Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Mtanzania/Mswahili. Show all posts
Showing posts with label Mtanzania/Mswahili. Show all posts

Monday 14 August 2017

Mtanzania Ashinda Tuzo ya Mhasibu Kiongozi London 2017


Baada ya kuhitimu Uhasibu na kufanya kazi kwa  bidii na nidhamu Mtanzania Joyce Materego aliteuliwa mmoja wa viongozi bora, London,  karibuni. 
Mahojiano yake na KSTL ,  yadokeza kifupi ilikuwaje




Mhasibu, mkalimani, mzazi, mpenzi wa sanaa na fasihi- mchapa kazi Joyce Materego. Kati ya Watanzania Ughaibuni wenye bidii. Anatueleza jinsi alivyozawadiwa kazini kwake kama mhasibu kiongozi sekta yake, London, 2017.


Kwa Simu Toka London- Na Freddy Macha

Thursday 9 March 2017

Maandalizi Ya TANZANIA DAY 2017 Dallas Texas






Aprili 29, 2016, Mstahiki Meya wa jiji la Dallas, jimbo la Texas aliitangaza rasmi siku hiyo kuwa SIKU YA TANZANIA

Na mwaka huu, Jumuiya ya waTanzania waishio jimboni humo kwa kushirikiana na Baraza la waTanzania waishio nchini Marekani (Diaspora Council of Tanzanians in America) wanaandaa maadhimisho makubwa ya siku hiyo yatakayofanyika katika jiji la Dallas.

Viongozi Ben Kazora wa Jumuiya ya Dallas na Charles Bishota wa DICOTA wamezungumza na Mubelwa Bandio kuhusu maandalizi ya siku hiyo

KARIBU USIKILIZE


Saturday 23 April 2016

FRANK LYIMO APEPERUSHA BENDERA YA TANZANIA MAREKANI, ASHINDA MR. VIRGINIA INTERNATIONAL UNIVERSITY




Frank Lyimo (mwenye vazi la kimasai) mmoja ya Watanzania wanaosoma katika chuo cha kimataifa cha Virginia, ameshinda kwenye shindano la vivazi lililofanyika siku ya Alhamisi April 21, 2016. Vazi lililompa taji hilo ni vazi la kimasai.
Frank Lyimo akiwa katika picha ya pamoja na miss District of Columbia mara tu alipovikwa taji na kuwa Mr. Virginia International University.
Frank Lyimo akiwa katika picha ya pamoja na wanachuo wenzake wa Kitanzania wakipeperusha bendera ya Tanzania chuoni hapo katika kusherehekea ushindi.
Frank Lyimo (kati) akiwa na washiriki wengine.


Thursday 6 August 2015

BALOZI LIBERATA MULAMULA AONDOKA RASMI MAREKANI KURUDI TANZANIA.


 Balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja  na baadhi ya Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC walipokwenda kumuaga nyumbani kwake Bethesda Maryland.




                               Safari ya kuelekea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Dulles ikianza.

 Mhe Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Agnes Mutta Mke wa Mwambata wa Jeshi wa Ubalozi wa Tanzania Washington DC.

Mhe Balozi Liberata Mulamula pamoja na Mkuu wa Utawala Lily Munanka wakibadilishana mawazo pamoja na familia ya Mwambata wa Jeshi.

 Mhe Balozi Liberata Mulamula akiwa pamoja na Mwambata wa Jeshi Col. Adolph Mutta pamoja na Mkewe Agnes Mutta.

               Mhe Balozi Liberata Mulamula akitoa  pasi yake ya kusafiria kwaajili ya kujisajili tayari kwa kuondoka.

                        Mhe Balozi Liberata Mulamula  akiwa katika hatua za mwisho za usajili.

                           Mhe Balozi Liberata Mulamula tayari usajili ulipokamilika

Mhe. Katibu Mkuu Balozi Liberata Mulamula kwenye picha ya pamoja na baadhi ya wafanyakazi wa Ubalozi pamoja na familia zao.

