Swahili na Waswahili

Swahili na Waswahili
Waswahili na Mswahili Rachel Siwa...Pamoja Daima!!
Showing posts with label Burudani. Show all posts
Showing posts with label Burudani. Show all posts

Monday 10 September 2012

KHADIJA MNOGA AKA KIMOBITEL AWABIP WAPENZI NA WASHABIKI WA EXTRA BONGO KWA WIMBO WAKE MPYA ALIOUPA JINA LA "MGENI" NDANI YA MEEDA.!!!


Kimobitel akiimba wimbo wake aliyeutunga mwenyewe unaojulikana kwa jina la "MGENI" ndani ya Meeda Sinza Usiku wa kuamkia leo.
Kulia ni Mkurugenzi wa Extra Bongo Ally Choki akiimba wimbo mpya wa Kimobitel ndani ya Meeda Sinza
Banza Stone AKA Generale akifurahi pamoja na Khadija Mnoga AKA Kimobitel wakati wa utambulisho usio rasmi wa ujio wa Kimobitel
Kushoto ni Athanas mwanamuziki anayekuja kwa kasi ndani ya Extra Bongo, akishoo luv na Kimobitel ndani ya Meeda Sinza.
Safu ya wanamuziki nguli wa Extra Bongo walioimba wimbo mpya wa Kimobitel (Mgeni) wakiongozwa na Ally Choki wa pili kutoka kushoto, wa kwanza kulia ni Rogert Hega Katapila, anafuatiwa na Banza Stone na Kushoto ni Kimobitel.

Kimobitel akiwa na nyuso ya furaha baada ya wapenzi na wadau mbali mbali kumpongeza na kumpokea kwa mikono miwili ujio wake.

Khadija Mnoga "Kimobitel" hivi majuzi alitangaza rasmi kuihama Bendi yake ya Twanga Pepeta ambayo aliitumikia kwa miezi kadhaa na kuhamia Extra Bongo, sababu za kuhama Kimobitel alisema ameamua kurudi Extra Bongo kwa sababu kuna mipango yake ambayo aliianzisha kwa hiyo amekuja kuimalizia kama wimbo ambao aliwahi kuimba wakati anaiimbia bendi hiyo unaotambulika kwa jina la "MJINI MIPANGO" kwa hiyo ameamua kurudi kuja kuikamilisha mipango hiyo.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki amesema KIMO KIMO kama wengine wanavyomuita atatambulishwa rasmi siku ya Ijumaa ya tarehe 14/09/2012 katika ukumbi wao wa nyumbani New White House uliyopo Kimara Korogwe jijini Dar es salaam.

Saturday 18 August 2012

MASHUJAA MUSICA NA RATIBA YAO YA SIKUKUU YA IDD EL FITR!!!!!


Martin Sospeter Luhangisa, Meneja wa Mashujaa Bendi
BAADA ya kukamilisha ziara ya kutambulisha wanamuziki wake wapya wa Mashujaa Band, sasa ni zamu ya kuwapa burudani wapenzi wa bendi hiyo kwa siku ya Idd Mosi na Idd Pili.
Meneja wa Bendi hiyo Martin Sospeter alisema kuwa, siku ya Idd mosi watakuwa Msasani kwenye ukumbi wa Emirates.
Sospeter alisema kuwa, siku ya Idd pili watakuwa Mjini Mtwara katika ukumbi wa Makonde Beach ili kuwapa radha wakazi wa huko.
Bendi hiyo ambayo hivi sasa ipo hivi chini ya Rais wake Chalz Baba, itatoa burudani hiyo kwa ajili ya kutangaza kazi zao mpya kwa wapenzi wa nyimbo zao na Bendi yao kwa ujumla.
Alisema, pia kwa wale wanaoisikia Bendi ya Mashujaa kwenye vyombo vya Habari, sasa ndiyo wakati wao wa kuiona bendi hiyo laivu katika Sherehe za Eid El Fitri.
"Kama tulivyowapagawisha wakazi wa Songea na Mbeya wiki iliyopita, sasa ni zamu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na Mtwara," alisema Sospeter.

Thursday 16 August 2012

FFU wa Ngoma Africa band na Mashambulizi yao Tubingen,Ujerumani!!!!!













