Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!

Thursday 6 December 2012

Jikoni Leo;Tupike Pamoja-Mapishi ya Meat Roll - Recipe of (in Swahili subtitled in english)!!!!!



Waungwana;"Jikoni Leo" ni Tupike Pamoja wametuletea............

Mapishi ya Meat Roll.....


Hakuna kinachoshindikana Kujaribu ndiyo kujifunzaaa...pia usisite kuuliza.

Kujua Meengi ungana na da'Sophi kupitia;
www.tupikepamoja.com/Tupike Pamoja


Mhhhhh Tamu saaaaaana!!!!!!!!!
             
"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana. 

Wednesday 5 December 2012

Nderemo Na Vifijo kwa;Kaka Frank Mungo'ngo' Na da'Levina Kimwaga!!!!![1]

           Da'Levina na Mpambe wake  wakielekea Kanisani.
         kaka Frank na Mpambe wake wakisubiri
  Mmmhhh mmependeza sana
      Wametulia ndani ya Nyumba ya Ibada
   Yaanii wee acha tuu!!!!
        Tuependezaaa Hahahaahaa 
             Viapo..
             Mmmmhhh Mke Mkeo kaka Frank......
   Naona Mchungaji Hiza yupo makini....
                Pingu/Pete...........
         Hahahahah Busu la kwanzaaaaaaa..
   Hahahahahhhhh   Mr&Mrs Mungo'ngo......MUNGU asimamie Ndoa yenu!!!!!!!
     MmePendeza sana Wapendwa... 
Mchungaji Hiza,Wapembe na Ma-Arusi MUNGU  awe nanyi...
     Furahaaaaa
  Mmmhhhh Mmependezaaaaaaaaaaaa...
   Uwiiiiii Tumemalizaaaaa sasa...

      Haya Mr&Mrs Mungo'ngo'
    Nzuriiiiiiii kupita Maelezooooooo...
                 Da'Levina na Wapambe....
      Umenoga dadake!!!!
Pendeza mnoo babake!!!
                   Mapoziii kwa Raha zako.....
          Sasa lazima ujidai babake!!!!!!!
         Safari ya kuelekea Kwenye Ukumbi sasa.....
         Ukumbini.......
    Hapo vipi...Hapo sawa sawiaaaa...Mr&Mrs Mung'ngo'.

Waungwana;Wapendwa wetu kaka Frank na da'Levina, Wameungana kuwa kitu kimoja/Kufunga Ndoa.
Alichokiunganisha MUNGU  Binadamu hawezi kukitenganisha. Sasa ni Bwana na Bibi Mungo'ngo'.


Mimi na Familia Yangu,Tunawatakia kila lililo jema,Baraka,Amani,Upendo,Huruma,Samahani,Asante,Uvumilivu, Muwe Pamoja kwa kila Shida na Raha.Mkazae Matunda Mema.

Picha Zitaendelea Usicheze mbali...

"Swahili NA Waswahili" Pamoja saaaana.

Friday 30 November 2012

Kisa Cha Leo; na Mswahili Emu-Three-Uchungu-wa-mwana-aujuaye-ni-mzazi-31!!!!



Waungwana; Si Mwingine ni Emu wa 3. "Kisa cha Leo" ni Uchungu wa Mwana.....Inaendelea,Si mimi ni yeye  na 

DiaryYangu [Yakeeeee!!!!]



Marejeo: Tukumbuke hiki kisa alikuwa akisimulia yule binti niliyekutana naye akiwa kajiinamia kashika shavu, ….akiwa kasimuliwa na mama yake. Huyu binti kwa hali aliyokuwa nayo, alifikia hadi kukusudia hata kujiua.

Binti aliona kabisa , kuwa maisha kwake hayana thamani tena. Na binadamu anapofikia hapo, ujue kweli kuna jambo…nani asiyependa kuishi, hata yule anayekusudia kujiua, muda roho ikitaka kutoka, huwa anajitahidi kuiondoa ile kamba shingoni, lakini anakuwa keshachelewa, siku yake imeshafika, inabidi aonje umauti…na jamani kutoka kwa roho sio kitu cha mchezo.

Katika kisa hiki utagundua kuwa kuna mwanamama hapo ambaye ana jina hilo hilo, …jina ambalo nilisikia akiitwa huyu binti na mama yake mdogo, wakati namuulizia kuhusu maisha yake, kwanini imetokea hivyo, sasa tuendelee na kisa chetu, ………….

*********

‘Mimi sikujua kabisa huyo baba mlevi ninayeishi naye sio baba yangu wa kunizaa, kumbe alikuwa ni baba wa kufikia, hayo niliyajua baadaye, wakati najiandaa na safari ya kuja kuishi huku Dar, mji ambao kila mmoja kule kijijini alitamani kuja kuishi.

Mama yangu aliniambia huyo baba ndiye aliyekuja kumuokoa pale alipoachwa pale porini…..ili wenzake wafike huko wanapohitajika kwa wakati muafaka, na baadaye watarejea kumchukua, au kumtafutia sehemu ya kumuhifadhi.