Mhe. Katibu Mkuu Balozi Liberata Mulamula akiwa tayari anajiandaa kwa ukaguzi wa mwisho na kuelekea kwenye ndege.

 Kwa pamoja tunasema Safari Njema na Ubarikiwe Sana Balozi Mulamula daima tutakukumbuka.

                    PICHA ZOTE KWA HISANI YA CAMERA YA UBALOZI.

Tuesday 10 February 2015

Tanzanian Dentist Dr. Talib Ali on the TOP Doctors Interviews - Sedation Dentistry


Dr. Talib Ali, a top dentist from Avatar Dental Care in Leesburg, Virginia, discusses the benefits of Sedation Dentistry on the TOP Doctors Interviews which are seen on CNN Headline News, CNBC, FOX News and other networks. Call Avatar Dental Care Today and set your consultation with Dr. Talib Ali at 703-669-8600 or visit http://www.avatardental.com/ or his office at:

Avatar Dental Care

545 G. East Market Street

Leesburg, VA 20176

Monday 24 March 2014

[AUDIO]: Mdau Boniface Makulilo akijadili suala la Scholarship katika kipindi cha NJE-NDANI‏

Mdau Ernest Makulilo ambaye huandika kuhusu masuala ya Scolarship HAPA na pia kutoa video za suala hili HAPA
UNATAKA SCOLARSHIP?
Unajua pa kuzipata?
Unajua namna ya kuzipata?
Masharti yake je?
Makosa yanayofanywa na wengi?
Tofauti ya Scholarships za Undergraduate na Graduates wazijua?
Yapi ya kuchunga wakati wa kutafuta scholarships?
Boniface Makulilo ambaye amenufaika na scholarship hizi na kuandika kuzihusu kwa miaka ipatayo sita anaungana na Mubelwa Bandio wa Jamii Production kujadili hili.
Kuna mengi mema ya kujifunza.
KARIBU

NJE-NDANI ni kipindi kutoka Jamii Production Washington DC kinachokujia moja kwa moja (LIVE) kila Jumamosi kuanzia saa 6 mpaka 8 mchana (saa za Marekani mashariki) ambacho kinaleta Habari na Taarifa kuhusu yale yanayotokea na kuwagusa waAfrika walio NJE na NDANI ya Afrika.

Tuesday 18 March 2014

IskaJojo Studios; Ilimuhoji Miriam Kinunda Author of Taste of Tanzania Cookbook‏


IskaJojo Studios; Ilimuhoji "Miriam Kinunda" Mwandishi wa kitabu cha mapishi a Taste of Tanzania: Modern Swahili Recipes for the West.
Akieleza historia yake fupi ya kazi na mapishi na mengineo yanayoweza mnufaisha yoyote anayetaka kuandika kitabu na kufanikisha.



Miriam Kinunda - Taste of Tanzania  Na  IskaJoJo Studios 


"Swahili Na Waswahili" Pamoja Sana.

Monday 17 March 2014

Boniface Makulilo azungumzia maisha katika jeshi la Marekani kwenye kipindi cha NJE-NDANI‏

Boniface Makulilo alipokuwa katika Jeshi la Maji la Marekani (Navy)
Mtanzania Boniface Makulilo ametumikia Jeshi la Maji (NAVY) hapa
Marekani kwa miaka miwili na sasa ni mwanajeshi mstaafu (Veteran)

Amezungumza
na Mubelwa Bandio wa Jamii Production kuhusu maisha yake ya jeshini na
namna ambavyo watu toka nje ya nchi wanaweza kunufaika na mafao yaliyopo
jeshini.

Ameeleza mengi ya manufaa ambayo wengi hatuyajui kuhusu maisha katika jeshi hilo.

Karibu uungane nasi

NJE-NDANI ni kipindi kutoka Jamii Production Washington DC kinachokujia moja kwa moja (LIVE) kila Jumamosi kuanzia saa 6 mpaka 8 mchana (saa za Marekani mashariki) ambacho kinaleta Habari na Taarifa kuhusu yale yanayotokea na kuwagusa waAfrika walio NJE na NDANI ya Afrika.