FFU wa Ngoma Africa band  imewasha moto,TUBINGEN
  
Wamechukua Tuzo ya "IDA-International Diaspora Award"

Bendi maarufu ya muziki wa dansi barani ulaya,Ngoma Africa Band
Siku ya Jumamosi 11.8 .2012 walishambuli jukwaa na la
International Africa Festival 2012,Tubingen,Ujerumani,
na kuhakikishia washabiki kuwa FFU ni tishio la kimataifa !
Kiongozi wa bendi Ras Makunja alikabidhiwa Tuzo ya kimataifa ya
"International Diaspora Award" kwa niaba ya bendi hiyo.

The Ngoma Africa Band

Thursday 2 August 2012

OFFICIAL VIDEO-LEKA DUTIGITE VIDEO-KIGOMA ALL STARS!!!!!!

Kigomaaa Leka Dutigiteee!!!


Haya Waungwana mambo ya Kigoma hayo.Jee nawengine mnakuja kama hivyo?
Dar,Iringa,Tanga,Mwanza,Mbeya na.....................


Waungwana mna  Maoni,Ushauri,Mawazo Gani katika hili?


 LEKA DUTIGITEEE!!!!!!


"SWAHILI na WASWAHILI" Pamoja Daima.


Monday 30 July 2012

GERRY TEGETE, NGASA WASHEREHEKEA UBINGWA PAMOJA NDANI YA WHITE HOUSE KIMARA KOROGWE.!!!!!!


Mwanamuziki nguli wa Bendi ya Mashujaa Musica Chaz Baba akiimba kwa furaha kubwa ndani ya Ukumbi wa White House Kimara Korogwe usiku wa kuamkia leo.

Kutoka kulia Chaz Baba, Mrisho Ngasa Mchezaji wa Azam na Gerry Tegete Mchezaji wa Yanga wakiwa ndani ya viunga vya White House Kimara Korogwe jana baada ya kutoka kwenye Mechi kali baina ya timu zao, ya kombe la Kagame ambayo Yanga waliibuka mabingwa kwa mabao 2 kwa bila.

Kulia Gerry Tegete akishoo luv na Mchezaji mwenzake Mrisho Ngassa anayechezea club ya Azam.

Rapa maarufu wa Bendi ya Mashujaa Fagasoni akiimba ndani ya ukumbi wa White house Kimara Korogwe.


Mpiga tumba namba moja Afrika mashariki MCD akiwakimbiza washabiki wao ndani ya White house Kimara.

Mrisho Ngassa na Chaz Baba wakifurahia kwa pamoja Ushindi waYanga, Mrisho ngassa ni Mshambuliaji mahiri wa Club ya Azam.

Tegete, Henry na kulia Mrisho Ngassa ndani ya White House Kimara.

 kulikulikuwa na mechi ya fainali ya kombe la Kagame kati ya Yanga afrikani na Azam FC ndani ya uwanja wa Taifa ambapo Yanga waliibuka mabingwa

Ngassa na Tegete kwa kuonyesha mpira sio ugomvi walisherehekea pamoja ushindi wa Yanga baada ya mechi katika viwanja vya White House Kimara korogwe wakati bendi ya Mashujaa ilipokuwa inatumbuiza

Monday 16 July 2012

EXTRA BONGO NEXT LEVEL YAWAAGA WAPENZI NA WASHABIKI WAKE KWA SHOW KALI ILIYOSINDIKIZWA NA MATONYA, Q CHIF NA CHID BENZ NDANI YA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE - KIMARA KOROGWE JIJINI DAR ES SALAAM


Mkurugenzi wa Extra Bongo Ally Choki akiimba mbele ya mamia ya washabiki wake jana usiku ndani ya Ukumbi wa New White House Kimara Korogwe

Msanii wa kizazi kipya Bongo Fleva Matonya akiwarusha mashabiki wa Extra bongo usiku wa kuamkia leo ndani ya New white house Kimara Korogwe.

Q chif akiimba kwa hisia kali usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi wa New white house Kimara Korogwe katika show kali ya Extra bongo ya kuwaaga mashabiki wao, usiku wa leo wanaelekea Finland kwa mwaliko rasmi wa kwenda kufanya show kadhaa huko.

