI TUNAWAZA NINI?




***"Waliwaza nini ni kipengele cha kuelimishana tukifurahia. Hiki kitakuwa kikikuletea habari za kweli na kushangaza kuhusu watu ambao wamefanya yale ambayo unaweza kujiuliza kuwa WALIWAZA NINI? wakati wanatenda haya. Kitakuwa na habari fupifupi kutoka ulimwenguni kote. Kwa habari zaidi kuhusu kipengele hiki BOFYA HAPA"***

Wimbo mpya wa UCHAGUZI toka kwa INNOCENT GALINOMA


Kuelekea uchaguzi mkuu nchini Tanzania, watu kupitia fani na kazi mbalimbali wamekuwa wakijaribu kuhamasisha wananchi kushiriki kufanya maamuzi yatakayolipeleka taifa letu mbele.

Innocent Galinoma, ni msanii mkongwe wa Reggae anayefanya kazi zake nchini Tanzania.

Naye ametunga wimbo maalum kwa ajili ya uchaguzi huu mkuu. Akisisitiza kuhusu kusikiliza na kuwahoji wagombea ili kujua fika wanalotaka kutufanyia katika kutatua kero zetu

Karibu usikilize kibao....UCHAGUZI

Sunday 6 September 2015

Nimatumaini yangu Jumapili inaendelea vyema;Amani na itawale Tanzania,Burudani - Sisi sote,Gusa,Mungu yu mwema,Moyo wangu......




Wapendwa/Waungwana jumapili iendelee kuwa njema na yenye Baraka,Upendo na Amani ikatawale

 1Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, 2 “Iambie jumuiya yote ya watu wa Israeli hivi: Ni lazima muwe watakatifu kwani mimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, ni mtakatifu.3Kila mmoja wenu ni lazima amheshimu mama yake na baba yake, na kuzishika Sabato zangu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu. 4Msizigeukie sanamu za miungu, wala msijitengenezee sanamu za kusubu za miungu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
5“Mnaponitolea mimi Mwenyezi-Mungu sadaka za amani, mtanitolea kama itakiwavyo ili mpate kukubaliwa.6Sadaka hiyo ni lazima iliwe siku hiyohiyo inapotolewa au kesho yake. Chochote kinachobaki hadi siku ya tatu ni lazima kiteketezwe kwa moto. 7Kama sehemu ya nyama yake italiwa siku ya tatu, tendo hilo ni chukizo; na sadaka hiyo haitakubaliwa, 8naye atakayekula nyama hiyo ni lazima awajibike kwa uovu wake kwa sababu amekitia unajisi kitu kitakatifu cha Mwenyezi-Mungu. Mtu huyo atatengwa na watu wake.
Neno La Leo;Walawi19;1-37
Kutenda mema

9 “Utakapovuna mavuno ya nchi yako, usivune kabisa hadi mpakani mwa shamba wala usirudi nyuma kukusanya mabaki. 10Msirudie kukusanya kila kitu katika shamba la mizabibu, wala usiokote zabibu zilizoanguka chini; utawaachia maskini na wageni. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
11 “Msiibe, msidanganye wala kuambiana uongo.12Msiape uongo kwa jina langu hata kulikufuru jina la Mungu wenu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
13 “Usimdhulumu jirani yako wala kumwibia. Mshahara wa mtu aliyeajiriwa usikae kwako usiku kucha hadi asubuhi.14 Usimlaani kiziwi wala kuweka kizuizi mbele ya kipofu, bali umche Mungu wako. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
15 “Unapotoa hukumu uamue kwa haki; usimpendelee maskini wala kumwogopa mwenye cheo. Bali ni lazima kumwamua jirani kwa haki. 16Kamwe usipitepite ukiwachongea watu wa jamaa yako. Usiyatie maisha ya jirani yako katika hatari ya kifo kwa maneno yako. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
17 “Usimwekee kisasi ndugu yako moyoni mwako, bali upatane daima na jirani yako ili usije ukatenda dhambi. 18Usijilipize kisasi au kuwa na kinyongo dhidi ya wazawa wa watu wako bali umpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.


