Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Sunday 7 July 2013

Nawatakia J'Pili njema na yenye Furaha;Burudani -Sifa Voices,Enda Nasi na Nyingine!!!!!!










Wapendwa Muwe na J'Pili njema yenye Furaha,Amani,Rehema,Wema na Hekima....
N'nani aliye na hekima na ufahamu kwenu? Na aonyeshe kazi zake kwa mwenendo wake mzuri, katika upole  wa hekima...

Neno La Leo:Waraka wa Yakobo;3:10-18..Na tunda la haki hupandwa katika amani na wale wafanyao amani.

"Swahili Na Waswahili"Mungu Atubariki Sote.

Saturday 6 July 2013

Chaguo La Mswahili Leo;Nyota Ndogo-Anakwambia,Kuna Watu Na Viatu na nyingine!!!!!









Waungwana; Leo tunaye "NYOTA NDOGO"  Ni ndogo inayo Nga'aa...
Mhhh...Rafiki yangu mpendwa...naja kwako siku nyingi wanipokea kwa uzuri siku zote,Wakati sina wanipa nitakachoo.....
Hivi majuzi nilipata kazi nzuri  nikaja kukueleza,Mtu wa kwanza nilifiria ni wewe rafiki yangu,Nilifurahi na kuruka na kutaja jina lake Mungu.........  Ohhh Kuna Watu Na Viatu DUNIANI!!!!!!
 Mhhh si Maneno yagu....... Endelea mwenyewe Mpenzi.....

Jee huyu  Rafiki utamuweka  kwenye Fungu Gani? 
Nyota Ndogo anakubamba/kupenda kazi zake?

"Swahili Na Waswahili" Pamoja Daima.

Friday 5 July 2013

Wa-Afrika na Sherehe zao;Zambian Kitchen Party!!!!!!!








Waungwana;Wa-Afrika na Sherehe zao..hii Kitchen Party ya Wa Zambia na wanaume walikuwepo....
za Waswahili/Tanzania nyingi wanaume hawaingizwi. Nilisikia Waziri Mkuu  Mizengo Pinda aliingia kwenye K/party ya mtoto wake..jee alikosea?
Unafikiri ni kwa nini wanaume hawaingii? kuna sababu za msingi au wanaonewa na kukosa UHONDO? 
 Jee Kichen Party zina faida kwenye maisha ya ndoa au nikutaka kukusanya Zawadi ,Kupata Nafasi ya Wanawake Kujimwaga peke yao au Kuna siri zao?
 Jee kwanini Wanaume hawafanyiwi Kitchen Party/Party za Kufundwa? Au wao wanajua kila kitu kabla ya ndoa?

Swali la Kizushi;Kwanini Wanawake wanapenda Party za Peke yao kuliko Wanaume?

 Karibuni wote kwa Maoni/Ushauri,Tujifunze pamoja na Kuelimishana kwa Upendo

"Swahili Na Waswahili"Pamoja Sana.

Thursday 4 July 2013

KUNDI JIPYA LA MUZIKI LAJA JIJINI, LITAKALO JULIKANA KWA JINA LA NDEGE WATATU


Kutoka kushoto ni Paulyne Zongo, Khadija Mnoga (Kimobitel) na Joan Matovolwa.
Wanamuziki hao watatu na wakongwe nchini ndio wanaounda kundi hilo litakalojulikana kwa jina la NDEGE 3
Kundi la Ndege 3 linaloundwa na wanamuziki wakongwe katika Tasnia ya muziki wa dansi na kizazi kipya Joan matovolwa, Khadija Mnoga (Kimobitel)na Paulyne Zongo, hivi karibuni limeshatoa kibao chake kinachokwenda kwa jina la 'MISUKOSUKO YA MAPENZI' ambacho redio kadhaa nchini zimeanza kukirusha.
MISUKOSUKO YA MAPENZI ni nyimbo ambayo imetungwa kwa umahiri wa hali ya juu, na kuonyesha viwango vya juu katika uimbaji na utunzi.

Kwa sasa Joan Matovolwa na Paulyne Zongo ni wanamuziki huru wakati Khadija Mnoga (Kimobitel) ni mwanamuziki anayeimba katika bendi ya Extra Bongo inayoongozwa na Camarade Ally Choki.



"Swahili Na Waswahili" Wanawake na Maendeleo.

Tuesday 2 July 2013

Mswahili wetu Leo; Da'Tolly Ben..Alianzia wapi na yeye ni Nani?