Chid Benz kama kawa akiwarusha mashabiki wake.

Matonya na Q Chif

Choki na Chid Benz

Ally Choki akimsikiliza kwa umakini mdhamini mkuu wa Bendi yake Chif Kiumbe, wakati wa show ya kuwaaga washabiki na wapenzi wao iliyofanyika ndani ya ukumbi wa New white house Kimara Korogwe

Saturday 7 July 2012

EXTRA BONGO WAFUNIKA MBAYA KATIKA UZINDUZI WA UKUMBI WAO MPYA NEW WHITE HOUSE A.K.A BONGO RESORT KIMARA KOROGWE NDANI YA JIJI LA DAR ES SALAAM.!!!


Rais wa bendi ya Extra Bongo Ally Choki akiimba mbele ya wapenzi na washabiki wa bendi yake ndani ya ukumbi wao mpya New White House aka Bongo Resort Kimara Korogwe jana.

Rogert Hegga Katapila akiimba mbele ya washabiki wao katika ukumbi wao mpya uliopo Kimara Korogwe Dar es salaam.
Ally Choki na Henry

Mnenguaji mahiri wa Extra bongo akiwapagawisha washabiki wao ndani ya Kimara Korogwe.

Wakata nyonga wa kiume wa Extra Bongo wakiwakimbiza washabiki wao ndani ya ukumbi wao mpya Bongo Resort Kimara Korogwe.

 la Extra Bongo Banza Stone A.K.A Makaveli, Generale akipagawisha wapenzi wao ndani ya White Inn Kimara Korogwe.Jembe

Mwanamuziki wa BAIKOKO akiimba mbele ya washabiki wa Extra Bongo ndani ya Kimara Korogwe.

Tunda Man naye hakuwa nyuma katika kuwaburudisha mashabiki wa Extra Bongo.

Mwanamuzi wa Kizazi kipya Bongo Fleva Sheta akiwakimbiza washabiki wake ndani ya ukumbi mpya wa Extra Bongo katika uzinduzi wa ukumbi huo.

Extra Bongo jana walizindua ukumbi wao mpya New White House a.k.a Bongo resort uliopo kimara Korogwe. Uzinduzi huo ulisindikizwa na kundi la bendi ya taarabu Coast modern Taarab chini ya omary tego na Maua Tego, Tunda Man, Cheta na kundi maarufu la BAIKOKO ambalo linapiga muziki wenye maadhi ya utamaduni wa makabila ya watu kutoka Mkoa wa Tanga.

Thursday 5 July 2012

FFU kupeleka hewani "Bongo Tambarare" na "Supu ya mawe"!!!!!!!!!




    WaTanzania  Kusherekea Saba Saba na CD " BONGO TAMBARARE"
                         Ya Ngoma Africa Band
  
     Nyimbo za "Supu ya Mawe" na "Uhuru wa Habari" Kutinga Redioni


Wakati tunapoelekea katika shamra shamra ya sikuu ya Saba Saba,
watanzania tunafurahia sikuu hii kwa kupata burudani ya raha ya nyimbo
mpya zilizopo katika CD "Bongo Tambarare" kutoka kwa bendi maarufu ya
muziki wa dansi  Ngoma Africa Band aka FFU yenye maskani nchini Ujerumani,
CD hiyonyimbo tatu  "Bongo Tambarare" , "Supu ya Mawe" na "Uhuru wa Habari"
Inasemekana imeshaanza kupiga hodi katika milango ya vituo mbali mbali vya redio
duniani na hapa nyumbani itasikika wakati wowote kuanzia sasa,hili watanzania wenye
Bongo Tambarare yao wapate raha ya muziki.
CD hiyo yenye nyimbo tatu zilizojaa ujumbe wenye furaha na mafunzo kwa jamii,
kama vile "Supu ya Mawe" ni utunzi na  wake kiongozi wa bendi hiyo
kamanda Ras Makunja wa FFU akiimba kwa kushirikiana na mpiga solo
afande Chris-B.
Watanzania tuipokee CD "Bongo Tambarare" na tufurahie Saba Saba kwa 
kupata raha ya "Supu ya Mawe" kutoka kwa Kikosi kazi Ngoma Africa aka FFU.
unaweza kusikiliza pia at www.ngoma-africa.com au http://www.ngoma-africa.com

Sunday 17 June 2012

EXTRA BONGO WAZEE WA KIZIGO WAZIDI KULITIKISA JIJI NDANI YA MEEDA SINZA.