19 “Yakupasa kuyashika masharti yangu. Usiiache mifugo yako ipandwe na wanyama wa aina nyingine. Shambani mwako usipande mbegu za aina mbili. Usivae vazi lililofumwa kwa aina mbili za nguo.
20“Mwanamume akilala na mwanamke mtumwa ambaye ameposwa na mwanamume mwingine, lakini bado hajakombolewa wala kupewa uhuru, uchunguzi ufanywe. Lakini wasiuawe kwa sababu mwanamke huyo hakuwa bado huru. 21Mwanamume huyo ataleta mbele ya hema la mkutano sadaka yake ya kondoo dume ya kuondoa hatia na kunitolea mimi Mwenyezi-Mungu. 22Kuhani atamfanyia ibada ya upatanisho kwa kutumia kondoo huyo mbele ya Mwenyezi-Mungu kwa ajili ya dhambi aliyotenda; naye atasamehewa dhambi hiyo aliyotenda.
23“Mtakapofika katika nchi ya Kanaani na kupanda aina zote za miti ya matunda, matunda hayo hamtayala; hamtaruhusiwa kuyala kwa muda wa miaka mitatu.24Mnamo mwaka wa nne matunda yake yote yatakuwa matakatifu, yatatolewa kuwa sadaka ya sifa, kwa Mwenyezi-Mungu. 25Lakini matunda ya kuanzia mwaka wa tano hayo mnaweza kula, na mavuno yenu yataongezeka. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
26 “Msile nyama yoyote yenye damu. Msipige bao wala kufanya uchawi. 27 Nywele zenu msizikate pembeni wala kunyoa ndevu zenu. 28Msijitie alama zozote mwilini mwenu kwa ajili ya kuomboleza au kujikatakata mwilini au kujichanja chale. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.


29 “Usimchafue binti yako kwa kumfanya kahaba, nchi nzima isije ikaangukia katika ukahaba na hivyo kujaa uovu.30 Mtazishika Sabato zangu na kupaheshimu mahali pangu patakatifu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.
31 “Msiwaendee waaguzi wa mizimu wala wachawi ili kuwaomba wawaagulie na hivyo mkajitia najisi. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.
32“Uwapo mbele ya mzee ni lazima usimame ili kumpa heshima yake; nawe umche Mungu wako. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.



33“Kama kuna mgeni katika nchi yako usimtendee vibaya. 34Huyo mgeni anayekaa nawe atakuwa kwako kama mwenyeji nawe utampenda kama unavyojipenda mwenyewe, kwa kuwa nawe ulikuwa mgeni katika nchi ya Misri. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu.




35 “Usikose kamwe kuamua kwa haki kuhusu vipimo vya urefu, uzito na ujazo. 36Ni lazima mtumie mizani halali, na vipimo vilivyo halali. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, niliyewatoa katika nchi ya Misri. 37Ni lazima kuyashika na kuyatekeleza masharti yangu na maagizo yangu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.”

Bible Society of Tanzania




"Swahili na Waswahili" Mbarikiwe wote.

Saturday 5 September 2015

Reggae Time ya Pride FM......Justin Kalikawe




Ni zaidi ya miaka 12 sasa tangu kuondokewa na mwanamuziki mahiri wa Reggae kutoka nchini Tanzania, Justine Kalikawe.

Kwangu
ni kumbukumbu “mbichi” ya kuondoka kwake, kwa kuwa alifariki tukiwa
kwenye mkakati wa kufufua hamasa na umuhimu wa muziki wa reggae nchini.

Nakumbuka
ilikuwa ni mwaka 2003. Mwaka ambao ulikuwa na mambo mengi saana kwangu.
Ndio mwaka ambao nikiwa na Dj Fax (wakati huo sote tukiwa 100.5 Times
Fm) tulipanga mikakati ya kuwa na kipindi bora zaidi cha Reggae jijini
Dar (ambako radio hiyo ilikuwa ikisikika).