039
Naitwa Akii Tolly Chawachi,najulikana kama Tolly Ben.Mtoto wa sita wa Mchungaji Benjamin Chawachi na Mama mchungaji Hezeline Chawachi.Nimezaliwa kwenye familia iliyosimama katika nguzo ya kumcha Mungu,Upendo,Umoja ,amani na furaha.Nguzo hizi husimamisha maisha yangu.
Tangu nikiwa mtoto, ni mtu wa kufurahi na kucheka wakati wote.Nilijisika vibaya na kuumia nilipoona mtu akiwa na sura ya huzuni.Niliamini kila mtu anapaswa kuwa na furaha,na nilipata shida kuelewa kwanini watu wengine hawawi na furaha.
Muda wa chakula ulikua muda maalum sana kwa familia yetu.kila mtu alikaa mezani kwaajili ya chakula.Tulikula na kufuraia chakula , Baba na Mama siku zote walikuwa na mambo mengi ya kutusimulia na kutuambia ambayo yalifanya tucheke sana na kufurahi.Kila mtu aliupenda muda wa kula na kuungoja kwa hamu.
Ilijengeka kichwani kwangu kwamba wakati wa kula ni wakati wa kufurahi na kucheka.Jambo ambalo lilinijengea mapenzi na chakula na kunifanya nipende kupika na kula chakula kizuri.Sikupenda kula chakula ambacho hakinifurahishi.
Ingawa nilipenda kupika,  sikujua kwamba nilikua na uwezo mkubwa kwenye sanaa ya chakula hadi pale nilipofika kidato cha tatu na kuchagua kusoma somo la chakula na virutubisho kama somo la ziada. Ujuzi wa awali nilioutoa jikoni kwa mama yangu,na uwezo wangu mkubwa jikoni uliongezeka na kukua kwa kasi ndani ya miaka niliyosoma somo hilo. Nilifanya vizuri sana katika somo hilo na kupata alama “A”katika mtihani wa Taifa.
Nilipokua mtu mzima na kuanza kutembea na kula katika nyumba na familia za ndugu, jamaa na marafiki Niligundua ambavyo watu wengi hupungukiwa na ujuzi wa sanaa ya chakula na ufahamu wa virutubisho vya vyakula.Jambo ambalo linachangia familia zao kutokufurahia chakula.
Ili kukuza furaha ya chakula Katika familia za kitanzania,nilianzisha blog rasmi “TOLLYZKITCHEN’’kwa ajili ya kufundisha sanaa ya chakula ,lengo kuu likiwa ni kuwasaidia watanzania kuboresha mapishi yao nyumbani na kuwaelimisha juu ya virutubisho na lishe ili kuleta furaha na vicheko katika familia kila waketipo kula na kuboresha afya zao
Leo,Kupitia “TOLLYZKITCHEN” nawafikia,nawafundisha na kuwaelimisha maelfu ya Watanzania na watu wengine wazungumzao lugha ya Kiswahili kote duniani.


MALENGO
Moja:Kuboresha mapishi nyumbani
Ingawa Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kwa vyakula vingi, Ufahamu na ujuzi wa kuandaa chakula Bora chenye ladha nzuri,muonekano wakuvutia na wingi wa virutubisho ni mdogo miongoni mwa watanzania.Jiko hili liko hapa kutatua tatizo hilo
Mbili:Kuielimisha jamii juu ya virutubisho vya chakula na umuhimu wake katika mwili.
Elimu ndogo juu virutubisho vya chakula na umuhimu wake katika mwili huwafanya watanzania wengi wale mlo usio kamili,hivyo kusababisha ukosefu wa virutubisho muhim mwilini na kua chanzo cha magonjwa mbalimbali katika jamii.jiko hili hutoa elimu juu ya virutubisho vya chakula na umuhim wake katika mwili.
Tatu:Kukuza matumizi ya bidhaa za chakula zilizosindikwa na kuzalishwa hapa nchini.
Tanzania ni nchi inayozalisha bidhaa nyingi za chakula,bidhaa hizo ni nyingi sana sokoni,lakini Watanzania wengi hupenda kununua na kutumia bidhaa za chakula zitokazo nje ya nchi.Jiko hili linawahimiza watanzania kutumia bidhaa za chakula za hapa nchini kwani bidhaa hozo ni bora na fresh kuliko zile zitokazo nje.
DIRA
Dira ya Tollyzkitchen ni kua jiko linalotoa elimu na mafunzo bora ya upishi,chakula na virutubisho,na kuboresha upishi na ulaji wa virutubisho sahihi vya chakula kwa watanzania na watu watumiao lugha ya Kiswahili.Kuona watanzania wakitumia bidhaa za chakula zinazozalishwa hapa nchini.
DHIMA
  • Kutoa Elimu na mafunzo ya upishi,chakula na lishe bora kwa kupitia,tovuti ,simu,redio ,runinga ,vitabu na mafunzo kwa vitendo.
  • Kutoa ushauri na maelekezo juu ya chakula na lishe kwa makundi maalum
  • Kutoa Elimu juu ya chakula na virutubisho kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari ,kwa kushirikiana na taasisi za elimu
  • Kufundisha na kuelimisha jamii juu ya upishi,vyakula na lishe bora kwa kutumia michezo,mashindano,muziki na sanaa mbalimbali.
  • Kukuza na kuboresha matumizi ya bidhaa za chakula zinazozalishwa hapa nchini kwa kutoa elimu ya uelewa na utambuzi wa bidhaa bora za chakula.
kumjua/kujua kazi zake ingia;

     "Swahili NA Waswahili" Wanawake Na Maendeleo/Kujituma.

Monday 1 July 2013

Waswahili na Vituko;Teacher Wanjiku: Mwalimu wa Kiswahili





Waungwana;Waswahili wa Kenya na Vituko/Ucheshi...
Si kunausemi kucheka kunaongeza Uhai?..Tucheke Pamoja!!!!!!

"Swahili NA Waswahili" Tufurahi Pamoja.

Jikoni Leo;Kuku wa kuokwa na Da'Cecy!!!!!



Waungwana;"Jikoni Leo"ni Mapishi ya KUKU wa Kuokwa..
Mengimsina Fuata na Da'Cecy...

Unaweza kupata meengi hapa;Cecy Lyengi


"Swahili NA Waswahili! Pamoja Sana.