Thursday 30 January 2014

Mswahili Wetu Leo; Tupo Kigoma Tanzania na Fundi Khamiss!!!!




Waungwana,Mswahili Wetu  Leo ;
Tupo Kigoma kwa Fundi Khamiss,Yeye ni Mshonaji na Mbunifuni.

Jee unamtazamo gani na Mafundi Nguo wa [Mitaani/Vibarazani] kwa sasa,Soko lao linazidi kupanda au Linashuka?
Haya tumuunge mkono. Unaweza kuwasiliana naye kupitia:Email;Khamiss@gmail.com,Simu,+255 714481790.
Kuona kazi zake zaidi ingia;http://mitindoafrica-abroad.blogspot.co.uk/

Monday 2 December 2013

[AUDIO]: Maandalizi ya matembezi ya hisani: NCHI YANGU, WAJIBU WANGU, TAIFA KWANZA‏


 Matukio Chuma, muandaaji wa matembezi ya hisani akizungumzia matembezi hayo yatakayofanyika Januari 11, 2014 yenye kauli mbiu Nchi yangu, wajibu wangu, taifa kwanza.

Katika mahojiano haya Chuma anazungumzia mambo mbalimbali kuhusu matembezi hayo, ikiwemo sababu ya kuyaandaa, sababu za kuyafanya katika njia waliyoamua kuyafanya (Dar-Moro), mambo ya kufanya kabla hujashiriki matembezi haya na mengine mengi.

Unaweza kuwasiliana nao kwa simu namba 0784 311-056, 0772 545-562 ama barua pepe ambayo ni kwetutanzania@yahoo.com

--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"

Saturday 19 October 2013

Kukamatwa kwa mtuhumiwa wa mauaji ya Omar Sykes Washington DC‏


Eneo la tukio Washington DC ambapo Omar Sykes (picha ya ndani) aliuawa.
Photo Credits: National Review Online


Jumanne wiki hii, idara ya Polisi Washington DC (Metropolitan Police Department) ilitangaza kukamatwa kwa mtuhumiwa mmoja kati ya wawili waliokuwa wakitafutwa kwa mauaji ya mwanafunzi mTanzania aliyekuwa akisoma katika chuo kikuu cha Howard hapa jijini.

Omar Sykes (22) aliuawa usiku wa Julai 4 mwaka huu nje kidogo ya maeneo ya chuo hicho alipokuwa pamoja na mwenzake.

Wakiwa mtaa mmoja toka chuoni, wanafunzi hao walivamiwa na watu wenye silaha waliotaka kuwapora, na katika harakati hizo, Omar alipigwa risasi
kifuani na kufariki.


Hii ni sehemu ya ripoti ya Jamii Production kwenye kipindi cha DAKIKA 90 ZA DUNIA kinachorushwa na kituo cha Radio cha Capital FM cha Dar Es Salaam Tanzania kila Jumamosi kuanzia saa moja na nusu asubuhi (7:30 AM).



Bahati Alex (L) Capital Radio Jijini Dar es
Salaam na Mubelwa Bandio (R) wa Jamii Production Washington DC


Hii ilikuwa ripoti ya Oktoba 19, 2013



--
*JAMII PRODUCTION*
"Usahihi wa fikra ndio fikra sahihi"


Friday 26 July 2013

Wimbo Toka Kwa Neema Decoras Milele Nitalisifu Jina Lako!!!!



 Ndugu,

 Salamu katika Jina la Yesu Kristo,

 Ninaitwa Neema
 Decoras. Ni muimbaji wa Nyimbo za Injili toka Dar es Salaam, Tanzania.
 Nimeambatanisha wimbo wa kwanza kutoka katika albam yangu, uitwao Milele Nitalisifu Jina Lako na kuutuma kwako ili uusikilize.