Wakati kaachwa pale, akiwa kachoka, kwani mwili ulikuwa hauna nguvu, baada ya safari ndefu, baada ya mapigano, na yeye kujitolea kumsaidia huyo jamaa aaliyeficha sura yake kwa kofia ya ngozi ….na haat kujeruhiwa tena…akawa anatamani kulala tu.

‘Wewe pumzika hapa, na utakula nyama hii…mimi nahitaji huko kwetu haraka, leo najua inawezekana ikawa siku ya mwisho, nimeota kuwa nahitaji haraka sana….na kama ulivyoona, hawa watu walikuja kuniua, lakini tumeweza kuokoka…..ngoja nifike huko nyumbani haraka, halafu nitarudi kuhakikisha kuwa upo mikono salama….’akasema.

‘Sawa wewe nenda tu, na nakutakia mafanikio mema, mungu yupo pamoja na wewe, ila ninachokuomba ni kuhusu mtoto wangu…..naomba siku ukija, uje na mtoto wangu, usije bila ya kuwa na mtoto wangu….’akasema huyo mwanamama.

‘Naahidi nitafanya hivyo…na wewe hakikisha unakuwa salama, usiondoke, hapa, …hapa ni salama zaidi’akasema na akambusu kichwani na kuondoka. Huyu mwanamama alikaa pale kwa muda, halafu akaona akatafute maji ya kuoga, maji yaliyokuwepo pale yalikuwa ni machache, ….........
Endelea kusoma Zaidi,Ingia;http://miram3.blogspot.co.uk/

                           "Swahili NA Waswahili" Pamoja Saaaana.

Wednesday 28 November 2012

Ngoma Africa Band growing stronger and stronger in Europe !!!



Ngoma Africa Band, a German based Tanzanian band is now one of the oldest and most successful Africans bands in Germany.

Many African bands in Europe hardly survive for more than a year. Yet Ngoma Africa Band, founded by Ebrahim Makunja aka Ras Makunja in 1993, is still growing stronger.
The band plays "Bongo Dance", which is a unique combination of traditional and modern Tanzanian rhythms with  Soukous and Rumba. All theirs songs are in Kiswahili.

Ngoma Africa Band has released several successful hits including "Mama Kimwaga" (Sugar Mummy), "Anti-Corruption Squad" and "Apache wacha Pombe" (Stop over drinking).

In 2010 Ngoma Africa Band released a single in praise of Tanzania's President Jakaya Kikwete. The song titled "Jakaya Kikwete 2010" praises Mr. Kikwete's good leadership skills and commitment to fight corruption.

On 12th August 2012, Ngoma Africa Band received the International Diaspora Award (IDA) at the International African Festival Tubingen 2012, Germany, for their hard work in promoting East African music throughout Europe.

Ms. Susan Muyang Tatah, CEO of the International African Festival Tubingen 2012 said Ngoma Africa Band was also chosen for the Award because of their creative performance on stage. It's difficult to resist dancing at their concerts, she said.

This year the band released a new CD titled "Bongo Tambarare" featuring "Supu ya Mawe" and "Uhuru wa Habari". The new release is already dominating air waves in Tanzania.

"Supu ya Mawe" advices the listeners to work hard and be patient while pursuing their objectives in life. It also appeals for generosity towards the needy.

"Uhuru wa Habari" praises African journalists who are bold enough to speak out the truth in environments where freedom of speech is quite limited.

Ngoma Africa Band is famous for staging thrilling shows in festivals in different parts of Europe. The band's joyful female dancers, wearing traditional costumes and dancing vigorously to their tunes, always leave fans asking for more.

Ngoma Africa Band is composed of talented young musicians including soloist Christian Bakotessa aka Chris-B, Said Vuai, Matondo Benda, Jonathan Sousa, Aj Nbongo, Richard Makutima, Bedi Beraca "Bella" and Jessy Ouyah.

For further information about Ngoma Africa Band and to listen to their music, please visitwww.ngoma-africa.com.
By Stephen Ogongo Ongong'a



Watanzania waishio Ujerumani kufanya hafla ya kumuaga Mhe,Balozi Bw.Ahmada Ngemera !!!








Watanzania waishio Ujerumani kufanya hafla ya kumuaga Mhe,Balozi Bw.Ahmada Ngemera !
Jumamosi 08-December 2012 mjini Berlin,Ujerumani