Ally Choki akiwaburudisha washabiki na wapenzi wa Extra Bongo ndani ya Meeda usiku wa kuamkia leo
Choki akichea show na wanenguaji wake wa Extra bongo ndani ya Meeda Sinza.
Banza Stone Mwana wa Masanja - AKA Jenerale akiimba nyimbo yake ndani ya Meeda Sinza.

Mmiliki wa KAPINGAZ Blog Henry Kapinga alikuwepo ndani ya Meeda Sinza, hapa akishoo luv na kuwapa Big Up Ally Choki na Banza Stone wakati Extra Bongo walipokuwa wanapamofu usiku wa kuamkia leo ndani ya ukumbi huo.
Rapa maarufu namba moja Afrika mashariki wa Extra Bongo Kaba Tano akirap ndani ya Meeda Sinza usiku wa kuamkia leo

Saturday 9 June 2012

MASHUJAA MUSICA BENDI WAZIDI KUPAA NDANI YA BUSINESS CENTRE CHINI YA UONGOZI WA CHAZ BABA.




Kiongozi na mwimbaji wa Bendi maarufu wa Mashujaa Chaz Baba jana akizikonga nyoyo za mashabiki wake kwa nyimbo zake mpya ndani ya ukumbi wa Business Centre Maeneo ya makumbusho.
Mpiga tumba maarufu Afrika Mashariki wa Bendi ya Mashujaa MCD akipafomu ndani ya Business Centre jana Usiku.


Maua ya Mashujaa Band yakiwachengua mamia ya washabiki wao ndani ya Business centre jana usiku.

Bendi ya Mashujaa ni moja ya Bendi maarufu Nchini ambazo zinakuja juu katika medani ya muziki wa bendi na kuthamini thamani ya mwanamuziki.
habari zaidi utazipata.KapingaZBlog.

Asanteni.

Wednesday 16 May 2012

Mswahili;SAM MACHOZI - MY ANGEL.{OFFICIAL VIDEO}

Hii ni yenu.....!! ni video yangu ya kwanza kama sam machozi nigependa sana saport zenu wa TZ ili niweze kuipeleka bendera yetu mbele kimataifa zaidi tuamini kama tunaweza na tutaweza mungu yupo na sisi milele amine... ni sam machozi`TO ALL MY BEAUTIFUL PEOPLE...!




Hayo ni Maneno yake kaka Sam Machozi.

Pamoja sana Waungwana!!! Swahili na Waswahili.

Monday 30 April 2012

Wimbo Mpya "Uhuru wa Habari" kutoka Ngoma Africa band aka FFU





                  FFU wa Ngoma Africa Band wameachia Jipya "Uhuru wa Habari"
                  Unasikika at www.ngoma-africa.com


Kwa kawaida wanahabari na vyombo vyao ndio wanarusha hewani habari za
matukio mbali mbali pamoja wasanii na burudani zao kwa jamii,
Lakini bendi maarufu Ngoma Africa aka FFU imewageuzia kibao !!
Kuliweka hewani song jipya "Uhuru wa habari" wimbo huo mpya
utunzi wake kamanda Ras Makunja akiimba kwa kushirikiana na
kijana Christian Bakotessa aka Chris-B,ambaye pia ni mpiga
gitaa la solo(mtutu) wa kikosi kazi iko.
Bendi hiyo maarufu Ngoma Africa yenye makao yake kule ujerumani,
miezi michache tu iliachia hewani CD ya "Miaka 50 ya Uhuru" na sasa
wanarusha hewani "Uhuru wa habari" ,
Taarifa za kuhaminika zinaeleza kuwa Remix ya wimbo huo pia itakua
hewani siku za usoni,katika Remix hiyo kutakua na majina mengi ya wa
dau wa habari ambao wanachangia kuijulisha jamii habari mbali mbali.
Sikiliza na pata burudani ya bure katika ffu camp at www.ngoma-africa.com
au http://www.ngoma-africa.com