 Mashairi ya wimbo huu ni haya yafuatayo:

Kibwagizo (Chorus)
 Milele, Milele, Milele eeee,
 Milele, Milele, Milele
 eeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
 Aaah,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,

 Beti 1
 Hakika Upendo wako, ooooh
 Nashindwa
 kuupima mimi,
 Ulinipenda mimi, iiiih,
 Ukatoa uhai wako,
Yote hii Bwana, aaaah
Uniepushe na mateso,
Yote hii Bwana, aaaah
Uniepushe na kuzimu,
Ukaja duniani, iiiih,
Ukapata mateso mengi,
Ulijishusha sana, aaaah,
 Ili utukomboe sisi,
 Mimi sijaona, aaaah
 Upendo kama wako tena
 Mimi sijaona, aaaah
Upendo kama wako tena
 Nasema, Milele, Milele Nitalisifu Jina Lako

 Kibwagizo
 Milele, Milele, Milele eeeee,
 Milele, Milele, Milele eeeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
 Milele eeee, Milele, Milele eeeee,
  Aaah,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako Bwana,
 Aaaah, Nitalisifu Jina Lako oooh,

 Beti 2
 Niwapo mashakani, iiiih
 Rafiki hunikimbia,
 Niwapo ni mgonjwa, aaaah
 Watu husema pole sana,
 Lakini hawawezi, iiiih
 Kutatua shida zangu,
 Lakini hawawezi, iiiih
 Kutatua shida zangu,
 Peke yako nakuona,
 aaaah
 Waja kunifariji moyo,
 Peke yako nakuona, aaaah
 Waja kutibu afya yangu,
 Peke yako nakuona, aaaah
 Wanitendea miujiza,
 Ndio maana nasema, aaaah
 Una upendo mwingi sana,
 Ndio maana nasema, aaaah
 Una upendo mwingi sana,

 Kibwagizo
 Milele, Milele, Milele eeeee,
 Milele, Milele, Milele eeeee,

Swahili Na Waswahili;Inakutakia kila lililojema,Baraka katika Yote.Hongera Sana da'Neema Decoras.

Friday 5 April 2013

Mswahili Wetu Leo;Joseph Mfugale- Toka fundi seremala mpaka kumiliki Peacock Hotel!!!!!!!

I

Waungwana,Safari ya Maisha ni ndefu sana..Kuna Mabonde na Milima..Kuna Shida na Raha..
Hebu Leo Tumsikilize mzee MFUGALE.

Jee kuna lolote umejifunza?

Shukrani;PAUL MASHAURI

"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana.







Wednesday 2 January 2013

Kitabu Kimojawapo cha Prof.Mbele-Africans and Americans: Embracing Cultural Differences








The book is available at http://www.lulu.com/shop/joseph-mbele/africans-and-americans-embracing-cultur... and other internet sites.
 

Here is a review on Amazon http://www.amazon.com/Africans-And-Americans-Embracing-Differences/dp/1411623...


"Mbele takes on the arduous task of comparing American and African cultural differences, focusing mostly on Tanzanian culture and customs - and he does this in less than 100 pages. Anyone interested in this topic will find mostly anecdotal comments and observations from someone who has spent time on both continents. In the end Mbele notes that people are different and that we should embrace and accommodate our differences as much as possible. This is a good book with good information to consider if you are traveling to Africa anytime soon or hosting an exchange student from Africa.


Kujua Mengi kuhusu Prof.Mbele ingia;Joseph Mbele na http://hapakwetu.blogspot.co.uk/


"Swahili NA Waswahili" Pamoja Sana

Tuesday 23 October 2012

Mswahili Wetu Leo; Arba Manillah wa Kukaye Motooooooo!!!!!!!