Umoja wa Tanzania Ujerumani (UTU) unaheshima kubwa kutarifu na kuwaomba watanzania wote
wanaoishi ujerumani na jirani ya Ujerumani kuwa umoja wetu tunatarajia kufanya afla ya kumuaga
Mheshimiwa balozi  Bw. Ahmada Ngemera ambaye anamaliza mda wake wa kufanya kazi,
Afla hiyo itafanyika mjini Berlin siku ya Jumamosi tarehe 8.12.2012 .
Mhe.Balozi bwana Ahmada Ngemera amekua balozi wa Tanzania nchini Ujerumani na watanzania
wanaoishi ujerumani watamkumbuka daima Mheshimiwa Balozi Bw.Ahmada Ngemera kwa kuwa
karibu sana na jamii ya watanzania,pia atakumbukwa kwa jitihada zake au kile ambacho watanzania
 wa ujerumani wanachokiita kuasisi Umoja na mshikamano wa watanzania nchi ujerumani,ambapo
 Mhe.Balozi Bw.Ngemera na msaidizi wake Mhe.Bw.Ali Siwa wahamua kuhamasisha watanzania 
waishio Ujerumani kuungana katika kila hali kuanzisha umoja wa mshikamano wa watanzania,kitu 
ambacho mabalozi wengi walishindwa kufanikiwa kufanya labda kwa sababu ya ukubwa wa nchi ya
 ujerumani wa watanzania wanaishi katika miji mbali mbali,lakini kazi hiyo ya kuwaungunganisha 
watanzania, Balozi Bw.Ahmada Ngemera na Msaidizi wake Bw.Ali Siwa walifanikiwa kuwafikia
 watanzania wote waishio Ujerumani na kuwashauri waanzishe umoja wa mshikimano,na matunda
ya juhudi zao ndipo kukazaliwa Umoja wa waTanzania Ujerumani.(UTU)  Umoja ambao ni chombo
 cha watanzania wote ! chombo ambacho watanzania waishio ujerumani wanajivunia !
UMOJA NA MSHIKAMANO NDIO MSINGI WETU IMARA!
OMBI:
TUNAWAOMBA WATANZANIA WOTE ! NA MARAFIKI WOTE WA TANZANIA
AMBAO WANATAKA KUSHIRIKI KATIKA AFLA HII,
TUNAOMBA MTOE MCHANGO WA EURO 20.00 NA KWA WANAFUNZI EURO 10.00 TU
 kwa kupitia Account : Union of Tanzania in German e.V.
VR Bank Rosenheim-Chiemsee AG
Konto-No.: 59641   BLZ: 71160161
Verwendungszweck: „Kumuaga Mhe. Balozi Ngemera


Pia unaweza kuwasiliana na kamati.utu@googlemail.com
simu namba +491734297997 au Katibu simu namba 01734744265 .




Tuesday 27 November 2012

Ya Kale Ni Dhahabu;Burudani-Kanda Bongo Man na Brandy - I Wanna Be Down na Nyingine!!!!!





Waungwana "Ya Kale Ni Dhahabu"  Duuhh Zilipendwa.........Haya unakumbuka nini ukiangalia picha hiyo na Miziki hii....hahahhaa Jamani jamani...

 Jee Ulivaa Loso/Rosooo,Robot/Utanikoma Saa Nane, T-shirt iliandikwa Yes/No, Bareeeet/Kofia,Mungu Usinione/Kofia,Raba Mtoni na sketi ya Jeans..... Mkanda wa Kipepeo,wa Plastiki....ulipaka Ayu/Yolanda....Kunyoa Panki,Push Back..... na..... Ongezea Mwenyeweeeee!!!!!!

Leo Nimewaletea Sister Duuuhhh wa Uhakika.........

Ngoja Niimbe kidogo...........Inde moniiiiiiii  Inde moniiii Inde Inde........eeehhh ukishakula umaaa tingisha umaaaa......

Hahahahaha "Swahili NA Waswahili" Mjumbe Hauawiiiiii.....

yeehhh mayebo yakuporaaaaaa dengu kuchanganya na dengueee dengu na piripiriiii.....

Tutumie Picha zako za Enziii  kupitia; rasca@hotmail.co.uk

  Pamoja Daima.

Sunday 25 November 2012

TAARIFA RASMI YA MSIBA WA MTOTO MARY SHABANI KACHUA KUTOKA CANADA.


Marehemu Mary Shabani Kachua (3 Yrs) enzi za uhai wake.
Familia ya Dr Shabani Kachua kutoka Canada inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao mpendwa Mary Kachua kilichotokea tarehe 19/11/2012 nchini Canada.
Mwili wake uliagwa jana York Funeral Home, Fredericton, NB. Canada na leo kutakuwa na misa maalum Symthe Cathedral Church, Fredericton, NB, Canada.
Familia ya Dr S. Kachua wataondoka leo Canada kuelekea Jijini Dar es salaam Tanzania kwa ajili ya kuupokea mwili na wanatarajiwa kufika kesho jumapili saa 7:30 Mchana kwa ndege ya Ethiopia Airlines.
Mwili wa marehemu Mary Kachua unatarajiwa kufika siku ya Jumatano tarehe 28/11/2012 kwa ndege ya KLM. Shughuli na taratibu za mazishi zinatarajiwa kufanyika nyumbani Tanga mjini.
Kwa mawasiliano zaidi ya taratibu zote za mazishi unaweza ukapiga namba:
+255 784 670866
+255 713 254553
Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahala pema peponi.
Amen