Na nakumbuka tulipanga
kukutana na kushauriana na wadau mbalimbali wa Reggae nchini kuhusu
namna tunavyoweza kushirikiana kuunyanyua muziki huo uliolenga katika
KUELIMISHA, KUBURUDISHA na KUIKOMBOA AKILI YA JAMII ya wanyonywaji. Ni
katika harakati hizo nilipoweza kuonana na kufanya mahojiano na wasanii
kama Jah Kimbute, Ras Inno na nikakosa nafasi kuonana na Justine
Kalikawe ambaye alikuwa akikosekana kutokana na ratiba yake ya kurekodi.
Hivyo nikawa "namvizia" ili kujua muda ambao hashiriki kurekodi nimpate
naye aweze kuizungumzia tasnia ya Reggae nchini Tanzania.

Bahati
mbaya Justine aliondoka na kwenda nje ya nchi kwa zaiara ya kimuziki na
aliporejea hakukaa muda mrefu akakutwa na mauti. Huo ndio ukawa mwisho
wa ushiriki wake katika mkakati huo.

Lakini wakati anafariki,
nilikuwa likizo Bukoba, hivyo siku hiyohiyo nilipata taarifa
zilizonishtua sana, lakini nikazikubali na kuanza mikakati ya kushiriki
mazishi yake, jambo ambalo nililifanikisha.

Lakini….

Justin Kalikawe ni nani?

Thursday 3 September 2015

DIASPORA YA MONTGOMERY COUNTY YAMUAGA BALOZI AMINA SALUM ALI




 Bwn. Daniel Korona akisherehesha hafla futi ya kumuaga Balozi wa Umoja wa Afrika aliyemaliza muda wake Mhe. Amina Salum Ali iliyoandaliwa na Jumuiya ya Diaspora kutoka Afrika wanaoishi Montgomery county iliyofanyika siku ya Jumatano Sept 2, 2015 Silver Spring, Maryland.
Kulia ni mwongozaji maswali Bi. Soffie Ceesay ambaye ni mwanachama mwanzilishi wa Montgomery County's African Affairs Advisory Group na African Immigrant Caucus akimuuliza Mhe. Amina Salum Ali maswali mbalimbali likiwemo nini anajivunia kwenye uongozi wake kama Balozi wa kwanza wa Umoja wa Afrika nchini Marekani. Balozi Amina Salum Ali alieleza ni ushirikiano wa nyanja mbalimbali mabazo nchi za Afrika zimenufaika na kupata mafanikio na uhusiano wa AU na Marekani kwa kuwezesha kupata Balozi wao nchini Marekani na kikubwa kabisa katika historia ya AU na yeye  kama Balozi kuwezesha Rais Barack Obama kwa mara ya kwanza katika historia kama Rais wa Marekani kuhutubia Umoja huo.


Isiah Leggett ambaye ni Montgomery County Executive akimtunukia cheti Mhe. Balozi Amina Salum Ali


Balozi Amina Salum Ali akitoa shukurani zake ambapo leo anaondoka kurudi Tanzania baada ya kumaliza muda wake kama Balozi wa kwanza wa Umoja wa Afrika nchini Marekani kazi aliyoifanya tangia 2006.
 Wahudhuriaji 
 Wageni waalikwa kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani.

Tuesday 1 September 2015

Mahojiano na Tausi Sued juu ya CSI FUNDRAISING




Dear All,



Come join the Embassy of Tanzania and Childbirth
Survival International (CSI) for CSI’s first annual fundraising on
September 12th at 4:30pm to 7pm, at the Embassy of Tanzania, Washington
DC.



In Tanzania, many of the lives lost during pregnancy,
childbirth, and immediately after birth, are often 100% preventable. We
are calling upon You to join us and help save lives. This fundraising is
to kickoff CSI’s saving lives at birth project in Biharamulo District
in northwest Tanzania. Biharamulo is one of Tanzania’s poorly performing
Districts that deserves immediate support and attention – We thank you
for answering the call. Visit www.childbirthsurvivalinternational.org for more information.



There’s
a registration fee of $100 and it includes a raffle ticket. All
donations are tax deductible and will be used to implement project
activities in Biharamulo. Registration link here.



Light Refreshments | Entertainment | Raffle Prizes | Networking



For information about the event, please contact

Sandra Kiyonga at sandra.kiyonga@childbirthsurvivalinternational.org or call 202-763-2100.



Tuko Pamoja!