 Waungwana;MSwahili Wetu Leo ni  Kaka ARBA  MANILLAH.
Ni mwanamuziki anayeishi na kufanya kazi zake Nchini Ujerumani[Chemnitz, Germany].
Arba Alizaliwa na kukulia IRINGA,TANZANIA.
Bendi yake inaitwa "KUKAYE MOTO"
Kujua zaidi kuhusu kaka huyu ingiaKukaye Moto na www.kukayemoto.de Twende sote sasa....
 "WANYALUKOLO"......Kihesa,Mkimbizi,Semtema,Ruaha,Ipogolo,Kigonzile,Ilala,Lugalo.....................Dar-es-salaam,Ilala,Mabibo....

"Swahili NA Waswahili" IRINGA TO GERMANY.




Monday 8 October 2012

Mpigie kura Jestina mwana wa George!!!!!!


JESTINA-GEORGE.COM HAS BEEN NOMINATED FOR BLOG OF THE YEAR 2012 @ THE PRESTIGIOUS BEFFTA AWARDS. VOTING HAS NOW STARTED & WILL CLOSE ON THE 22ND OF OCTOBER. IT'S EASY AND IT'S ONLINE JUST VISIT http://www.beffta.com/voting.htm FILL IN YOUR NAME, EMAIL ADDRESS, UNDER CATEGORY CLICK NEWS 4. BLOG OF THE YEAR AND UNDER NOMINEE CLICK AND VOTE FOR JESTINA-GEORGE.COM THEN CLICK SUBMIT YOUR VOTE.

PLEASE VOTE FOR YOUR BLOG, OUR BLOG, MY BLOG TO WIN BLOG OF THE YEAR 2012.

Thank you for your support & God bless you.


LOVE YOU ALL
Jestina George

xoxox

Sunday 26 August 2012

Mswahili Wetu Leo;AIKAROSE MWASHA-Anaishi BELGIUM;NYOTA TUMAINI LETU!!!

NYOTA TUMAINI LETU





Jina: AikaRose Mwasha
Jinsia:Kike
Miaka:12
Utaifa:TANZANIA
Mchezo: Taekwando 
KILO: 28 kg- beginners FEMALE
Club: Nong Jang
MAKAZI: Leuven Belgium
MAFANIKIO: MEDALI YA FEDHA & DHAHABU


Kijana wa kitanzania mwenye ndoto ya kuwakilisha nchi yake kwenye mashindano ya kimataifa hapo usoni kwa kupitia mchezo wa mbinu za kujihami wa TAEKWANDO ,anamapenzi makubwa na mchezo huu aliouanza angali mdogo akiwa na umri wa  miaka 9 ,ameshashiriki mashindano madogo madogo nchini Belgium na kupata mafanikio makubwa kufikia medali ya fedha. Hivi karibuni alifanikiwa kupata medali ya dhahabu katika mashindano ya Olympic open Brussels yaliyofanyika Rue Du Lombartzyde Brussels Belgium tarehe  27 May 2012.
Sasa hivi anajiandaa na team yake kwenda Copenhagen kwenye  mashindano ya Wonderfull Copenhagen yatakayofanyika mwezi ujao.
Wito wake hasa kwa vijana wadogo akitilia mkazo jinsia ya kike ni kujifunza michezo mbalimbali na kuwa na ndoto ya kuwa mabalozi kwa taifa lao la TANZANIA.
VIPAJI HUINUA TAIFA

"Swahili NA Waswahili" Tunakutakia kila la kheri.

Wednesday 13 June 2012

TuMpigie Kura Christina SHUSHO;Viva Shusho Viva Tanzania!!!!!!!!

Waungwana;Tumpigieni Kura Christina Shusho aweze kupata tuzo ya Africa Gospel Music Award 2012
Jinsi ya kupiga kura nenda,
www.africagospelawards.com/nominate.html

VIVA SHUSHO, VIVA TANZANIA   "pamoja Tunaweza"

Sunday 10 June 2012

Mswahili wetu Leo;kaka Mod-Med[Mbuko]Raha Jipe mwenyewe!!!!!!

Mswahili Kaka Mbuko akijipa Raha mtaani Huko Holland[Uholanzi],Raha tele Tabu ya nini?

"Swahili na Waswahili" Pamoja sana!!!!